Isaya
31 Ole wao wanaoshuka kwenda Misri kutafuta msaada,+
Wanaotegemea farasi,+
Wanaotumaini magari ya vita kwa sababu ni mengi,
Na farasi wa vita* kwa sababu wana nguvu.
Lakini hawamtegemei Mtakatifu wa Israeli,
Na hawamtafuti Yehova.
2 Lakini yeye pia ana hekima na ataleta msiba,
Naye hatayabatilisha maneno yake.
Atainuka dhidi ya nyumba ya watenda maovu
Na dhidi ya wale wanaowasaidia wakosaji.+
Yehova atakapounyoosha mkono wake,
Yeyote atakayetoa msaada atajikwaa
Na yeyote atakayesaidiwa ataanguka;
Wote wataangamia wakati mmoja.
4 Kwa maana Yehova ameniambia hivi:
“Kama simba anavyonguruma, mwanasimba mwenye nguvu,* juu ya mawindo yake,
Kundi lote la wachungaji linapokusanywa kupigana naye,
Naye haogopi sauti yao
Au kutishwa na kelele zao,
Ndivyo Yehova wa majeshi atakavyoshuka ili kupigana vita
Juu ya Mlima Sayuni na juu ya kilima chake.
5 Kama ndege wanaoshuka kwa ghafla, ndivyo Yehova wa majeshi atakavyolilinda Yerusalemu.+
Atalilinda na kuliokoa.
Atalihifadhi na kuliokoa.”
6 “Rudini kwa Yule ambaye mmemwasi bila aibu, enyi watu wa Israeli.+ 7 Kwa maana siku hiyo kila mmoja ataikataa miungu yake ya ubatili ya fedha na miungu yake ya dhahabu ambayo haina thamani, ambayo mikono yenu wenyewe ilitenda dhambi kwa kuitengeneza.
8 Na Mwashuru atauawa kwa upanga, lakini si wa mwanadamu;+
Na upanga, usio wa mwanadamu, utamwangamiza.
Atakimbia kwa sababu ya upanga,
Na wanaume wake vijana watalazimishwa kufanya kazi za kulazimishwa.