-
Yeremia 31:31-34Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
31 “Tazama! Siku zinakuja,” asema Yehova, “nitakapofanya agano jipya pamoja na nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda.+ 32 Halitakuwa kama agano nililofanya pamoja na mababu zao siku niliyowashika mkono na kuwaongoza kutoka nchini Misri,+ ‘agano langu ambalo walilivunja,+ ingawa nilikuwa bwana* wao wa kweli,’ asema Yehova.”
33 “Kwa maana hili ndilo agano nitakalofanya pamoja na nyumba ya Israeli baada ya siku hizo,” asema Yehova. “Nitaitia sheria yangu ndani yao,+ nami nitaiandika katika moyo wao.+ Nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”+
34 “Nao hawatafundishana tena kila mtu na jirani yake na kila mtu na ndugu yake, wakisema, ‘Mjue Yehova!’+ kwa maana wote watanijua, kuanzia mdogo zaidi mpaka mkubwa zaidi kati yao,”+ asema Yehova. “Kwa maana nitalisamehe kosa lao, nami sitaikumbuka tena dhambi yao.”+
-