147 Msifuni Yah!
Ni vema kumwimbia sifa Mungu wetu;
Jinsi inavyopendeza na jinsi inavyofaa sana kumsifu yeye!+
 2 Yehova analijenga Yerusalemu;+
Huwakusanya pamoja watu wa Israeli waliotawanywa.+
 3 Huwaponya waliovunjika moyo;
Huyafunga majeraha yao.
 4 Huhesabu idadi ya nyota;
Zote anaziita kwa majina.+
 5 Bwana wetu ni mkuu naye ana nguvu nyingi;+
Uelewaji wake haupimiki.+
 6 Yehova huwainua wapole,+
Lakini huwatupa chini waovu.
 7 Mwimbieni Yehova kwa shukrani;
Mwimbieni sifa Mungu wetu kwa kinubi,
 8 Yeye anayezifunika mbingu kwa mawingu,
Yeye anayeiletea dunia mvua,+
Yeye anayechipusha majani+ milimani.
 9 Anawapa wanyama chakula,+
Kunguru wachanga wanaokililia.+
10 Hapendezwi na nguvu za farasi;+
Wala havutiwi na miguu yenye nguvu ya mwanamume.+
11 Yehova anafurahishwa na wale wanaomwogopa,+
Wale wanaongojea upendo wake mshikamanifu.+
12 Mtukuze Yehova, Ee Yerusalemu.
Msifu Mungu wako, Ee Sayuni.
13 Huyafanya makomeo ya malango ya jiji lako yawe imara;
Huwabariki wana wako walio ndani yako.
14 Huleta amani katika eneo lako;+
Hukushibisha kwa ngano bora kabisa.+
15 Huituma amri yake duniani;
Neno lake hukimbia upesi sana.
16 Hutoa theluji kama sufu;+
Hutawanya theluji nyembamba kama majivu tu.+
17 Huyatupa chini mawe yake ya mvua kama chembe za mkate.+
Ni nani anayeweza kustahimili baridi yake?+
18 Hulituma neno lake, nayo inayeyuka.
Huufanya upepo wake uvume,+ maji yanatiririka.
19 Anamtangazia Yakobo neno lake,
Na Israeli masharti yake na hukumu zake.+
20 Hajalifanyia hivyo taifa lingine lolote;+
Hawajui lolote kuhusu hukumu zake.
Msifuni Yah!+