Ulimwengu Mpya—U Karibu Sana!
ULIMWENGU huu umo katika maumivu ya kifo! Je! inaweza kuwa hivyo kweli kweli? Basi, fikiria hali za ulimwengu kwa uangalifu.
Kuna silaha za nyukilia zinazotosha kurudia-rudia kuwaharibu mara kadhaa wakaaji wote wa dunia. Vita ya wenyewe kwa wenyewe inawaka moto katika nchi nyingi, kama vile Angola na Musumbiji. Kuna mapambano kati ya watu wa rangi mbalimbali katika Afrika Kusini, Sri Lanka, na nchi nyinginezo. Uvamizi-haramu na njaa kubwa pia ni mambo yanayomaliza uhai wa wanadamu wengi mno.
Namna gani kipuku cha UKIMWI? Sunday Times ya Afrika Kusini ya Oktoba 25, 1987, ilikiita “kifo cheusi kipya” na kusema: “Sasa matokeo mabaya sana ya Ukimwi wa Kiafrika ulio wa kuogofya yanafunuliwa: Inaelekea kwamba katika nchi fulani-fulani watu sita kati ya kila kumi watakufa ifikapo 1994.”
Kuna hofu nyingi kwa sababu ya hali hizo. Kama vile Harold C. Urey mshindi wa zawadi ya Nobeli alivyosema miaka kadhaa iliyopita: “Sisi tutakula hofu, tutalala katika hofu, tuishi katika hofu na kufa katika hofu.” Kwa njia yenye umaana mkubwa, Yesu Kristo, mnabii mkubwa zaidi aliyepata kuwapo duniani, alitabiri kwamba katika siku za mwisho za ulimwengu huu, wanadamu wangekuwa ‘wenye kuzirai kwa sababu ya woga na taraja la vitu vinavyokuja juu ya dunia inayokaliwa.’—Luka 21:26, NW.
Lakini wengi hawana hofu. Badala ya hivyo, wao wanashangilia. Kwa nini? Kwa sababu wanajua kwamba mfumo huu wa ulimwengu (si Dunia sayari) u karibu na mwisho wao, lakini ulimwengu mpya u karibu sana. Wanaweza kuwa na uhakika hivyo jinsi gani? Kwa sababu ya utimizo wa manabii mengi sana ya Biblia.
Mathalani, Yesu Kristo alipoulizwa ni nini ingekuwa ishara ya kuwapo kwake na ya mwisho wa ulimwengu, yeye alisema: “Taifa litainuka dhidi ya taifa na ufalme dhidi ya ufalme.” Katika 1914, Vita ya Ulimwengu ya 1 ilifoka. Ilisababisha upotezo ulio mkubwa zaidi wa uhai ambao umepata kutokana na vita kufikia wakati huo. Hasara ya wapiganaji ilikuwa nini? Wapatao 9,000,000 walikufa, zaidi ya mamilioni ya raia wa kawaida! Lakini Vita ya Ulimwengu ya 2 ilikuwa yenye teketezo kubwa zaidi, ikichukua uhai wa watu wapatao 55,000,000! Yesu alionyesha wazi kwamba yote hayo yangeambatana na upungufu wa vyakula, matetemeko ya dunia, magonjwa ya kipuku, na kutotii sheria.—Mathayo 24:7-13; Luka 21:10, 11, NW.
Mtume Mkristo Paulo alitabiri pia kwa usahihi juu ya hali zilizopo za ulimwengu. Yeye aliandika hivi: “Siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu; wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao.” (2 Timotheo 3:1-5) Paulo angeweza kutabiri hali za siku iliyopo kwa usahihi hivyo kwa sababu Mungu ndiye aliyemvuvia kuandika maneno hayo.
Kwa habari ya maneno yake mwenyewe kuhusu wakati wa mwisho, Yesu alisema: “Mwonapo mambo hayo yanaanza kutokea, tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu u karibu.” (Luka 21:31) Mamilioni wanatumia sala ya kiolezo ya Yesu na kuomba Ufalme wa Mungu uje. (Mathayo 6:9, 10) Lakini wanapoulizwa, “Ni nini hasa ambacho Ufalme huu utafanya?” wao hawana jibu. Kwa utofautiano, mamilioni wanaojifunza Biblia kwa bidii-endelevu wamejifunza kwamba Ufalme huo utaleta mwisho kwa ulimwengu huu wa zamani na kusimamisha imara ulimwengu mpya ambao utaletea aina ya binadamu baraka zisizohesabika. Lakini jinsi gani? Wakati gani?