Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 17:2-5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 “Ikiwa mwanamume au mwanamke atapatikana miongoni mwenu, katika mojawapo ya majiji ambayo Yehova Mungu wenu anawapa, aliye na mazoea ya kufanya uovu machoni pa Yehova Mungu wenu na kuvunja agano lake,+ 3 naye anapotoka na kuabudu miungu mingine na kuiinamia miungu hiyo au jua au mwezi au jeshi lote la mbinguni,+ jambo ambalo sijaamuru,+ 4 ukiambiwa au kusikia habari hiyo, unapaswa kuchunguza jambo hilo kikamili. Ikithibitishwa ni kweli+ kwamba jambo hilo lenye kuchukiza limefanywa katika Israeli, 5 utamtoa nje ya malango ya jiji lenu mwanamume au mwanamke ambaye amefanya uovu huo, na lazima mwanamume au mwanamke huyo auawe kwa kupigwa mawe.+

  • Waroma 16:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Sasa ninawahimiza ninyi, akina ndugu, waangalieni wale wanaosababisha migawanyiko na kuweka vikwazo kinyume cha fundisho ambalo mmejifunza, nanyi mjiepushe nao.+

  • 1 Wakorintho 5:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Lakini sasa ninawaandikia mwache kushirikiana*+ na mtu yeyote anayeitwa ndugu ambaye ni mwasherati* au mtu mwenye pupa+ au anayeabudu sanamu au mtukanaji* au mlevi+ au mnyang’anyi,+ hata msile chakula pamoja na mtu wa namna hiyo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki