Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 8/15 kur. 3-4
  • “Si Shauri Langu!”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Si Shauri Langu!”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UKATILI NA KUTENDA MABAYA HUTOKEZA KUTENGWA
  • MSAADA UNAOFAA USIPOTOLEWA
  • KUNAPOKUWA UONEZI
  • UHITAJI WA UPENDO NA KUTUMAINI
  • Usizishiriki Dhambi za Wengine
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Kwa Nini Lililo Baya Liripotiwe?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Ni Kosa la Nani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Iweni na Akili Mambo Yote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 8/15 kur. 3-4

“Si Shauri Langu! ”

JE! SIKUZOTE unaweza kusema hivyo? Maneno na matendo ya wengine yanakuwa na matokeo fulani juu ya watu. Nyakati nyingine, wanaweza kukasirika kwa haki, au kushuka moyo sana, kwa sababu ya matendo au maneno ya wenzao.

Pengine umekwisha kupatwa na mambo hayo. Hata hivyo, je! una hakika kwamba haujapata kuwa na daraka la kukasirika, kushuka moyo au kuteseka kwa wengine? Kweli kweli, unaweza kusema sikuzote, “Si shauri langu”?

UKATILI NA KUTENDA MABAYA HUTOKEZA KUTENGWA

Kwa kawaida, watu mmoja mmoja hutamani kuwa na angaa ushirika wenye kupendeza pamoja na wanadamu wenzao. Kwa kweli, mara nyingi watu wanaona huzuni sana wengine wakiwapuza. Huenda hata wakafikiri kwamba wale wanaoelekea kuwaepuka ni wale wasiojali au wasiopenda.

Hata hivyo huenda ikawa kwamba lawama yote si ya rafiki za mtu “anayepuzwa.” Mithali iliyoongozwa kwa roho inasema hivi: “Mtu mwenye fadhili za upendo anatendea nafsi yake mwenyewe kwa njia yenye kuthawabisha, bali mtu mkatili huuletea mwili wake mwenyewe kutengwa.” (Mit. 11:17, NW) Ndiyo, twaweza kujikaza wenyewe tunapokuwa wakatili na wasio na fadhili kwa wengine. Mwishowe, wale tunaowatendea vikali huenda wasipende ushirika wetu, hata kama ”‏wanatupuza” kwa sababu tu hawataki kuumizwa tena na ukatili wetu.

Vilevile twaweza kutengwa kwa sababu ya mwenendo wetu mbaya. Katika Israeli wa kale, vichwa vya jamaa ambao hawakutii amri za Mungu wangeweza kufanya nyumba zao zitengwe. Kwa mfano, Akani alimwibia Mungu kwa kujitwalia isivyofaa vazi fulani kutoka Shinari, shekeli za fedha na ufito wa dhahabu. Lakini kosa la Akani lilipofichuliwa, ‘Yehova alimtenga,’ naye pamoja na washiriki wa jamaa yake walipigwa kwa mawe mpaka kufa. (Yos. sura 7) Leo, kichwa cha nyumba ya Kikristo na wengine katika jamaa yake wanaweza kushiriki katika kosa ambalo laweza kufanya watengwe na ushirika wa kundi la Kikristo. Kwa kweli, mtu huyo anayevunja Neno la Mungu na kuruhusu utendaji wa kosa zito ndani ya jamaa yake ‘huitenga nyumba yake mwenyewe.’ (Mit. 11:29, NW) Yeye, na pengine wengine katika jamaa yake, wanatengwa kwa haki na Wakristo waaminifu, wakiondolewa katika ushirika wao kama wakosaji wasiotubu. (1 Kor. 5:11-13) Akielekeana na matokeo hayo ya kutenda kosa, mtu huyo hawezi kusema, “Si shauri langu! ”

MSAADA UNAOFAA USIPOTOLEWA

Bila shaka, wazee Wakristo wanapaswa kujitahidi kusaidia waamini wenzao ambao kwa kutokukusudia wanachukua hatua mbaya. Mtume Paulo analisema jambo hilo hivi: “Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lo lote, ninyi mlio [na sifa za kiroho] mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe.” (Gal. 6:1) Hata hivyo, wazee wa kundi waliowekwa wakikosa kutoa msaada wa kiroho wakati unapohitajiwa, je! wanakuwa hawana daraka kabisa iwapo mtu huyo mwenye kukosa anaangukia jaribu mwishowe?

