-
Waebrania 8:8-12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Kwa maana anaona hatia ya watu anaposema: “‘Tazama! Siku zinakuja,’ asema Yehova,* ‘nitakapofanya agano jipya pamoja na nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda. 9 Halitakuwa kama agano nililofanya pamoja na mababu zao siku niliyowashika mkono na kuwaongoza kutoka nchini Misri,+ kwa sababu hawakuendelea kulishika agano langu, basi nikaacha kuwajali,’ asema Yehova.*
10 “‘Kwa maana hili ndilo agano nitakalofanya pamoja na nyumba ya Israeli baada ya siku hizo,’ asema Yehova.* ‘Nitazitia sheria zangu katika akili yao, nami nitaziandika katika mioyo yao.+ Nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.+
11 “‘Nao hawatafundishana tena kila mtu na raia mwenzake na kila mtu na ndugu yake, wakisema: “Mjue Yehova!”* Kwa maana wote watanijua, kuanzia mdogo zaidi mpaka aliye mkubwa zaidi miongoni mwao. 12 Kwa maana nitaonyesha rehema kwa matendo yao yasiyo ya uadilifu, nami sitazikumbuka tena dhambi zao.’”+
-