-
Mathayo 22:15-22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Ndipo Mafarisayo wakaenda kupanga njama pamoja ili wamtege Yesu kwa maneno yake.+ 16 Basi wakawatuma wanafunzi wao kwake, pamoja na wafuasi wa chama cha Herode.+ Wakamwambia: “Mwalimu, tunajua wewe husema ukweli nawe hufundisha njia ya Mungu katika kweli, na hutafuti kibali cha yeyote, kwa maana huangalii sura ya nje ya mtu. 17 Basi tuambie, unaonaje? Je, ni halali* au si halali kumlipa Kaisari kodi?”* 18 Lakini Yesu akijua uovu wao, akasema: “Kwa nini mnanijaribu, ninyi wanafiki? 19 Nionyesheni sarafu ya kodi.” Wakamletea dinari.* 20 Akawauliza: “Sura hii na maandishi haya ni ya nani?” 21 Wakajibu: “Ni ya Kaisari.” Ndipo akawaambia: “Basi, mlipeni Kaisari vitu vya Kaisari, na Mungu vitu vya Mungu.”+ 22 Waliposikia hilo, wakashangaa, wakamwacha na kwenda zao.
-
-
Marko 12:13-17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 Kisha wakawatuma baadhi ya Mafarisayo na wafuasi wa chama cha Herode ili wamnase kwa maneno yake.+ 14 Walipofika wakamwambia: “Mwalimu, tunajua wewe husema ukweli na hutafuti kibali cha yeyote, kwa maana huangalii sura ya nje ya mtu, bali unafundisha njia ya Mungu kupatana na kweli. Je, ni halali* au si halali kumlipa Kaisari kodi?* 15 Je, tunapaswa kulipa, au hatupaswi kulipa?” Akagundua unafiki wao, akawaambia: “Kwa nini mnanijaribu? Nileteeni dinari* niitazame.” 16 Wakaleta dinari moja, akawauliza: “Sura hii na maandishi haya ni ya nani?” Wakajibu: “Ni ya Kaisari.” 17 Ndipo Yesu akasema: “Mlipeni Kaisari vitu vya Kaisari,+ na Mungu vitu vya Mungu.”+ Nao wakashangazwa naye.
-