-
Zaburi 95:7-11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
Leo ikiwa mtaisikiliza sauti yake,+
8 Msiufanye moyo wenu kuwa mgumu kama mlivyofanya kule Meriba,*+
Kama katika siku ya Masa* kule nyikani,+
9 Mababu zenu waliponijaribu;+
Walinipima, ingawa walikuwa wameona matendo yangu.+
10 Kwa miaka 40 nilichukizwa na kizazi hicho, nikasema:
“Wao ni watu wanaopotoka sikuzote katika mioyo yao;
Hawajazijua njia zangu.”
11 Kwa hiyo niliapa kwa hasira yangu:
“Hawataingia katika pumziko langu.”+
-