28 Kisha nitaimimina roho yangu+ juu ya kila aina ya mwili,
Na wana wenu na mabinti wenu watatoa unabii,
Na wanaume wenu wazee wataota ndoto,
Na wanaume wenu vijana wataona maono.+
29 Na hata juu ya watumwa wangu wa kiume na watumwa wa kike
Nitaimimina roho yangu siku hizo.
30 Nami nitafanya mambo ya ajabu mbinguni na duniani,
Damu na moto na nguzo za moshi.+
31 Jua litatiwa giza na mwezi utatiwa damu+
Kabla ya kuja kwa ile siku ya Yehova iliyo kuu na yenye kuogopesha.+
32 Na kila mtu anayeliitia jina la Yehova ataokolewa;+
Kwa maana kwenye Mlima Sayuni na katika Yerusalemu kutakuwa na wale wanaosalimika,+ kama Yehova alivyosema,
Waokokaji wanaoitwa na Yehova.”