Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 2/1 kur. 66-68
  • Ufanisi Chini ya Ufalme wa Mungu Katika Kizazi Chetu Wenyewe

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ufanisi Chini ya Ufalme wa Mungu Katika Kizazi Chetu Wenyewe
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Habari Zinazolingana
  • Karibuni Kusudi la Mungu Kutimizwa
    Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?
  • Matukio Hayo Yote Yanamaanisha Nini?
    Endeleeni Kukesha!
  • Ulimwengu Mpya—U Karibu Sana!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Habari Njema Wanazotaka Wewe Usikie
    Mashahidi wa Yehova Katika Karne ya 20
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 2/1 kur. 66-68

Ufanisi Chini ya Ufalme wa Mungu Katika Kizazi Chetu Wenyewe

HALI ya ulimwengu leo ni yenye hatari sana hivyo kwamba watu wengi wenye ujuzi wanatia shaka kama maisha yataendelea. Ilisema hivi ripoti ya pekee kwa Post la Washington: “Wakuu wameona hatari inayokaribia isiyolingana na nyingine yo yote waliyoiona wanadamu. Wataalamu wa siku zijazo wanaiita hatari kubwa kupita zote, upeo wa makosa yasiyomalizika.”

Hakuna wakati mwanadamu ameelekea kuiharibu dunia kama huu, kuichafua hewa tunayopumua, maji tunywayo na chakula tulacho. Hakuna wakati mwingine serikali zilipopatwa na magumu makubwa sana ya kitaifa na mataifa yote zisiyoweza kuazimia kama sasa. Na hakuna wakati mwingine wale wanaoipinga enzi yote ya Mungu walipojionyesha waziwazi kama sasa. Mamilioni yanakanusha kwamba Mungu haishi. Hata kati ya wale wanaokubali kuwako kwake kunao wengi wanaodai kwamba hapendezwi na wanadamu. Kwa hiyo kuna takwa kubwa kwa Yehova Mungu kuonyesha kwamba yeye ni Mfalme juu ya dunia yote.

Habari za kuchangamsha ni kwamba yeye atafanya hivyo katika kizazi chetu. Ufalme wake kupitia kwa Kristo karibuni utazivunja-vunja serikali zote vipande vipande zinazoupinga nao wenyewe utasimamia mambo ya mwanadamu pasipo mpinzani. (Dan. 2:44) Ufanisi wa kweli utaanza, na umaskini, taabu na uonezi vitakwisha. Kwa sababu gani tuna uhakika mwingi juu ya hili?

Kwanza, orodha ya tarehe ya Biblia inaonyesha kwamba tangu vuli ya mwaka wa 1914 C.E. tumekuwa tukiishi katika “siku za mwisho” za hii taratibu ya mambo. Yesu Kristo alionyesha kwamba hizi “siku za mwisho” hazingeendelea zipite muda wa kizazi kinachoona mwanzo wake. (Mt. 24:34) Kwa hiyo, walau watu fulani walioyashuhudia maogofyo ya Vita ya Kwanza ya Ulimwengu watauona mwisho wa serikali yenye kuongozwa na wanadamu wasiokamilika na kuletwa kwa ufanisi chini ya ufalme wa Mungu.

Kwa kuonyesha orodha ya tarehe ya Biblia ni ya kweli, twaziona hali zile zile zilizotangulia kusemwa katika Maandiko Matakatifu kama zikionyesha “siku za mwisho.” Angalia, kwa mfano, ambayo 2 Timotheo 3:1-5 anayotuambia: “Ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu; wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake.” Je! hujaziona hali izi hizi? Si kweli kwamba zinaonekana kati ya wale wanaojidai kumtumikia Mungu, yaani, washiriki wa makanisa ya Kristendomu?

Uhakika wa kwamba “siku za mwisho” zitakomea katika uharibifu wa kila mtu na kila kitu kiupingao ufalme wa Mungu unatoa sababu ya kufikiri kwa uzito. Imempasa mtu ajiulize mwenyewe, Je! mimi ni katika hali njema kuweza kulindwa kama mmojawapo wa wafuasi waaminifu wa ufalme wa Mungu?

Kwa mfano, je! wewe umezijua kanuni za Mungu za adili, zinazoonyeshwa katika Biblia, na je! unaishi kupatana nazo? (1 Kor. 6:9-11) Vile vile, je! unazitumia nafasi zako kwa njia bora uwezavyo? Je! unafanya yote uwezayo uitunze nyumba yako kuwa safi na malidadi? Je! wewe u mfanya kazi mwenye bidii, ukijaribu sana kufanya yote uwezayo? Je! wewe unazitumia nguvu zako na akili kwa hekima, bila ya kupoteza mali zako na nguvu kwa mazoea machafu?

Hata ikiwa wewe si mmojawapo wa maskini, je! maisha yako ni kupatana na mapenzi ya Mungu? Je! wewe u mwenye huruma, mkarimu na mwenye upendo? Je! moyo wako unakuchochea ufanye tendo uwezalo kuwasaidia wale wenye shida iliyowapata kwa kutokupenda kwao? Je! unahuzunishwa na maonezi mabaya sana wanayoyavumilia mamilioni?

Mambo haya ni ya maana, kwa maana Yehova Mungu hawataki watu wachafu katika mazoea, mwenendo, utu na nyumbani wawe raia zake. Wakristo wanakumbushwa: “Kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote; kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.” (1 Pet. 1:15, 16) Zaidi ya hayo, Yehova Mungu haukubali uvivu. Kanuni iliyoongozwa na roho ya Mungu ni: “Ikiwa mtu hataki kufanya kazi, basi, asile chakula.” (2 The. 3:10) Kwa upande mwingine, wale wasiozijali shida za walioonewa na wenye huzuni wanasemwa kuwa waovu. Inasema Mithali 14:21: “Amdharauye mwenzake afanya dhambi; bali amhurumiaye maskini ana heri.”

Ni jambo la haraka kwamba watu mmoja mmoja waonyeshe kweli kwamba wao ni wapenda haki na wachukia mabaya. Imempasa mtu ashukuru kwamba Mungu amekuwa mvumilivu kwa wanadamu, akiwapa watu wote nafasi ya kuonyesha kama wanataka kuishi kupatana na njia zake ama sivyo.

Ikiwa wewe u mmojawapo wa wale wanaopenda kweli na haki na unataka sana kuyafanya mapenzi ya Mungu, tunakusihi ulikubali karibisho la mashahidi wa Yehova wa Kikristo la kujifunza Biblia pamoja nao. Kwa njia hiyo, hata wewe waweza kulishiriki tumaini lenye kufariji kwamba ufalme wa Mungu karibuni utaitosheleza tamaa ya kila mtu mwenye moyo mnyofu. Ufanisi chini ya ufalme wa Mungu utashuhudiwa katika kizazi chetu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki