Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 33:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Nami nitawatakasa kutokana na hatia yote ya dhambi walizonitendea,+ nami nitasamehe hatia yote ya dhambi zao na makosa waliyonikosea.+

  • Yeremia 50:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 “Siku hizo na wakati huo,” asema Yehova,

      “Hatia ya Israeli itatafutwa,

      Lakini hakutakuwa na hatia yoyote,

      Na dhambi za Yuda hazitapatikana,

      Kwa maana nitawasamehe wale nitakaowaacha wabaki.”+

  • Mathayo 26:27, 28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Kisha akachukua kikombe, akashukuru na kuwapa akisema: “Kunyweni ninyi nyote,+ 28 kwa maana hii inamaanisha ‘damu yangu+ ya agano,’+ ambayo itamwagwa kwa ajili ya wengi+ ili wasamehewe dhambi.+

  • Waebrania 8:10-12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 “‘Kwa maana hili ndilo agano nitakalofanya pamoja na nyumba ya Israeli baada ya siku hizo,’ asema Yehova.* ‘Nitazitia sheria zangu katika akili yao, nami nitaziandika katika mioyo yao.+ Nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.+

      11 “‘Nao hawatafundishana tena kila mtu na raia mwenzake na kila mtu na ndugu yake, wakisema: “Mjue Yehova!”* Kwa maana wote watanijua, kuanzia mdogo zaidi mpaka aliye mkubwa zaidi miongoni mwao. 12 Kwa maana nitaonyesha rehema kwa matendo yao yasiyo ya uadilifu, nami sitazikumbuka tena dhambi zao.’”+

  • Waebrania 9:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Hiyo ndiyo sababu yeye ni mpatanishi wa agano jipya,+ ili kwa sababu kifo kimetokea kusudi waachiliwe huru kupitia fidia+ kutoka kwenye makosa chini ya agano la zamani, wale ambao wameitwa waipokee ahadi ya urithi unaodumu milele.+

  • Waebrania 10:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Kisha inasema: “Nami sitazikumbuka tena dhambi zao na matendo yao ya kuasi sheria.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki