Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w77 2/15 kur. 75-76
  • Wakristo wa Kweli Hawawezi Kuwa Waoga

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wakristo wa Kweli Hawawezi Kuwa Waoga
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Habari Zinazolingana
  • Kuvumilia Matendo Mabaya Kwaleta Utukufu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Iweni Wanafunzi wa Kweli wa Kristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • 2 Timotheo 1:7—“Mungu Hakutupa Roho ya Woga”
    Mistari ya Biblia Yafafanuliwa
  • ‘Iweni Hodari na Wenye Moyo wa Ushujaa!’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
w77 2/15 kur. 75-76

Wakristo wa Kweli Hawawezi Kuwa Waoga

INAMPASA mtu awe hodari ili awe Mkristo wa kweli, kwa sababu ni lazima mtu akubali kupatwa na hatari, magumu, upinzani, ndiyo, na hata mauti yenyewe. Wanafunzi wa kweli wa Yesu Kristo hawawezi kutazamia kutendewa vizuri zaidi asivyotendewa Bwana wao. Kama Yesu mwenyewe alivyosema: “Mutumwa si mukubwa kuliko bwana yake. Kama wakinitesa mimi, watawatesa ninyi vilevile.”​—Yoane 15:20, ZSB.

Ijapokuwa Yesu aliteswa, hakukuwa na sababu yenye haki kufanya hivyo. Yeye alihurumia watu wengine. Alikuwa mwenye huruma, fadhili na upendo. (Mt. 8:2, 3; 11:28-30; Marko 8:2) Alifanya kazi bila kuchoka, mara nyingi akijinyima chakula na pumziko alilohitaji, ili awaondolee wanadamu wasiokamilika maumivu yao na kuwapa faraja ya kiroho na kitiamoyo. (Mt. 14:13, 14; Marko 6:31-34) Ijapokuwa alitukanwa, yeye hakutukana mtu ye yote. Mwenendo wake wa maisha ulikuwa bila lawama, usiokuwa na dhambi.​—1 Pet. 2:22, 23.

Hata hivyo Yesu Kristo alikuwa chombo cha kuchukiwa vibaya sana. Alishtakiwa vibaya ulevi na ulafi, kuvunja sheria ya Mungu na hata kuwa mwenda wazimu. (Luka 7:34; Yohana 5:18; 8:48) Alitendewa kwa aibu sana, akatemewa mate, akapigwa makofi, ngumi, viboko na mwisho akapigiliwa kwenye mti wa mateso afe kwa aibu mbele ya watu wote kama mtu anayemkufuru Mungu.​—Mt. 26:65-67; Yohana 18:22; 19:1, 17, 18.

Ilikuwa lazima Yesu awe hodari sana ili avumilie haya yote. Angaliweza kuepuka asichukiwe kwa kuishi maisha mema kama seremala katika Nazareti. Lakini aliitangaza kweli bila kuogopa, akafunua uongo wa kidini na makosa ya kuishi maisha kwa ajili ya faida ya pekee tu. Jambo hilo lilimletea chuki ya ulimwengu, kwa sababu wale waliopendelea kuishi maisha yaliyokuwa kinyume cha mapenzi ya Mungu hawakutaka kuonyeshwa kwamba walikuwa waovu. Waliudhika kufunuliwa kwamba hawakuwa “wenye haki” kama vile wengi wao walivyojidai kuwa.​—Yohana 3:19, 20.

Wanafunzi wa Yesu wanatakiwa wafanye yale ambayo yeye alifanya. Si kuishi maisha yanayopatana na mapenzi ya Mungu tu, bali wasaidie na wengine wafanye hivyo. (Mt. 28:19, 20) Kwa kweli, kazi hii inawafanya wapingane na wale wanaopendelea njia mbaya. Hawa wanatenda kijeuri, wakitaka kazi hii izuiwe. Wakipingwa kijeuri, waoga ndio wangeacha, lakini Wakristo wa kweli hawawezi kuacha.

Roho au nia yenye kutokeza sana ya Wakristo wa kweli si ile ya woga. Huenda wakawa wenye haya, wenye kuogopa kuumizwa au wenye kutaka kutiwa moyo ili waonyeshe zaidi hali ya kutoogopa. Lakini hawaruhusu woga wo wote wala haya uwazuie kufanya mapenzi ya kimungu, kama vile waoga wangeweza kufanya. Mtume wa Kikristo Paulo alimkumbusha mfanya kazi mwenzake mwaminifu Timotheo hivi: “Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.”​—2 Tim. 1:7.

Paulo alifahamu sana sana kwamba Mungu alikuwa amempa roho ya nguvu. Katika barua yake kwa Wakristo katika Filipi, alisema hivi: “Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.” Paulo alikuwa amepewa nguvu ya kupambana na adui na hatari za namna zote hata hakurudi nyuma kwa woga. Alipewa nguvu ya kuvumilia majaribu makali na mateso.​—Flp. 4:11; 2 Kor. 11:23-27; 12:9, 10.

Pamoja na ‘roho ya nguvu’ ya kupewa na Mungu, ‘roho ya upendo’ ilimhimiza aendelee katika utumishi wa uaminifu. Yeye alikuwa na upendo mwingi sana kwa Yehova Mungu na kwa Yesu Kristo. Akithamini sana yale waliyokuwa wamemfanyia, yeye aliandika hivi: “Maana mimi ni mdogo katika mitume, nisiyestahili kuitwa mtume, kwa sababu naliliudhi Kanisa la Mungu,. Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo; na neema yake iliyo kwangu ilikuwa si bure, bali nalizidi sana kufanya kazi kupita wao wote; wala si mimi, bali ni neema ya Mungu pamoja nami.” (1 Kor. 15:9, 10) Tena, Paulo aliwapenda sana wanadamu wenzake, kutia na wananchi wenzake ambao ndio waliomtesa sana. Aliweza kusema akiwa na dhamiri safi hivi: “Nina huzuni nyingi na maumivu yasiyokoma moyoni mwangu. Kwa maana ningeweza kuomba mimi mwenyewe niharimishwe na kutengwa na Kristo kwa ajili ya ndugu zangu, jamaa zangu kwa jinsi ya mwili.”​—Rum. 9:2, 3.

Pamoja na hayo, roho ya akili timamu ilimsaidia Paulo audumishe uaminifu. Aliweka maoni yaliyosawazika, akitambua kwamba jambo lililokuwa la maana sana lilikuwa uhusiano wake na Yehova Mungu kama mwanafunzi aliyejitoa kweli kweli wa Yesu Kristo. (Flp. 3:8-11) Hili lilimsaidia asishindwe na mikazo afanye mambo yake yawe rahisi.

Paulo aliweza kuendelea kuwa mwanafunzi wa Yesu Kristo aliyekubalika kwa sababu alidumisha roho ya “nguvu na upendo na ya moyo wa kiasi” ambayo alipewa na Mungu. Yeye alikuwa na hakika ya zawadi yake, basi, alipokuwa akitazamia kufa, alimwandikia Timotheo hivi: “Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda; baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.”​—2 Tim. 4:7, 8.

Lakini, waoga, hawana msingi wa kuwa na uhakika kama huo. Kwa kweli, Neno la Mungu laonyesha wazi kwamba wao hawana zawadi. Wao wamo kati ya wale watakaopatwa na “mauti ya pili,” kifo kisicho na tumaini la ufufuo.​—Ufu. 21:8.

Ni haki hii iwe hivyo, kwani mwoga hana ushikamano na Mungu. Wakati anapoona wengine wakitaabikia haki, yeye anaogopa na kuacha kumtumikia Mungu ili asiumizwe na watu. Anapopata jaribu la ukamilifu wa moyo wake, yeye anajiweka upande wa Shetani Ibilisi kwa kuonyesha kwamba shtaka la adui huyo ni la kweli: “Ngozi kwa ngozi, naam, yote aliyo nayo mtu atayatoa kwa ajili ya uhai wake.”​—Ayu. 2:4.

Mwoga anaonyesha kutokuwa na imani kabisa na uwezo wa Mungu wa kulipia hasara yo yote ambayo Shetani na watumishi wake wangeweza kuleta. Akishindwa kwa sababu ya kuogopeshwa na kifo, anaonyesha haiamini ahadi ya Mungu ya ufufuo. (Mt. 10:28; Ebr. 11:35) Ikiwa mikazo ya uchumi yamfanya avunje sheria ya kimungu, yeye anafunua kwamba hana imani na uhakikisho wa Mungu wa kuruzuku watumishi wake wote.​—Ebr. 13:5, 6.

Ikiwa wewe watamani kuwa kati ya wale wasioshindwa na woga wa namna hiyo chini ya mikazo, chukua hatua utie nguvu imani yako. Jifunze Neno la Mungu, umsihi akupe uongozi, ushiriki pamoja na Wakristo wasioogopa na kuwa mtendaji katika kusaidia wengine wawe wanafunzi wa Yesu. Kama Paulo, ndivyo unavyoweza kutazamia zawadi ile itakayotolewa, si kwa waoga, bali kwa Wakristo wasioogopa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki