Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w78 8/15 kur. 14-17
  • Bora ya Jamaa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Bora ya Jamaa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • NYUMBA YENYE UTARATIBU
  • BIBLIA INASAIDIA HALI YA JAMAA
  • UNYENYEKEVU NA NYUMBA
  • Familia—Binadamu Wanaihitaji!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Kutumia Neno la Mungu Katika Jamaa Zetu Wenyewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Maisha ya Jamaa Yanayofaa—Si Jambo la Zamani Tu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Jifunzeni Neno la Mungu kwa Ukawaida Mkiwa Familia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
w78 8/15 kur. 14-17

Kuendeleza Hali

Bora ya Jamaa

SISI sote katika jamaa​—⁠baba, mama na watoto​—⁠tunapendezwa na kuona hali njema katika jamaa. Haipaswi kuonwa kwamba baba peke yake ndiye mwenye daraka hilo. Jamaa yote inapendezwa na mambo kama chakula, mavazi, mahali pa kukaa, afya na ukuzi. Sisi sote tunashiriki katika baraka na taabu ya jamaa. Na zaidi ya yote, jamaa yote inahitaji kuendeleza uhusiano (ushirikiano) mzuri na Yehova Mungu. Ijapokuwa baba ndiye anayeongoza, wale wengine wanapaswa kushiriki na kuunga mkono mambo haya yote. Ni kweli kwamba, baba ndiye anayetafuta riziki, lakini huenda wengine washiriki mzigo huu nyakati nyingine.

Katika siku hizi ambazo bei ya vitu inapanda sana, na fedha zinapunguza thamani (bei), ni jambo linalofaa jamaa kupanga juu ya matumizi ya fedha. Washiriki wa jamaa wanahitaji kukuza maoni yanayofaa. Watoto hawapaswi kuwa wakiuliza-uliza wanunuliwe vitu na kusisitiza wafuate wanavyotaka. Wote wanapaswa kushirikiana kwa kusaidiana katika njia yenye upendo. Wakiwa na roho hii inayofaa washiriki wote wa jamaa watakuwa waangalifu watumie vitu kulingana na mapato ya jamaa. Wote na watosheke kuwa na riziki. (1 Tim. 6:8) Epuka kuingia katika deni isiyo ya lazima. Biblia inasema hivi: “Msiwiwe na mtu cho chote.” (Rum. 13:8) Ninyi watoto, mnapoketi mezani, je! mnamaliza chakula chote mnachowekewa katika sahani bila kuacha kitupwe? Ndiyo, tunapaswa kuepuka matumizi mabaya. Na tuwe waangalifu tutumie fedha zetu kwa mahitaji ya lazima kwanza, wala si kwa anasa.

Sasa basi, enyi watoto, mnasaidiaje kuongeza mambo ya kimwili ya jamaa ili jamaa iwe na hali yenye furaha? Ni wangapi kati yenu walioshiriki katika kazi ya kukuza chakula katika shamba kwa ajili ya jamaa yenu wakati wa masika na wa kiangazi uliopita? Ni jambo linalofaa kujifunza kukuza chakula, kwa sababu huenda siku zenye magumu zikawa mbele na huenda wote wakahitajiwa washiriki katika kutafutia jamaa chakula. Je! wewe wasema kwamba unaishi mjini na huna shamba la kulima? Haya, basi, enyi vijana wa kiume ni vitu vingapi vilivyoharibika nyumbani ambavyo mmewasaidia wazazi wenu kutengeneza wakati wa miezi sita iliyopita? Nyakati zote kuna vitu vinavyohitaji kutengenezwa nyumbani, na havipaswi kuachiwa baba peke yake avitengeneze. Labda baba yako anaweza kukuzoeza na kukusaidia uwe ukitengeneza vitu vilivyoharibika nyumbani kutia na baisikeli.

Enyi vijana wa kike, je! mnapendezwa na kupikia jamaa yenu chakula? Je! mmejifunza kuoka maandazi na chapati? Hizi ni kazi zenye kupendeza ambazo akina mama wanaweza kushiriki na binti zao, Watoto hawapaswi kuruhusiwa wawe wavivu, wakipoteza wakati wao bure. Pahali pake, watoto wetu wanapaswa wakaribishwe wawe washiriki wa jamaa yenye furaha. Na tukuze roho ya kuwa wenye kusaidia katika kila mshiriki wa jamaa.

Katika njia hii hali yetu ya jamaa kwa kweli itakuwa ya rafiki wenye furaha​—⁠washiriki wenye upendo. Watoto wanahitaji kuwa rafiki wakubwa wa wazazi wao, wakiwa na uhuru wa kupashana habari nao juu ya matatizo (magumu) yote. Ninyi wazazi hampaswi kupiga ubwana juu ya jamaa. Mahali pake, baba anapaswa kuwa kama Yesu “Baba wa Milele,” aliyewafanya wanafunzi wake rafiki zake. Yesu alizungumza mambo ya siri na wanafunzi wake. (Isa. 9:6; Yohana 15:14) Vivyo hivyo, ninyi akina baba, iweni rafiki sana wa watoto wenu. Ni mpango mzuri kwa jamaa kuwa na wakati wa tafrija pamoja kama jamaa, ikipanga likizo kulingana na kupenda kwa kila mshiriki wa jamaa. Mwifanye igeuze mwendo, iwe yenye kujenga, yenye kupumzisha, yenye kuelimisha na isiyotumia fedha nyingi. Ufumbuzi wa kukuza hali bora ya jamaa ni kutumia wakati mkifanya mambo pamoja. Kushirikiana kwa njia halisi kunaunganisha jamaa.

NYUMBA YENYE UTARATIBU

Furaha ya jamaa inaonekana nyumbani nyakati zote. Nyumba inapaswa iwekwe ikiwa safi na yenye kupendeza. Washiriki wote wa jamaa wanaweza kushiriki katika kuweka nyumba yenye furaha katika njia safi na ya Kikristo, ili iwe na utaratibu, tayari kuwapokea wageni. Ndipo, hakuna mshiriki ye yote wa jamaa atakayeaibika anapowapokea wageni wake wanapomtembelea. Nyumba yenye utaratibu na yenye kupendeza inaonyesha hali safi ya kiroho ya Wakristo wa kweli.

Tena jamaa ya Kikristo yenye umoja huona kwamba sehemu ya nje inayoizunguka nyumba inawekwa ikiwa safi na nyasi imekatwa vizuri. Ili kupunguza kazi ya kuweka sehemu inayoizunguka nyumba ikiwa safi, jamaa nyingine wanaipamba kwa maua yasiyo mengi sana. Wanaepuka kuweka mapambo mengi ambayo ingetumia wakati mwingi wa kuitunza. Wakiwa na nyumba ambayo imepambwa kwa kiasi tu, vikundi vya jamaa vinaweza kufanya kazi pamoja kwa saa moja au mbili kila juma waiweke sehemu ya nje ya nyumba yao iwe kitu cha kuleta sifa katika ujirani wao. Na kwa hiyo jirani hatawashtaki jamaa ya Kikristo yenye shughuli (kazi) nyingi zinazofanywa mbali na nyumbani kwamba wameachilia nyumba yao iharibike kwa sababu ya shughuli (kazi) hizo. Wakati ule ule, washiriki wote wa jamaa wanaweza kuendeleza urafiki na jirani zao. Kukumbuka kwamba, sehemu za nje ya nyumba chafu na nyumba zisizotunzwa vizuri ndani zaweza kuwa ‘vikwazo’ kwa jira ni ambao bila hiyo wangeukubali ujumbe wetu wa Kikristo. Na tuache hali yenye furaha ya nyumba yenye utaratibu ionekane na jirani.​—⁠1 Kor. 10:32, NW.

BIBLIA INASAIDIA HALI YA JAMAA

Kusoma Biblia pamoja kama jamaa likawa jambo la kawaida katika Ulaya na Amerika katika karne ya 18 na 19. Mazungumzo ya ujumbe wa Biblia ulileta uongozi wa kiroho katika jamaa na yakawezesha kanuni za msingi za haki zikaziwe katika mioyo yenye kuitikia. Biblia ikawa chombo chenye nguvu cha kujenga hali bora ya jamaa katika nyumba nyingi.

Katika kame hii ya 20, Mashahidi wa Yehova wametilia mkazo maana kubwa ya funzo la Biblia la nyumbani. Mazungumzo ya kila siku ya maandiko pamoja na funzo kubwa zaidi la kila juma la Maandiko Matakatifu yametoa msingi wa umoja wa jamaa ya Kikristo. Si kwamba tu kumekuwa na kusoma na kusikia ile kanuni ya kuwatendea wengine kama vile ungetaka wao wakutendee (Mt. 7:12) pamoja na tunda la roho (Gal. 5:22, 23), bali pia (vilevile) jamaa zimeongozwa ziwe “watendaji wa neno” kweli kweli. (Yak. 1:22) Chini ya uongozi wa baba, mafundisho ya msingi ya kweli za Biblia yamezungumzwa katika njia ambayo inaamsha mioyo ya washiriki wote wa jamaa. Hii imewasaidia washiriki wa jamaa wawe na matokeo mazuri katika kuwafanyia kazi njema washiriki wengine kwa furaha na hata wale walioko nje ya jamaa. Kwa kutokuwa na choyo, jamaa zimeshiriki kuridhika ambako Yesu alitaja aliposema: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko zilivyo katika kupokea.”​—⁠Matendo 20:35, NW.

Kuwa na mazungumzo ya Biblia nyumbani kunaonyesha kutambua uhakika wa kwamba Yehova Mungu ndiye Baba mkuu na Mtoaji wa riziki kwa jamaa. (Yak. 1:17; Zab. 145:16) Katika njia hii uhusiano (ushirika) mzuri na Mungu si ule wa jamaa peke yake, bali pia na wa mtu binafsi unatiwa moyo na kuendelezwa. Utawa na kuridhika unakuwa faida kubwa kwa jamaa. (1 Tim. 6:6) Wote katika jamaa wanaona kwamba wanapendwa na wanahitajiwa, na wanatiwa moyo wamtumikie Yehova pamoja kwa moyo wote. Washiriki wa jamaa wanajiona kuwa wanalindwa na wako salama.

Katika nyakati za zamani, kulikuwako na sala za kila siku za jamaa katika jamaa zenye hali bora ya Kikristo. Sala hazikutolewa wakati wa chakula peke yake, bali pia wakati wa kumaliza siku wakati ambapo jamaa yote ilipiga magoti pamoja kwa heshima. Baba aliongea na Mungu aliwakilisha jamaa yote, akishukuru kwa sababu ya furaha waliyoipata katika siku hiyo na kuomba msamaha kwa makosa yao. Vivyo hivyo, katika nyakati hizi, jamaa za Mashahidi wa Yehova ‘wanakesha katika sala.’ (1 Pet. 4:7) Jamaa inayokaa karibu na Mungu kwa njia ya sala inasaidiwa katika kujenga hali bora ya jamaa.

UNYENYEKEVU NA NYUMBA

Wazazi wanyenyekevu wakiwa na akili nzuri ya Kikristo wanasikiliza upesi maoni ya watoto wao wenye furaha. Wote wawili baba na mama wanakuwa tayari kusifu na kuonyesha tumaini katika sifa njema za watoto wao. Wazazi hawapaswi wawe wepesi katika kulaumu watoto wao, sana sana mbele ya wengine, wakijaribu nyakati zote kujenga hali njema na ushirikiano kwa uthabiti na kwa fadhili, na kuweka wazi njia za kupashana habari na watoto wao. Wazazi hawapaswi kujifanya waonekane kana kwamba hawafanyi makosa hata kidogo, kwa sababu kufanya hivyo kungeleta kizuizi. Baba haachilii daraka lake alilopewa na Maandiko la kuwa kichwa, lakini hata hivyo anaweza kuwa mnyenyekevu. (Yak. 3:2) Huenda kukawa na nyakati atahitaji kujitoa makosa mbele ya jamaa yote na kutengeneza upya mengine ya maamuzi yake.

Wazazi hawapaswi kutazamia mengi mno kutoka kwa watoto wao au kuwa wakirudia-rudia udhaifu wa watoto. Kwa mazungumzo yenye kusudi na yenye kusaidia mezani, watoto wanaweza kutiwa moyo wafanye maendeleo katika mwenendo kwa njia yenye fadhili na unyenyekevu. Wanaposhughulika (maliza) na magumu ya jamaa, wazazi watafanya vizuri wakijaribu kuwa wenye kujenga na wenye furaha. Na ikumbukwe kwamba la pili katika matunda ya roho ni “furaha.” (Gal. 5:22) Tena, watoto hawapaswi kutazamia wengi mno kutoka kwa wazazi wao. Wao vilevile wanapaswa kuwa wanyenyekevu na wenye kufikiria wengine, wakingojea waongozwe na wazee wao.​—⁠Efe. 6:1-3.

Kunapokuwa na nafasi chache za watoto kushirikiana na watoto wengine Wakristo, wazazi wenyewe wanapaswa kuwa rafiki wema wa watoto wao na kushirikiana nao. Watoto wanapokuwa na rafiki wengi, wazazi watafanya vizuri kujuana na rafiki hawa wa watoto wao, na kuwa rafiki zao pia. Wazazi wanaweza kuwasaidia watoto wao wawe na rafiki wema kwa kuwaalika watoto wenye maoni mazuri nyumbani mwao, wakiwa na au bila wazazi wao.

Yehova aendeleapo kubariki watu wake kwa kuwapa riziki, na zaidi ya yote, kwa mipango bora ya kiroho, “nyumba” nyingi za watu wake duniani zimetayarishwa zionyeshe furaha kama ile ya jamaa Yake kuu ya ulimwengu wote. (Zab. 104:1, 14, 15; Mt. 4:4) Zinakuwa pahali pa amani ya kweli na usalama wa kweli ijapokuwa kuwe na migawanyiko iliyoko katika hizi ‘siku za hatari.’ (2 Tim. 3:1-5, 13) Kwa kweli hapapaswi pawe pahali pengine ‘kama nyumbani,’ kwa watoto na wazazi wanaothamini. Watoto wanapokuwa watu wazima, kumbukumbu zenye furaha na upendo kwa wazazi wao wanaoendelea kuzeeka zitawasukuma watembelee nyumbani kila wanapokuwa na nafasi, hata ingawa ni kwa saa chache tu ili wakumbuke vizuri na watoe shukrani kwa sababu ya amani, usalama na hali yenye kujenga waliyokuwa nayo katika wakati wa miaka yao ya mwanzoni. Ndiyo, nyumbani​—⁠hata iwe nyumba hiyo ya wakati wa utoto wetu ilikuwa ya kimaskini namna gani​—⁠inapaswa kutupa kumbukumbu njema za mazoezi mazuri pamoja na hali bora ya jamaa iliyojengwa imara juu ya msingi wa Neno la Mungu, Biblia.

[Picha katika ukurasa wa 15]

Jamaa yapaswa ijifurahishe pamoja tafrija isiyo na bei kubwa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki