Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g91 12/8 kur. 12-14
  • Je! Kuna Ubaya Hata Kama Ni Sinema Zipi Nionazo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Kuna Ubaya Hata Kama Ni Sinema Zipi Nionazo?
  • Amkeni!—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Sinema—Mielekeo ya Ki-Siku-Hizi
  • Shambulio Lililo Juu ya Macho na Masikio Yako
  • Shambulio kwa Akili na Adili Zako
  • Athari za Ujanja
  • Naweza Kuchaguaje Sinema ya Adabu?
    Amkeni!—1992
  • Utatazama Sinema Zipi?
    Amkeni!—2005
  • Miaka 100 ya Sinema
    Amkeni!—1996
  • Ninaweza Kupata Wapi Burudani Inayofaa?
    Amkeni!—2011
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1991
g91 12/8 kur. 12-14

Vijana Wanauliza. . .

Je! Kuna Ubaya Hata Kama Ni Sinema Zipi Nionazo?

‘SINEMA hazinishawishi sana,’ adai tineja mmoja aitwaye Karen, ‘kwa sababu mimi huenda sinema ili kushtuliwa na kuogopeshwa ili nitumbuizwe tu.’ Vijana wengi hutoa dai lilo hilo la kutoweza kuathiriwa na kishawishi cha sinema. Hata hivyo, kijana Georgia hakubali na hilo. Akiwa ameona sinema kadhaa zilizokadiriwa kuwa za kuonwa chini ya usimamizi wa mzazi au mlezi, alisema hivi: “Hupati kamwe kusahau mandhari hizo . . . Kadiri unavyozifikiri, ndivyo unavyojikuta ukitaka kufanya yale umeona.”a

Sinema hupendwa sana miongoni mwa vijana. Katika mwaka mmoja wa karibuni, asilimia 36 ya watu zaidi ya milioni 113 ambao walipiga mstari kwenye majumba ya sinema kotekote katika United States walikuwa katika miaka yao ya utineja. Mamilioni zaidi wanaonea sinema shangwe faraghani mwa nyumba zao kupitia kaseti za video au sinema zinazoletwa katika TV kwa nyuzi za simu. Bila shaka, sisi sote huhitaji pumziko na tafrija mara kwa mara. Tafrija ya aina hiyo yaweza kuburudisha na kuchochea akili. Kwa vijana wengi, kuona sinema ni njia moja ya kutimiza hilo na kufurahia alasiri au jioni ambayo kwa vingine ingekuwa isiyopendeza. Lakini ni sinema zipi hasa utakazotazama? Je! kuna ubaya wowote wa kuzitazama?

Sinema—Mielekeo ya Ki-Siku-Hizi

“Anasa, ngono, jeuri, pupa, ubinafsi.” Kulingana na Robert Coles mstadi katika utibabu wa ugonjwa wa akili wa watoto, hizo ndizo thamani kuu katika sinema zilizo nyingi zinazotolewa leo. Uchunguzi ulioongozwa na Dkt. Vince Hammond vilevile ulikata maneno kwamba “sinema zilizo nyingi zilizoonyeshwa katika nchi zenye viwanda zilikuwa na angalau jeuri fulani, nyingi zazo zikikadiriwa kuwa zenye jeuri au zenye wingi wa jeuri.” Wachunguzi wa Hammond walikagua sinema 1,000 kutoka nchi mbalimbali. Umalizio wao? “Kufanyizwa kwa sinema zenye jeuri ni tatizo la tufeni pote.”

Zenye kupendwa hasa miongoni mwa vijana ni sinema zenye kutisha zenye kuonyesha kupagawa na mashetani, kulalwa kinguvu, na umwagaji damu kwa njia zenye ukatili kabisa. Kama vile Dkt. Neil Senior, aliyenukuliwa katika gazeti Seventeen, anavyosema, sinema hizo “huonyesha kila jambo ambalo kila familia isingependa liwatukie.” Walakini, vijana wengi hupiga mstari ili kuziona.

Kumekuwa pia ongezeko lenye kutazamisha katika sinema za ngono ya waziwazi. Na kulingana na profesa mmoja wa chuo kikuu, “idadi kubwa ya wanaotazama video za ngono ya waziwazi katika Kanada ni vijana kati ya miaka 12 na 17 na huenda ikawa inapotosha mielekeo yao juu ya mwenendo unaohusu ngono.”

Hata hivyo, wenye biashara ya sinema hawaonekani wakijali sana. Gazeti Variety laripoti kwamba sinema zinazoonyesha jeuri na ngono ya wazi zinaongezeka, huku sinema za familia zinazofaa zikiwa hata hazifanyizwi sana. Je! yawezekana, basi, kwamba kutazama sinema zenye kuchukiza huenda kukakuathiri vibaya?

