8 Ninamweka Yehova mbele yangu daima.+
Kwa sababu yuko mkono wangu wa kulia, sitatikiswa kamwe.+
9 Kwa hiyo moyo wangu unashangilia, nafsi yangu yote ina shangwe.
Nami ninaishi kwa usalama.
10 Kwa maana hutaniacha Kaburini.+
Hutamruhusu mshikamanifu wako aone shimo.+
11 Unanijulisha njia ya uzima.+
Shangwe tele iko mbele zako;+
Kuna furaha kwenye mkono wako wa kuume milele.