Kwa Sababu Wanashikamana na Neno la Mungu
Unyofu na kushikamana na Neno la Mungu, Biblia, vinathawabisha katika njia mbalimbali. Jambo hilo linaonyeshwa waziwazi kutoka Afrika ya Kusini:
Katika miaka ya mapema ya kuanza na wa 1970 shahidi wa Yehova Mwafrika alianzisha biashara ndogo. Mara moja, akaajiri Wakristo wenzake. Alipojifunza kwamba tumbako (sigara) inahatirisha afya, na kwamba Wakristo hawapaswi kuitumia wala kuiuza, mwanamume huyo aliondoa tumbako yote iliyokuwa katika duka lake. Wenye duka waliokuwa jirani zake walimcheka, wakisema kwamba angefilisika kwa maana tumbako ndiyo bidhaa iliyokuwa ikiuzwa upesi zaidi katika sehemu zao za biashara.
Hata hivyo, ilishangaza jirani zake, wakati muda si muda Shahidi huyo alipopanua duka lake. Si kwamba tu lilikuwa kubwa zaidi kuliko yao, bali pia likawa duka kubwa zaidi la bidhaa la kwanza katika eneo hilo, likiwa na mkahawa na vyombo vya kulia pamoja na kituo cha petroli. Matukio hayo, katika mwaka 1976, yalibabaisha wenye maduka waliokuwa jirani, ambao walimwuliza namna alivyoweza kutimiza jambo hilo kwa muda mfupi hivyo, hali wao walikuwa wameng’ang’ana kwa miaka mingi wapate faida ili wasitawishe biashara zao.
Shahidi huyo alieleza kwamba wafanya kazi wake Wakristo walikuwa wenye kutegemeka na hata wasingeweza kumwibia peremende moja—si kwa sababu wanamwogopa mwenye kuwaandika bali kwa ajili ya kumwogopa Yehova Mungu. Vilevile, akataja kwamba bei zake zililingana na zile za Baraza yenye Kuongoza Bei napo mahali pake sikuzote ni pasafi.
Tangu wakati huo, wafanya kazi Mashahidi wanapatikana karibu katika kila duka katika mji huo, nalo ni jambo la kawaida kwa wenye kutafuta kazi kuulizwa hivi: “Wewe ni wa dini gani?” Nao Mashahidi wa Yehova wanapendelewa kama wafanya kazi. Sababu gani? Kwa sababu wanashikamana na Neno la Mungu nao wana sifa ya kuwa wenye kutegemeka na waaminifu.