‘Kuja Chini ya Kivuli’
Kivuli kinacholetwa na jabali, wingu, jengo, mti au kitu kingine kinaweza kukinga mtu kwa njia nzuri, kama na jua kali kwa mfano. Ndiyo sababu usemi wa Biblia ‘kuja chini ya kivuli cha kitu’ kwamaanisha kuingia mahali pa ulinzi, usalama au kimbilio. Kwa mfano, Lutu aliwaambia wanaume wa Sodoma kwa habari ya malaika waliokuwa wamemtembelea hivi: “Lakini kwa wanaume hawa tu msifanye lo lote, kwa kuwa hiyo ndiyo sababu wamekuja chini ya kivuli cha dari yangu.” (Mwa. 19:8, NW) Tazama pia Isaya 32:1, 2.