Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Mambo ya Nyakati 16
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

2 Mambo ya Nyakati—Yaliyomo

      • Asa afanya mkataba na Siria (1-6)

      • Hanani amkemea Asa (7-10)

      • Kifo cha Asa (11-14)

2 Mambo ya Nyakati 16:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kuimarisha; kujenga upya.”

  • *

    Au “asiondoke wala kuingia katika eneo la.”

Marejeo

  • +1Fa 15:25, 27
  • +Yos 18:21, 25
  • +1Fa 15:17-19

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    8/15/2012, uku. 10

  • Fahirishi ya Machapisho

    w12 8/15 10

2 Mambo ya Nyakati 16:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “jumba la.”

Marejeo

  • +1Fa 7:51
  • +1Fa 20:1; 2Fa 12:18; 16:8

2 Mambo ya Nyakati 16:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “agano.”

  • *

    Au “agano lako.”

2 Mambo ya Nyakati 16:4

Marejeo

  • +2Fa 15:29
  • +Amu 18:29
  • +1Fa 15:20-22

2 Mambo ya Nyakati 16:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kuimarisha; kujenga upya.”

2 Mambo ya Nyakati 16:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kuimarisha; kujenga upya.”

Marejeo

  • +Yos 18:21, 25; 1Fa 15:17
  • +Yos 18:21, 24; 1Nya 6:60, 64
  • +Yos 18:21, 26; Amu 20:1

2 Mambo ya Nyakati 16:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “ulimwegemea.”

  • *

    Tnn., “hukumwegemea.”

Marejeo

  • +1Fa 16:1; 2Nya 19:2; 20:34
  • +Yer 17:5

2 Mambo ya Nyakati 16:8

Marejeo

  • +2Nya 14:9, 11; Zb 37:39, 40

2 Mambo ya Nyakati 16:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “utegemezo wake.”

  • *

    Au “una ujitoaji kamili.”

Marejeo

  • +Zek 4:10
  • +1Pe 3:12
  • +1Fa 15:32

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mkaribie Yehova, kur. 42-43

    Mnara wa Mlinzi,

    10/15/2002, uku. 14

  • Fahirishi ya Machapisho

    w02 10/15 14; cl 42-43

2 Mambo ya Nyakati 16:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “katika nyumba ya mikatale.”

2 Mambo ya Nyakati 16:11

Marejeo

  • +1Fa 15:23

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    3/15/2009, uku. 32

  • Fahirishi ya Machapisho

    w09 3/15 32

2 Mambo ya Nyakati 16:12

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    8/15/2012, uku. 10

  • Fahirishi ya Machapisho

    w12 8/15 10

2 Mambo ya Nyakati 16:13

Marejeo

  • +1Fa 15:24

2 Mambo ya Nyakati 16:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “marhamu.”

  • *

    Inaonekana kwamba hawakuichoma maiti ya Asa, bali walichoma vikolezo vyenye manukato.

Marejeo

  • +2Sa 5:7
  • +Mk 16:1; Lu 23:55, 56; Yoh 19:40

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    The Watchtower,

    12/1/2005, uku. 20

  • Fahirishi ya Machapisho

    w05 12/1 20

Tafsiri Mbalimbali

Bofya nambari ya mstari ili kuona mstari huo katika tafsiri mbalimbali za Biblia.

Jumla

2 Nya. 16:11Fa 15:25, 27
2 Nya. 16:1Yos 18:21, 25
2 Nya. 16:11Fa 15:17-19
2 Nya. 16:21Fa 7:51
2 Nya. 16:21Fa 20:1; 2Fa 12:18; 16:8
2 Nya. 16:42Fa 15:29
2 Nya. 16:4Amu 18:29
2 Nya. 16:41Fa 15:20-22
2 Nya. 16:6Yos 18:21, 25; 1Fa 15:17
2 Nya. 16:6Yos 18:21, 24; 1Nya 6:60, 64
2 Nya. 16:6Yos 18:21, 26; Amu 20:1
2 Nya. 16:71Fa 16:1; 2Nya 19:2; 20:34
2 Nya. 16:7Yer 17:5
2 Nya. 16:82Nya 14:9, 11; Zb 37:39, 40
2 Nya. 16:9Zek 4:10
2 Nya. 16:91Pe 3:12
2 Nya. 16:91Fa 15:32
2 Nya. 16:111Fa 15:23
2 Nya. 16:131Fa 15:24
2 Nya. 16:142Sa 5:7
2 Nya. 16:14Mk 16:1; Lu 23:55, 56; Yoh 19:40
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Soma katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
2 Mambo ya Nyakati 16:1-14

Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati

16 Katika mwaka wa 36 wa utawala wa Asa, Mfalme Baasha+ wa Israeli alikuja kushambulia Yuda, akaanza kujenga* Rama+ ili kumzuia mtu yeyote asitoke wala kuingia kwa* Mfalme Asa wa Yuda.+ 2 Ndipo Asa akatoa fedha na dhahabu kutoka katika hazina za nyumba ya Yehova+ na nyumba ya* mfalme na kumpelekea Mfalme Ben-hadadi wa Siria,+ aliyekuwa akiishi Damasko, akamwambia: 3 “Kuna mkataba* kati yangu na wewe na kati ya baba yangu na baba yako. Ninakutumia fedha na dhahabu. Njoo, vunja mkataba wako* na Mfalme Baasha wa Israeli, ili aondoke kwangu.”

4 Ben-hadadi akamsikiliza Mfalme Asa, akawatuma wakuu wa majeshi yake kushambulia majiji ya Israeli, wakashinda Iyoni,+ Dani,+ Abel-maimu, na maghala yote ya majiji ya Naftali.+ 5 Baasha aliposikia habari hizo, mara moja akaacha kujenga* Rama, akasimamisha kazi hiyo. 6 Kisha Mfalme Asa akawachukua watu wote wa Yuda, nao wakabeba mawe na mbao zilizokuwa zikitumiwa na Baasha kujenga Rama,+ akazitumia kujenga* Geba+ na Mispa.+

7 Wakati huo mwonaji Hanani+ akaja kwa Mfalme Asa wa Yuda na kumwambia: “Kwa sababu ulimtegemea* mfalme wa Siria nawe hukumtegemea* Yehova Mungu wako, jeshi la mfalme wa Siria limeponyoka kutoka mikononi mwako.+ 8 Je, Waethiopia na Walibya hawakuwa jeshi kubwa sana lenye magari mengi ya vita na wapanda farasi? Lakini kwa sababu ulimtegemea Yehova, aliwatia mikononi mwako.+ 9 Kwa maana macho ya Yehova yanaenda huku na huku duniani kote+ ili adhihirishe nguvu zake* kwa niaba ya wale ambao moyo wao ni kamili* kumwelekea yeye.+ Umetenda kwa upumbavu katika jambo hili; kuanzia sasa na kuendelea kutakuwa na vita dhidi yako.”+

10 Hata hivyo, Asa akamkasirikia mwonaji huyo na kumtia gerezani,* alikasirishwa sana naye kwa sababu ya jambo hilo. Wakati huohuo, Asa akaanza kuwatesa watu wengine. 11 Sasa historia ya Asa, kuanzia mwanzo mpaka mwisho, imeandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Yuda na wa Israeli.+

12 Katika mwaka wa 39 wa utawala wake, Asa alishikwa na ugonjwa miguuni, akawa mgonjwa sana; na hata alipokuwa mgonjwa, hakumwomba Yehova msaada, bali waponyaji. 13 Kisha Asa akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake;+ alikufa katika mwaka wa 41 wa utawala wake. 14 Kwa hiyo walimzika katika kaburi lake la kifahari alilokuwa amejichimbia katika Jiji la Daudi;+ walimlaza kwenye machela ya kubebea maiti iliyojazwa mafuta ya zeri na mafuta* yaliyotengenezwa kwa njia ya pekee kwa mchanganyiko wa vikolezo mbalimbali.+ Isitoshe, waliwasha moto mkubwa isivyo kawaida kwa ajili yake.*

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki