Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 26:69-75
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 69 Basi Petro alikuwa ameketi nje katika ua, kijakazi akamjia na kumwambia: “Hata wewe ulikuwa pamoja na Yesu Mgalilaya!”+ 70 Lakini akakana mbele yao wote, akisema: “Sijui unachosema.” 71 Alipoenda kwenye chumba kilicho langoni, msichana mwingine akamwona na kuwaambia wale waliokuwa hapo: “Mtu huyu alikuwa pamoja na Yesu Mnazareti.”+ 72 Akakana tena akiapa: “Simjui mtu huyo!” 73 Baada ya muda mfupi wale waliokuwa wamesimama hapo wakaja na kumwambia Petro: “Hakika wewe pia ni mmoja wao, kwa maana matamshi* yako yanakutambulisha.” 74 Ndipo akaanza kulaani na kuapa: “Simjui mtu huyo!” Na mara moja jogoo akawika. 75 Naye Petro akakumbuka maneno aliyosema Yesu, yaani: “Kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”+ Naye akaenda nje akalia kwa uchungu.

  • Marko 14:66-72
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 66 Sasa Petro alipokuwa chini katika ua, mmoja wa wajakazi wa kuhani mkuu akaja.+ 67 Alipomwona Petro akiota moto, akamtazama moja kwa moja na kusema: “Hata wewe ulikuwa pamoja na Yesu Mnazareti.” 68 Lakini akakana, akisema: “Simjui wala sielewi unachosema.” Kisha akatoka na kuelekea langoni.* 69 Yule kijakazi alipomwona akaanza tena kuwaambia wale waliosimama hapo: “Huyu ni mmoja wao.” 70 Petro akakana tena. Baada ya muda mfupi, wale waliosimama hapo wakaanza tena kumwambia: “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana, wewe ni Mgalilaya.” 71 Lakini akaanza kulaani na kuapa: “Simjui mtu huyu mnayezungumza kumhusu!” 72 Papo hapo jogoo akawika mara ya pili,+ naye Petro akakumbuka maneno ambayo Yesu alimwambia: “Kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu.”+ Naye akalemewa akaanza kulia.

  • Yohana 18:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Sasa wale watumwa na maofisa walikuwa wamesimama kuzunguka moto wa makaa waliokuwa wameuwasha, kwa sababu kulikuwa na baridi nao walikuwa wakiota moto. Petro pia alikuwa amesimama pamoja nao akiota moto.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki