Kwa kiongozi; uimbwe kwa vinanda. Maskili. Wa Daudi, Wazifu walipokuja na kumwambia Sauli: “Daudi anajificha miongoni mwetu.”+
54 Ee Mungu, niokoe kwa jina lako,+
Na unitetee+ kwa nguvu zako.
 2 Ee Mungu, isikie sala yangu;+
Sikiliza maneno ya kinywa changu.
 3 Kwa maana wageni wanainuka dhidi yangu,
Na wanaume wakatili wanatafuta uhai wangu.+
Hawamheshimu Mungu.+ (Sela)
 4 Tazama! Mungu ni msaidizi wangu;+
Yehova yuko pamoja na wale wanaonitegemeza.
 5 Utawalipa maadui wangu+ uovu wao wenyewe;
Katika uaminifu wako, waangamize.+
 6 Nitakutolea dhabihu+ kwa hiari.
Nitalisifu jina lako, Ee Yehova, kwa maana ni jema.+
 7 Kwa maana wewe huniokoa kutoka katika kila taabu,+
Nami nitawatazama maadui wangu wakishindwa.+