Shambulio Lililo Juu ya Macho na Masikio Yako

Sinema husababisha shambulio lenye nguvu juu ya hisia. Yesu alisema kwamba “taa ya mwili ni jicho.” (Mathayo 6:22) Na lile unaloona laweza kuwa na athari yenye kina kirefu juu yako. Kama vile ensaiklopedia moja ilivyosema, “akili huyafuata macho.” Kwa kawaida, akili yako hudhibiti kile macho yako huchagua kukazia mtazamo na kuona. Lakini unapokazia mtazamo juu ya picha zisizopatana na uhalisi wa maisha zipitazo kwenye kiwambo kikubwa cha sinema, waweza kikweli kuitia akili yako katika mikono ya udhibiti wa mfanyiza sinema ili aidhibiti apendavyo. Wengine huvutiwa sana na sinema hivi kwamba huenda wakahitaji mdukuo thabiti kwenye mbavu zao ili washtuke waache kupumbazwa na sinema.

“Sikio lisikialo” pia hushawishi kwa nguvu mawazo na matendo yako. (Mithali 20:12) Mifano yenye kuonekana ya sinema zinazotisha mtu na maneno yanayosemwa yanatiwa nguvu kwa muziki uwezao kuchochea maono ya moyoni, kutokeza hofu, msisimko, hasira, harara. Kama tokeo, sinema zaweza kupeleka muono ulio halisi sana hivi kwamba ni vigumu kwa watazamaji fulani kutenganisha yaliyo halisi kutoka kwa yaliyo masingizio.

Shambulio kwa Akili na Adili Zako

Maoni au mwelekeo wa sinema waweza kushawishi sana tendo-itikio lako kwayo. Hivyo wafanya sinema hujaribu kufanya watazamaji wajitambulishe na wenye kuigiza wanaoonyeshwa—hata wakati shujaa ni mhalifu au mtu mkatili, mwenye kutamani sana mamlaka.b Usipokuwa mwangalifu, huenda ukajikuta ukimshangilia mhalifu!

Fikiria itikio-tendo la watazamaji wamoja kwa sinema yenye kutisha ya hila iliyohusu mkichaa mwenye vidole vya wembe ambaye alikatakata watu katika mfululizo wa mandhari. Walimshangilia huyo mwuaji mwenye kumwaga damu aendelee! Wakiongozwa na kamera yenye kuvuta akili kwa hila, watazamaji walionekana kama wamepoteza thamani zao za kiadili—na huruma yote kwa ajili ya wadhulumiwa.

Jinsi ilivyo kinyume cha himizo la Biblia kutoshangilia juu ya msiba wa mwingine! (Mithali 17:5) Ni kinyume kabisa cha Kanuni ya Kidhahabu ya Yesu—‘kuwatendea wengine yale mnayotaka wao wawatendee ninyi.’ (Mathayo 7:12, Habari Njema kwa Watu Wote) Zaidi ya hiyo, je! kushangilia juu ya uuaji kwaweza kupatana na sihi za Biblia za kuwa na “huruma nyororo”? (Waefeso 4:32, NW) Je! si sawa na kujitia katika “kusanyiko la watenda mabaya”?—Zaburi 26:4, 5.

Athari za Ujanja

Hata hivyo, huenda ukaona kwamba athari ya sinema ni ya muda, ya kipindi kifupi tu. Na ni kweli, haielekei kwamba utaanza kukatakata kila mtu unayemwona kwa kuwa hiyo ilionyeshwa katika sinema fulani. Hata hivyo, gazeti moja la New Zealand laripoti kwamba kuna “ushuhuda unaoongezeka wenye kufungamanisha sinema na video zenye jeuri na mwenendo wa jeuri wa baadhi ya wale ambao huzitazama.” Kitabu Adolescence pia kilirejezea kwenye uchunguzi mwingi juu ya uhusiano kati ya ‘jeuri ya televisheni na mwenendo wa ugomvi’ na kikakiri kwamba kuna “ushuhuda unaoongezeka” unaoonyesha ufungamanisho kati ya mambo hayo mawili.

Kumekuwako pia ripoti za habari za matendo yenye kutisha na yaliyopotoka yanayofanywa kama itikio kwa mandhari za sinema. Kwa mfano, kijana mmoja alikufa kutokana na majeraha aliyopata alipojaribu kusimama kwa mikono, kichwa chini miguu juu kwenye boneti ya lori dogo lililokuwa likienda kwa kasi. Alikuwa ameona juzijuzi tendo hilo la kuonyesha ustadi likifanywa katika sinema iliyopendeza watu wengi. Kwa hiyo, si jambo lisilo la kiakili kabisa kudokeza kwamba sinema huenda ikaathiri matendo yako.

Lakini mara nyingi, sinema hutoa kishawishi chenye ujanja zaidi. Kwa mfano, je! si wengi wa marika wako hujitahidi kuzungumza, kuvalia, na kujipamba kama mifano fulani katika kiwambo? Je! huo si ushuhuda wa ushawishi wa sinema wenye nguvu? Katika upande mwingine, kutazama sinema zisizofaa kwaonekana kuwa na athari yenye kumong’onyoa thamani za kiadili za kijana. Hivyo, mchunguzi Dakt. Thomas Radecki adai kwamba kufunuliwa wazi kwa muda mrefu kwa sinema za jeuri “huongoza kwenye kugandishwa hisi kunakoongezeka kuelekea jeuri.”

Biblia husema: “BWANA [Yehova, NW] humjaribu mwenye haki; bali nafsi yake humchukia asiye haki, na mwenye kupenda udhalimu.” (Zaburi 11:5) Je! mlo wa kawaida wa sinema zenye jeuri ungeweza kuathiri mwelekeo wako juu ya jeuri? Je! ungeanza kuona jeuri kuwa yenye kutumbuiza, hata yenye kuchekesha? Na je! hata ingewezekana kwamba ungejikuta ukitaka zaidi ya wakati mwingine uliotangulia kutatua matatizo na ugomvi kupitia jeuri? Mithali 10:23 ilisema vizuri kwamba: “Uhalifu ndilo tumbuizo la mjinga.”—New American Bible.

Na vipi maadili yako ya Kikristo? Je! kufunuliwa wazi kwako kwa picha za ngono na uchi kungesukumia nyuma ya akili yako kosa na matokeo yenye kuhuzunisha ya ngono kabla ya ndoa? Je! kungemong’onyoa ‘kuchukia kwako uovu’?—Zaburi 97:10.

Mwandikaji Jane Burgess-Kohn aeleza juu ya yaliyopata msichana aitwaye Jeanie. Baada ya “kutazama sinema yenye ngono sana”akiwa pamoja na kijana aliyekutana naye ili wafahamiane kirafiki, Jeanie alikubali alikuwa “amechochewa” sana mpaka wakaanza kupapasana na kushikana-shikana sana kimapenzi. Hata hivyo, hakuweza kuachia hapo. “Nasikitika kusema,” akakiri Jeanie, “usiku huo nilikuwa rahisi kushawishwa kufanya ngono. Bado sijui lililotokea hata nikapoteza uwezo wangu wote wa kusababu. Hata sikuwa hasa nikimpenda jamaa huyo!”

Pasipo shaka, basi, sinema zina uwezo wa kushawishi moyo wako, mawazo yako, na mwenendo wako. Kwa hiyo, je! hupaswi kuwa mwenye kuchagua yale unayotazama? Makala ya wakati ujao itazungumzia hilo.

[Maelezo ya Chini]

a Katika United States, hakuna yeyote chini ya miaka 17 anayepaswa kuruhusiwa (isipokuwa akienda na mzazi au mlezi) kwa sinema yoyote iliyokadiriwa kuwa ya R, au yenye kuwekewa vizuizi fulani, na Motion Picture Association ya Amerika. Sinema za aina hiyo kwa ujumla huwa na picha za jeuri ya wazi, lugha chafu, au picha za ngono za wazi na za uchi. Lakini kwa kawaida, vizuizi hivyo havitiliwi mkazo, na vijana hukubaliwa waingie.

b Majaribio yaliyoripotiwa katika gazeti la Science News yalionyesha kwamba watazamaji huelekea kuathiriwa sana na yale wanayoyaona “pasipo kujali jinsi sinema hiyo inavyoonekana ya kuwaziwa tu” mradi ‘wanajitambulisha kwa ukaribu sana na mwigizaji wa televisheni au wa sinema.’

[Blabu katika ukurasa wa 13]

“Hupati kamwe kusahau mandhari hizo . . . Kadiri unavyozifikiri, ndivyo unavyojikuta ukitaka kufanya yale umeona”

[Blabu katika ukurasa wa 14]

Kuna “ushuhuda unaoongezeka wenye kufungamanisha sinema na video zenye jeuri na mwenendo wa jeuri na baadhi ya wale ambao huzitazama”

[Picha katika ukurasa wa 12]

Wanapopumbazwa na sinema, watazamaji mara nyingi hushangilia uuaji, wivi na ukosefu wa maadili kuhusu ngono

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki