Wimbo wa Safari za Kupanda.
126 Yehova alipowakusanya na kuwarudisha mateka wa Sayuni,+
Tulifikiri tunaota ndoto.
 2 Wakati huo kinywa chetu kilijaa kicheko
Na ulimi wetu kelele za shangwe.+
Wakati huo ilisemwa miongoni mwa mataifa:
“Yehova amewatendea mambo makuu.”+
 3 Yehova ametutendea mambo makuu,+
Nasi tuna shangwe nyingi sana.
 4 Wakusanye na kuwarudisha watu wetu waliotekwa, Ee Yehova,
Kama vijito vya Negebu.
 5 Wale wanaopanda mbegu kwa machozi
Watavuna kwa kelele za shangwe.
 6 Yule anayetoka kwenda nje, ingawa analia,
Akiwa amebeba mfuko wake uliojaa mbegu,
Kwa hakika atarudi kwa kelele za shangwe,+
Akiwa amebeba masuke yake.+