Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 2/1 kur. 65-66
  • ‘Nia ya Kuamini’ Ni Hekima—Wakati Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Nia ya Kuamini’ Ni Hekima—Wakati Gani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Habari Zinazolingana
  • Uumbaji au Mageuzi?—Sehemu ya 1: Kwa Nini Nimwamini Mungu?
    Vijana Huuliza
  • Kutokuamini kwa Kisasa—Je! Jitihada ya Kutafuta Yapasa Kuendelea?
    Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu
  • Utamwambia Nini Mtu Asiyeamini Mungu?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Msingi wa Kumwamini Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 2/1 kur. 65-66

‘Nia ya Kuamini’ Ni Hekima​—Wakati Gani?

IMEDAIWA, “Sifa iliyo ya maana zaidi kupita zote na isiyotajwa sana katika ulimwengu ni nia ya kuamini. Inachukua nafasi yake kila mara tunapotumbukiza barua katika sanduku la posta au kupanda ndege au kufanya mambo mengi ya kawaida yanayotiwa ndani ya maisha yetu ya kisasa. Tangu fedha tunayoweka katika banki mpaka fedha tunayokopa . . . tunaishi katika ulimwengu uliojengwa juu ya imani,” juu ya nia ya kuamini.​—The Will to Believe, cha mtaalamu na mwandishi ajulikanaye sana Marcus Bach.

Hii inaweza kuwa hivyo kwa kadiri kubwa katika ulimwengu uonekanao, lakini ni kweli namna gani inapokuja kwa mambo ya kiroho? Wasioamini habari za Mungu na kuwako kwake wao zaidi hawaonyeshi nia ya kuamini. Kama mchunguzi wa filosofia William James alivyoonyesha wakati fulani, wapinzani hao wanaamini kwamba ni jambo la maana zaidi kukataa kosa kuliko kuikubali kweli. Kwa matokeo gani? Hawataki kuchukua nafasi ya kujifunza kweli zinazohakikisha kwamba kuna Mungu na kwa sababu hiyo wapate baraka zote zinazoletwa na ujuzi huo.

Mwendo usio wa hekima wa wapinzani hawa ni sawasawa na nia ya wengi katika karne ya kumi na saba kwa uvumbuzi wa Harvey wa kwamba damu inazunguka katika mwili wa kibinadamu. Harvey hakuwa na maelezo juu ya namna damu ilipita kutoka kwa mishipa mikubwa (arteries) mpaka kwa vena (vile vile mishipa ya damu), kwa sababu darubini ya kutazama vitu vidogo sana visivyoonekana kwa macho matupu wakati huo haikuwa imevumbuliwa; hivyo hakuweza kuona kapilari (mishipa midogo ya damu). Kutoonekana huku kwa kapilari kulileta mojawapo la makinzano yaliyotokezwa kwa fundisho lake. Kwa hiyo uvumbuzi wake “haukuwapata wafuasi kutoka kwa wo wote wa wataalamu wa mambo yanayokamatana na elimu ya mwili wa Ulaya.” Pahali pake, “watu mashuhuri waliandika makinzano makali,” tunaambiwa katika kitabu The Human Body.

Karne tatu nyuma ya hapo wataalamu wa udaktari wa Uingereza waliteta mno; wakati huu kwa sababu ya uvumbuzi wa Alexander Fleming wa penicillin (dawa ya kuzuia viini vya maradhi kutoongezeka). Lakini wachunguzi wawili walikuwa na nia ya kuchunguza kwa mioyo mizuri uwezekano wa dawa hiyo na walifanikiwa kukamilisha penicillin isiharibiwe na vitu vibaya. Kama matokeo wachunguzi hao watatu walipata zawadi kubwa kwa kazi yao juu ya ambacho kimeitwa “kitu kimoja cha kuokoa uhai kilicho kikubwa zaidi cha dawa ya kisasa.”

Mtu aliye na moyo safi, aliye na nia ya kuchunguza kwa habari ya Mungu, hatakosa kuamini habari zake na kuwako kwake. Hivyo Santiago Ramón y Cajal, mmoja wa waandishi wakubwa wa jicho, wakati fulani alidai kwamba hekima aliyoiona hapa ikionyeshwa, zaidi katika vioo vya macho, “kwa mara ya kwanza ilipunguza imani yangu katika kubahatisha kwa Darwin kwa sehemu ya asili.” Hii ilikuwa kwa sababu hakutaka kuziba ufahamu wake asione uhakika. Aliamini uhakika wa kwamba ni lazima iwe kuna nguvu fulani kuu.

Vile vile, Robert Millikan, aliyedhaniwa kuwa mkuu wa wanasayansi wa Amerika katika siku zake, wakati fulani alisema: “Kuna Uungu unaotengeneza makusudi yetu . . . ama sivyo tusingejua daraka letu wenyewe. FILOSOFIA YA MAMBO YA KIMWILI PEKE YAKE KWANGU NI UPUMBAVU MWINGI. Watu wenye hekima katika vizazi vyote kila mara wameona mambo ya kutosha kuwafanya kuwa wanyenyekevu.” Ndiyo, kama mtume Paulo alivyosema karne kumi na tisa mbeleni: “Mambo yake [Mungu] yasiyoonekana tangu kuumbwa ulimwengu yanaonekana, na kufahamika kwa kazi zake; . . . hata wasiwe na udhuru” kwa kukataa kuamini kuwako kwa Mungu.​—Rum. 1:20.

Nia ya kuamini katika nguvu kuu isiyoonekana huenda ikasemwa kuwa tabia ya msingi ya kibinadamu. Hivyo The World Book Encyclopedia kinasema kwamba “hakujawahi kuwa na taifa lisilokuwa na namna fulani ya dini.” Na kama Mtaalamu Nigg alivyoona, “Kumpenda Mungu kuliko katika mwanadamu hakuwezi kuondoleka, iwe yuko wapi na awe ni wa kizazi kipi.” Hii ni wazi zaidi wakati watu wanapoelekea hatari au kifo, sababu ambayo imefanya isemekane, “Hakuna wasioamini kuwako kwa Mungu katika matundu ya mbweha,” yaani, katika uwanja wa vita.

Kwa sababu nia ya kuamini ni tabia ya msingi na lazima, Urusi ya Kikomunisti yenye nguvu imelazimishwa kupatana na dini zinazojulikana zinazozoewa katika Kristendomu (jambo la aibu). Vijana wa Urusi wanaona filosofia ya mambo ya kimwili ya maisha kuwa si ya kuridhisha. Wanaowaza sana kati yao wanalilia uhafifu wa maisha zao na kulilia jambo wanaloweza kuamini. Vijana wa Amerika wanaonyesha lazima ile ile ya kuamini.

Nia ya kuamini kitu ni hekima, lakini, wakati tu inapokuwa juu ya msingi wa uhakika na busara, kama ilivyoonwa katika mtajo uliotangulia wa mwanasayansi Millikan. Imani katika kuwako kwa utu wa Mamlaka ya Juu Zaidi haitoshi. Ili nia ya kuamini iwe hekima ni lazima mtu aendelee na kuwa na nia ya kuchunguza kitu kinachodai kujibu maulizo kama: Aliye Mkuu Zaidi anataka nini kutoka kwetu? Tulitoka wapi? Hali yetu ni nini? Sababu gani tunapata taabu na kufa?

Kwa habari hii Biblia ina mengi ya kupendekeza tuichunguze kuliko kitabu kingine cho chote. Ni ya kale kupita vyote na inatafsiriwa zaidi sana​—yote au katika sehemu katika lugha 1,471​—jambo ambalo ndilo tungetazamia kwa ufunuo wa kimungu.

Zaidi, imetia moyoni uaminifu usiotiwa na kitabu kingine cho chote wakati wo wote. Watu wamejitoa ili kuitafsiri. Imeleta tumaini na furaha kwa wenye huzuni na maombolezo na imewasaidia wengi wasioweza kutajwa kuishi maisha bora.

Rais wa Amerika wa zaidi ya karne moja iliyopita anatajwa kama akimwambia rafiki mpinzani: “Soma Kitabu hiki [Biblia] kwa sababu ya unachoweza kukubali kwa busara na yaliyosalia yachukue kwa imani, na utaishi na kufa ukiwa mtu bora.” Kukusaidia wewe upate ufahamu bora na faida zaidi kutoka kwa Kitabu hicho ndilo kusudi la vitabu wanavyogawiwa watu na mashahidi wa Kikristo wa Yehova. Kwa kusoma gazeti ili hili unaonyesha nia yako ya kuamini​—⁠kwa ajili ya sababu za kutosha na uhakika.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki