Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 26:27, 28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Kisha akachukua kikombe, akashukuru na kuwapa akisema: “Kunyweni ninyi nyote,+ 28 kwa maana hii inamaanisha ‘damu yangu+ ya agano,’+ ambayo itamwagwa kwa ajili ya wengi+ ili wasamehewe dhambi.+

  • Luka 22:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Pia, akafanya vivyo hivyo na kile kikombe baada ya wao kula mlo wa jioni, akisema: “Kikombe hiki kinamaanisha agano jipya+ kwa msingi wa damu yangu,+ ambayo itamwagwa kwa ajili yenu.+

  • 1 Wakorintho 11:25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 Akafanya vivyo hivyo na kile kikombe+ pia, baada ya wao kula mlo wa jioni, akisema: “Kikombe hiki kinamaanisha agano+ jipya kwa msingi wa damu yangu.+ Endeleeni kufanya hivi, kila mara mnapokinywa, kwa kunikumbuka mimi.”+

  • Waebrania 8:8-12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Kwa maana anaona hatia ya watu anaposema: “‘Tazama! Siku zinakuja,’ asema Yehova,* ‘nitakapofanya agano jipya pamoja na nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda. 9 Halitakuwa kama agano nililofanya pamoja na mababu zao siku niliyowashika mkono na kuwaongoza kutoka nchini Misri,+ kwa sababu hawakuendelea kulishika agano langu, basi nikaacha kuwajali,’ asema Yehova.*

      10 “‘Kwa maana hili ndilo agano nitakalofanya pamoja na nyumba ya Israeli baada ya siku hizo,’ asema Yehova.* ‘Nitazitia sheria zangu katika akili yao, nami nitaziandika katika mioyo yao.+ Nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.+

      11 “‘Nao hawatafundishana tena kila mtu na raia mwenzake na kila mtu na ndugu yake, wakisema: “Mjue Yehova!”* Kwa maana wote watanijua, kuanzia mdogo zaidi mpaka aliye mkubwa zaidi miongoni mwao. 12 Kwa maana nitaonyesha rehema kwa matendo yao yasiyo ya uadilifu, nami sitazikumbuka tena dhambi zao.’”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki