Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g96 11/22 kur. 18-20
  • Kuondoa Mawazo Yasiyo ya Kweli Kuhusu Mashahidi wa Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuondoa Mawazo Yasiyo ya Kweli Kuhusu Mashahidi wa Yehova
  • Amkeni!—1996
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “Kwa Nini Hamjihusishi Katika Siasa?”
  • ‘Wamaanisha Ungeacha Mwana Wako Afe?’
  • Kumpa Kaisari Yaliyo ya Kaisari
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • “Vya Kaisari Mpeni Kaisari”
    Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
  • Jinsi ya Kujua Yule Tunayepaswa Kumtii
    Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
  • Je, Unapaswa Kulipa Kodi?
    Amkeni!—2003
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1996
g96 11/22 kur. 18-20

Kuondoa Mawazo Yasiyo ya Kweli Kuhusu Mashahidi wa Yehova

KATIKA kuhubiri kwao nyumba hadi nyumba, Mashahidi wa Yehova wawili walikutana na mtu aliyewaambia kwamba hapendezwi. Mashahidi hao waliondoka bila ya kusema neno, lakini walipokuwa wakitembea kando ya barabara, walimwona yule mtu akiwafuata. “Simameni, tafadhali!” mtu huyo akasema kwa sauti. “Ninataka kuomba msamaha. Sijui lolote kuhusu Mashahidi, na ninaamini kwamba wengi wetu wameelezwa mambo yasiyo ya kweli kuwahusu nyinyi.”

Kisha mtu huyo akajitambulisha kuwa Renan Dominguez, mwenyekiti wa programu ya Rotary Club of South San Francisco, California. Aliomba ikiwa Shahidi angekuja klabuni na kutoa hotuba juu ya imani na utendaji wa Mashahidi wa Yehova. Ajenda iliandaliwa. Huyo Shahidi angezungumza kwa dakika 30 kisha angejibu maswali kutoka kwa wasikilizaji. Ernest Garrett, Shahidi wa miaka mingi katika eneo la San Francisco, aliombwa atoe hotuba kwa Rotary Club katika Agosti 17, 1995, naye alishiriki yafuatayo:

“Sikujua na nilisali juu ya kile nitakachowaambia wanachama wa Rotary Club, ambao ni wafanyabiashara, na viongozi wa jumuiya, kama vile maofisa wa benki, wanasheria, na madaktari. Nilifanya utafiti kidogo na kugundua kwamba kusudi lililochapishwa la Rotary Club ni kuimarisha jumuiya. Hivyo, nilitoa habari katika ukurasa 23 wa broshua Mashahidi wa Yehova Katika Karne ya Ishirini, yenye kichwa ‘Thamani Yenye Kutumika ya Habari Njema kwa Jumuiya Yenu.’”a

“Nilieleza kwamba Mashahidi wa Yehova husaidia sana katika jambo hilo. Kila siku ya juma, Mashahidi wa Yehova wako nje wakigonga milango ya jumuiya zao. Tamaa yao ni kuwashawishi majirani wao wawe na familia imara—na familia imara hutokeza jumuiya imara. Kadiri mtu mmoja-mmoja na familia ashawishwapo na Mashahidi wa Yehova waishi kwa kupatana na kanuni za Kikristo, ndivyo uasi, ukosefu wa adili, na uhalifu upunguavyo katika jumuiya. Habari hii ilipokewa vizuri sana na washiriki hao kwa sababu ilipatana na miradi ya Rotary Club.”

“Kwa Nini Hamjihusishi Katika Siasa?”

“Mkutano ulipofikia wakati wa maswali, moja kati ya maswali ya kwanza lilikuwa: ‘Kwa nini hamjihusishi katika siasa na serikali?’ Kisha yule mwungwana aliyeuliza swali hilo akaongeza: ‘Wajua, kile Kitabu Bora husema: “Mlipeni Kaisari yaliyo ya Kaisari.’” Nilimwambia kwamba tunakubaliana kabisa na sentensi hiyo na tunaifuata kikamili. Nilieleza kwamba watu wengi ambao nimewasikia wakinukuu andiko hilo kamwe hawanukuu nusu nyingine ya mstari huo, ambao husema: ‘Na Mungu yaliyo ya Mungu.’ (Mathayo 22:21) Hivyo basi, twapaswa kufikia mkataa kwamba si yote yaliyo ya Kaisari. Kuna baadhi ya mambo ambayo ni ya Mungu. Tunakabili suala la kujua yapi ni ya Kaisari na yapi ni ya Mungu.

“Nilimwonyesha kwamba Yesu alipoulizwa swali, ‘Ni halali kumpa Kaisari kodi, ama sivyo?’ hakujibu kwa kusema ndiyo au la. Alisema: ‘Nionyesheni fedha ya kodi,’ dinari ya Waroma. Aliuliza: ‘Ni ya nani sanamu hii, na anwani hii?’ Wakamwambia, ‘Ni ya Kaisari.’ (Mathayo 22:17-20) Basi, akawaambia: ‘Basi, mlipeni Kaisari yaliyo ya Kaisari.’ (Mathayo 22:17-21) Yaani, mlipe Kaisari kodi kwa sababu sisi hupokea huduma fulani kutoka kwa Kaisari na sisi hulipa kodi ifaavyo. Nilieleza kwamba Mashahidi wa Yehova hulipa kodi zao na hawaidanganyi serikali kile kilicho haki yayo.

“Kisha nilieleza kwamba Mashahidi wa Yehova hawaamini kwamba wanadaiwa maisha yao na Kaisari. Wao huamini kwamba wapaswa kutoa ibada yao kwa Mungu, na wao humlipa hiyo kwa haki. Hivyo tuchukuapo msimamo huo, hatukusudii kudharau Kaisari kwa njia yoyote. Sisi hutii sheria zote za Kaisari, lakini kunapokuwa na mvutano kati ya pande hizo mbili, kwa heshima sisi huamua kumtii Mungu akiwa mtawala badala ya wanadamu. Kisha yule mtu aliyeuliza swali hilo alisema mbele ya kikundi chote: ‘Siwezi kubisha hilo!’

“Pia tuliweza kujibu maswali mengi kuhusu kazi yetu ya kuhubiri. Baada ya mkutano wengi wa washiriki walikuja na kutusalimu kwa mkono wakisema kwamba walikubaliana kabisa nasi kwamba familia ndio msingi wa jumuiya imara. Kisha tulimpa kila mshiriki broshua Mashahidi wa Yehova Katika Karne ya Ishirini.

“Baada ya mkutano huu mwenyekiti wa programu, Bwa. Dominguez, alinipigia simu na kuniomba niende ofisini mwake, kwani alikuwa na maswali zaidi ya kuuliza kuhusu itikadi zetu. Tulikuwa na mazungumzo mazuri juu ya maandiko kadhaa. Hasa alitaka mimweleze msimamo wetu kuhusu damu. Alisema kwamba hawezi kutiwa damu mishipani, na alivutiwa sana na habari niliyompa kutoka broshua Damu Yaweza Kuokoaje Uhai Wako? hivi kwamba alinialika kurudi tena na kuwahutubia wanachama wa klabu kuhusu msimamo wetu juu ya damu. Nilimwalika Shahidi mwingine, Don Dahl, kuungana nami katika programu hii. Yeye huenda hospitali kuzungumzia suala hilo na madaktari Mashahidi walazimikapo kufanyiwa upasuaji. Pamoja, tulieleza kwa ndani namna tufanyavyo kazi na madaktari na wasimamizi wa hospitali kubainisha msimamo wetu wa Kimaandiko na kuandaa vibadala vinavyofaa badala ya utiwaji wa damu mishipani.”—Mambo ya Walawi 17:10-12; Matendo 15:19-21, 28, 29.

‘Wamaanisha Ungeacha Mwana Wako Afe?’

“Baada ya huo mkutano mtu fulani alikuja na kuniuliza kibinafsi: ‘Wamaanisha ungeacha mwana wako afe ikiwa angepatwa na aksidenti na kuletwa katika chumba cha dharura akitokwa damu nyingi sana?’ Nilimhakikishia kwamba nashiriki hangaiko lake, kwani nilikuwa na mwana na alikufa katika ule mlipuko wa ndege juu ya Lockerbie, Scotland, katika 1988. Katika kujibu swali lake, kwanza nilimweleza kwamba nisingetaka mwana wangu afe.

“Sisi si wapinga-daktari, wapinga-tiba, au wapinga-hospitali. Hatuponyi kwa imani. Tunahitaji huduma za wataalamu wa tiba. Tumeweka tumaini letu katika Mungu na tuna uhakika kwamba miongozo yake katika suala hili la damu ni kwa faida yetu ya kudumu. Mungu anaelezwa katika Biblia kuwa ‘akufundishaye ili upate faida, akuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata.’ (Isaya 48:17) Pia yeye amempa Mwana wake uwezo wa kufufua wafu. Yesu alisema: ‘Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi, naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je! unayasadiki hayo?’—Yohana 11:25, 26.

“Yale tu sisi huomba madaktari kuelewa ni kwamba msimamo wetu ni suala la dhamiri na hatuwezi kulijadili. Hatuwezi kujadili suala hili kama vile hatuwezi kujadili amri ya Mungu kuhusu uzinzi. Hatuwezi kujadiliana na Mungu na kusema, ‘Mungu, je, kuna hali zozote ambazo zinaweza kuniruhusu kufanya uzinzi?’ Kisha nikamwambia mtu huyu: ‘Uliuliza ikiwa ningeacha mwana wangu afe kwa kukataa kutiwa damu mishipani. Kwa heshima zote ningependa kukuuliza ikiwa ungeacha mwana wako afe katika utumishi wa kijeshi wa taifa lolote?’ Alijibu mara moja na kwa mkazo, ‘Ndiyo! Kwa sababu huu ni wajibu wake!’ Nikasema: ‘Ungeacha mwana wako afe kwa ajili ya yale unayoamini. Niruhusu mimi niwe na pendeleo hilohilo na mwana wangu.’

“Maendeleo yenye kupendeza yaliyofuata baadaye ni kwamba mwenyekiti wa programu Bwa. Dominguez, alitukaribisha mke wangu na mimi kwa mlo mkuu pamoja naye na mke wake. Alifikiri kwamba mke wake alikuwa amearifiwa vibaya na kupewa mawazo yasiyo ya kweli kuhusu Mashahidi wa Yehova. Na ilikuwa kweli. Alikuwa amearifiwa vibaya. Tulikuwa na jioni yenye furaha, na mke wake aliuliza maswali mengi kutuhusu na kazi yetu, naye alituruhusu tuyajibu kirefu. Siku iliyofuata alipiga simu na kusema kwamba mke wake alifurahia sana kukutana na mke wangu nami na alifikiri kwamba sisi ni watu wazuri sana.

“Nimeendelea kufanya ziara za kawaida kwa Bwa. Dominguez, naye aonyesha shauku sana katika Biblia. Aliniambia: ‘Nisingesita kukutia moyo kuwasiliana na wenyekiti wa programu za Rotary Club katika eneo la Greater San Francisco Bay na kujitolea kutoa hotuba katika klabu zao inayofanana na ile uliyotoa katika klabu yetu. Waweza kutumia jina langu kama rejezo, na nikiulizwa, nitafurahi kutoa pendekezo la juu zaidi ili ualikwe ukiwa msemaji mgeni.’

“Klabu za Rotary ni za kimataifa. Je, inawezekana kwa klabu nyinginezo katika Marekani na duniani pote kukaribisha hotuba za Mashahidi wa Yehova?”

[Maelezo ya Chini]

a Iliyochapishwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc., katika 1989.

[Picha katika ukurasa wa 18]

Bwana Renan Dominguez, kushoto, na Ndugu Ernest Garrett

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki