Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 12/15 kur. 3-4
  • China na Ukristo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • China na Ukristo
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Habari Zinazolingana
  • Niko Huru! Baada ya Kutumia Miaka 20 Kizuizini
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Wamishonari wa Jumuiya ya Wakristo
    Amkeni!—1994
  • Uwezo Wenye Kutegemeza wa Neno la Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Sehemu ya 4—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 12/15 kur. 3-4

China na Ukristo

WATU elfu nyingi wanazuru China​—watalii waliokadiriwa kuwa 10,000 waliizuru mwaka jana. “Utakayoyaona,” yaripoti makala katika The Wall Street Journal, “ni vyumba vyenye nafasi kubwa, garimoshi zenye starehe, ndege zenye kusongamana watu kama kawaida, . . . chai bora sana pamoja na baadhi ya watu walio kati ya watu wenye adabu nzuri sana na wenye urafiki unaoweza kuwapata mahali po pote.” Lakini namna gani juu ya dini, na, sana sana Ukristo?

Dini haipendwi na watu wengi​—isipokuwa ile inayoitwa “dini nyekundu,” yaani, dini ya Kikomunisti. Ukristo sasa haupo kabisa. Taarifa ya habari iliyotumwa na Associated Press kutoka Peking Julai 31, 1978 ilisema hivi: “Makanisa mengi yamegeuzwa kwa matumizi mengine, kama shule, viwanda vya kutengenezea motokaa zilizoharibika au ghala. Kuna makanisa mawili ya Kikristo katika Peking, ambayo yanatumiwa hasa na wageni wanaoishi humo au wageni wanaozuru. Moja ni la Kikatoliki na jingine ni la Kiprotestanti.”

Ni kwa sababu gani kuna kupendezwa kidogo sana hivyo na Yesu na mafundisho yake? Bila shaka, Ukomunisti katika China umezuia dini ya namna hiyo. Walakini kuna zaidi ya hilo. Makanisa yamesingizia mafundisho ya Kristo, kama vile lilivyoripoti gazeti New York Times la Januari 15, 1979: ‘Umisionari wa nchi za Magharibi umeshirikishwa na siasa za nchi za Magharibi tangu wamisionari wa kwanza Wapresbyteri, Wamethodisti na Wakatoliki walipoingia nchini humo katika nusu ya pili ya kame ya 19.’

Ndiyo, inaelekea kwamba wamisionari wengi walitumikia zaidi kama mawakili wa serikali zao kuliko kuwa mawakili wa ufalme wa Mungu. Kulingana na ripoti ya mapema ya New York Times, baraza ya mataifa yote ya elimu ya dini ilitoa kilio hivi: “Ni bahati mbaya kwamba Ukristo ukiwa dini rasmi ya Magharibi ulifanywa katika njia nyingi uonyeshe ubeberu, uadui, ukoloni na ubepari kuwa mambo yanayofaa.”

Walakini, katika Juni wa 1947, wamisionari wawili Wakristo, wa namna iliyo tofauti kabisa na wamisionari wa makanisa ya Jumuiya ya Wakristo, waliingia China. Walikuwa Harold King na Stanley Jones, waliokuwa wamehitimu katika darasa la nane la Shule ya Gileadi. Walijiunga na kikundi kidogo cha Mashahidi wa Yehova huko Shanghai, China, wakashiriki pamoja nao katika kuhubiri ufalme wa Mungu nyumba kwa nyumba.

Baada ya muda fulani kupita, Stanley Jones alikutana na bibi wa nyumba Nancy Yuen wakati wa matembezi yake ya nyumba kwa nyumba. Ijapokuwa mumewe hakuwa akipendezwa na Biblia, Nancy alipendezwa, naye alipata kuona mara moja tofauti kati ya mafundisho ya Jumuiya ya Wakristo na mafundisho yenye msingi wa Biblia ya Mashahidi ya Yehova. Upesi yeye mwenyewe akawa Shahidi mwenye bidii sana. Alifanya maendeleo haraka sana, akajionyesha kuwa na bidii sana katika kazi ya nyumba kwa nyumba na katika kuongoza mafunzo ya Biblia, yote haya katika lugha ya Kichina.

Katika miaka michache iliyofuata mwaka wa 1950 watu wapata 175 walikuwa wakihudhuria mikutano huko Shanghai, ijapokuwa utendaji wa Mashahidi wa Yehova ulikuwa umewekewa vizuizi. Ndipo, katika mwaka wa 1956, Nancy Yuen alikamatwa na kuzuiliwa na wenye mamlaka. Wakati King na Jones walipouliza habari za hali yake, walijibiwa vikali hivi: “Hili ni jambo la Kichina. Angalieni mambo yenu wenyewe.” Miaka miwili baadaye, King na Jones wenyewe walikamatwa, wakafungwa mmoja miaka mitano na mwingine miaka saba katika gereza za Kichina kabla ya kufunguliwa na kufukuzwa nchini humo.

Lakini namna gani Nancy Yuen? Tunaamini kwamba utaona hadithi hii inayofuata inayomhusu kuwa yenye kupendeza kweli kweli.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki