Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 26:69-75
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 69 Basi Petro alikuwa ameketi nje katika ua, kijakazi akamjia na kumwambia: “Hata wewe ulikuwa pamoja na Yesu Mgalilaya!”+ 70 Lakini akakana mbele yao wote, akisema: “Sijui unachosema.” 71 Alipoenda kwenye chumba kilicho langoni, msichana mwingine akamwona na kuwaambia wale waliokuwa hapo: “Mtu huyu alikuwa pamoja na Yesu Mnazareti.”+ 72 Akakana tena akiapa: “Simjui mtu huyo!” 73 Baada ya muda mfupi wale waliokuwa wamesimama hapo wakaja na kumwambia Petro: “Hakika wewe pia ni mmoja wao, kwa maana matamshi* yako yanakutambulisha.” 74 Ndipo akaanza kulaani na kuapa: “Simjui mtu huyo!” Na mara moja jogoo akawika. 75 Naye Petro akakumbuka maneno aliyosema Yesu, yaani: “Kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”+ Naye akaenda nje akalia kwa uchungu.

  • Luka 22:55-62
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 55 Walipowasha moto katikati ya ua na kuketi chini pamoja, Petro alikuwa ameketi miongoni mwao.+ 56 Lakini kijakazi mmoja akamwona Petro akiwa ameketi kando ya moto, akamtazama kwa makini na kusema: “Mtu huyu pia alikuwa pamoja naye.” 57 Lakini Petro akakana, akisema: “Wewe mwanamke, mimi simjui.” 58 Baadaye kidogo mtu mwingine akamwona na kusema: “Wewe pia ni mmoja wao.” Lakini Petro akasema: “Mimi si mmoja wao.”+ 59 Baada ya saa moja hivi kupita mwanamume mwingine akaanza kusisitiza kwa nguvu: “Kwa hakika mtu huyu pia alikuwa pamoja naye, kwa maana, yeye ni Mgalilaya!” 60 Lakini Petro akasema: “Wewe mtu, mimi sielewi unachosema.” Mara tu alipokuwa akisema, jogoo akawika. 61 Ndipo Bwana akageuka, akamtazama Petro moja kwa moja, naye Petro akakumbuka maneno ambayo Bwana alimwambia: “Kabla jogoo hajawika leo, utanikana mara tatu.”+ 62 Naye akaenda nje akalia kwa uchungu.

  • Yohana 18:25, 26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 Sasa Simoni Petro alikuwa amesimama hapo akiota moto. Ndipo wakamwambia: “Wewe pia ni mmoja wa wanafunzi wake, sivyo?” Akakana na kusema: “Hapana.”+ 26 Mmoja wa watumwa wa kuhani mkuu, aliyekuwa mtu wa ukoo wa yule aliyekatwa sikio+ na Petro, akasema: “Nilikuona katika bustani pamoja naye, sivyo?”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki