Isaya
31 Ole wao wanaoshuka kwenda Misri kutafuta usaidizi,+ wale wanaotegemea farasi+ ambao si kitu, na wanaotegemea magari ya vita,+ kwa sababu ni mengi, na kutegemea farasi wa vita, kwa sababu wana nguvu sana, lakini ambao hawakumtazama Mtakatifu wa Israeli wala kumtafuta Yehova mwenyewe.+ 2 Na yeye pia ana hekima+ na ataleta msiba,+ naye hakuyatangua maneno yake;+ na hakika yeye atasimama kushindana na nyumba ya watenda-maovu+ na kushindana na usaidizi wa wale wanaozoea kufanya mambo yenye kudhuru.+
3 Hata hivyo, Wamisri ni watu wa udongo,+ wala si Mungu; na farasi wao ni nyama,+ wala si roho. Na Yehova mwenyewe atanyoosha mkono wake, na yeye anayetoa usaidizi atajikwaa, na yeye anayesaidiwa ataanguka,+ nao wote watafikia mwisho wakati mmoja.
4 Kwa maana Yehova ameniambia hivi: “Kama simba anavyonguruma, mwana-simba mwenye manyoya shingoni,+ juu ya mawindo yake, wakati hesabu kamili ya wachungaji wanapokusanywa kupigana naye, na ijapokuwa sauti yao yeye haingiwi na woga na ijapokuwa kelele zao yeye hatainama; vivyo hivyo Yehova wa majeshi atashuka ili kupiga vita juu ya Mlima Sayuni na juu ya kilima chake.+ 5 Kama ndege wanaoruka, vivyo hivyo Yehova wa majeshi atamlinda Yerusalemu.+ Atamlinda, yeye pia hakika atamkomboa.+ Atamwokoa, pia atamponya.”
6 “Rudini+ kwake Yeye ambaye wana wa Israeli wamemwasi kabisa.+ 7 Kwa maana katika siku hiyo watakataa kila mmoja miungu yake ya fedha isiyo na thamani na miungu yake ya dhahabu isiyo na thamani,+ ambayo mikono yenu imewafanyizia ninyi kuwa dhambi.+ 8 Na Mwashuru ataanguka kwa upanga, si ule wa mwanadamu; na upanga, si ule wa mtu wa udongo, utamla.+ Naye atakimbia kwa sababu ya upanga, na wanaume wake vijana watafanyishwa kazi ya kulazimishwa. 9 Na mwamba wake mwenyewe utapitilia mbali kwa sababu ya woga mtupu, na kwa sababu ya ishara+ wakuu wake wataingiwa na woga,” asema Yehova, ambaye nuru yake iko katika Sayuni na ambaye tanuru+ yake iko katika Yerusalemu.