Kwa upande mwingine, mambo mengi yanategemea juu ya namna msaada unavyotolewa. Paulo alisema kwamba wale walio na sifa za kiroho wanapaswa kurekebisha mtu huyo mwenye kukosa “kwa roho ya upole.” Lakini namna gani iwapo mzee hatoi shauri kwa upole, na kama matokeo mtu anayeshauriwa ashuke moyo sana, aghadhibike au kukasirika. Kwa sababu ya kutendewa vikali, mtu anayekosa huenda ‘asirekebishwe,’ na hata huenda akadumu katika mwendo mbaya. Chini ya hali kama hizo, je! mzee huyo asiye na fadhili aweza kusema kweli, “Si shauri langu”?​—Linganisha Luka 17:1, 2; 2 Wakorintho 6:3.

KUNAPOKUWA UONEZI

Kisha, pia, namna gani mtu mwenye mamlaka juu ya wengine akiwa mwenye kuonea? Kwa sababu ya kuwatendea kwa ukali, huenda wengine wakaona ni jambo linaloelekea kutowezekana kuwa na amani ya akili na hata huenda, kwa kweli, wakalazimika kujitahidi sana kuongoza roho zao. Jambo hilo halishangazi, kwa kuwa twaambiwa hivi katika Andiko hili: “Kweli [uonezi] humpumbaza mwenye hekima.”​—Mhu. 7:7.

Kwa hakika, uonezi wenye kuendelea muda mrefu unaweza kumfanya mtu mwenye hekima atende kwa kutokufikiri. kwa mfano, huenda akakosa kujiweza na kufanya jambo baya. Akifanya hivyo, je! mwonezi anaweza kuepuka daraka lote na kusema, “Si shauri langu”?

Kwa upande ule mwingine, Mhubiri 7:7 laweza kuhusu uonezi ambao mtu mwenye hekima hufanya, kutenda kinyume cha tabia ya kibinadamu na kujipofusha asione hali mbaya ya mwenye kuonewa. Anaweza kutenda kwa upumbavu kwa kuachilia roho ya uonezi imtawale naye aweza kujiona kuwa mfadhili mkubwa mwenye haki ya kuonea ye yote anayethubutu kulaumu njia zake. (Linganisha 2 Mambo ya Nyakati 16:10.) Walakini wazo lenye kosa la mwonezi huyo kwa hakika halimwondolei lawama.

UHITAJI WA UPENDO NA KUTUMAINI

Kwa asili, suala la kuwa na lawama linahusu sehemu nyingi za maisha. Kwa mfano, fikiria mwungano wa ndoa. Upendo, upole na kuhangaikiana ni vya lazima ili kuleta furaha katika ndoa. Lakini namna gani iwapo mwenzi wa ndoa anakosa kuonyesha sifa hizo? Na namna gani ikiwa yeye (mume) au yeye (mke) anakataa kwa makusudi na wakati wote haki za ndoa?

Chini ya mkazo wa kunyimwa huko, na ukosefu wa upendo, upole na kuhangaikia kikweli mwenzi aliyekataliwa anaweza kuangukia jaribu na kufanya uzinzi. Jambo hilo likitokea, je! mwenzi huyo wa ndoa asiye na upendo anaweza kukataa kuwa na daraka lo lote kwa kusema, “Si shauri langu”? Hata kidogo!

Mtume Paulo aliandika hivi ili kuzuia mambo hayo: “Msinyimane [haki za ndoa] isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu.”​—1 Kor. 7:1-5.

Mkristo awe anashughulika na mshiriki wa jamaa yake au mtu wa nje ya nyumba yake, anapaswa kutenda katika njia inayotokeza kutumaini. Mtu mwenye nia ya kutimiza makusudi yake bila kujali hali njema ya wengine anaweza kujaribiwa atumie mipango iliyopotoka, akiwaza kwamba kusudi lake ni zuri, ingawa njia anayotumia ni mbaya.

Lakini mara nyingi ni jambo gani linalotokea wakati wengine wanapogundua kwamba rafiki fulani ‘anasema uongo” (Mik. 6:12) Inaelekea kwamba hawatamtumaini mtu huyo aliyepotoka katika wakati ujao nao huenda wakajitenga sana naye. Inaelekea kuwa ataona jambo hilo linafadhaisha. Walakini iwapo anajiletea mwenyewe, je! yeye anaweza kusema, “Si shauri langu”?

Basi, kwa ujumla, wote wana lazima ya kumjibu Aliye Juu Zaidi. (Rum. 14:10-12) Jambo hilo linakazia umuhimu wa kukubali uongozi wa roho ya Mungu na Neno lake lililoongozwa kwa roho, huku tukidumu katika kusali tupate msaada ili sisi wenyewe binafsi tuepuke ukatili, kukosa, kutojali, njia za uonevu, kutenda bila upendo na kutokutumainika. Ndiyo katika hali nyingi, kwa lazima huenda isiwezekane mtu kuepa daraka kwa kusema tu, “Si shauri langu!”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki