Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 12/15 uku. 3
  • Endeleeni Kulinda!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Endeleeni Kulinda!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • ‘INUENI VICHWA VYENU JUU’
  • KESHENI!
  • Zile “Siku za Mwisho” na Ule Ufalme
    “Ufalme Wako Uje”
  • Ishara za Nyakati—Zina Maana Gani Kwako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Siku za Mwisho
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Uharibifu wa Ulimwengu Uliotabiriwa Utakuja Lini?
    Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 12/15 uku. 3

Endeleeni Kulinda!

MAKALA fulani yenye kichwa “Kuwaza juu ya Yasiyowazika” ilitokea katika gazeti New York Times la Februari 14, 1980. Humo maneno ya Dakt. Howard H. Hiatt, mkuu wa shule ya Harvard ya Afya ya Watu Wote, yalitajwa kuhusiana na matokeo yanayoweza kuletwa na kombora moja la nuklea “bila shaka likiwa si ndilo kubwa zaidi katika silaha,” juu ya eneo la mji wa Boston. Alisema hivi:

“Silaha moja hiyo inaweza kuharibu kila kitu kilicho umbali wa maili nne. Shimo ambalo lingelipuliwa na kombora lenyewe lingekuwa na urefu wa nusu maili toka upande huu hadi ule mwingine na kina cha futi mia kadha. Sehemu inayozunguka mviringo huo wa maili nne ulioharibiwa kamili mkazo mkubwa wa hewa, ukifuatwa na pepo zenye mwendo wa maili 1,000 kwa saa moja, waweza kutokeza moto mkubwa sana. Maili arobaini toka hapo, watu wenye kutazama upande ulipo mlipuko huo wangepofushwa kwa kuunguzwa kwa tabaka ya ndani-ndani ya jicho. Kati ya watu milioni 3 wanaoishi katika mji wa Boston, milioni 2.2 wangeuawa mara moja na mlipuko huo au moto mkubwa.”

Hayo ndiyo yangekuwa matokeo ya mwanzo iwapo moja tu ya maelfu ya makombora yaliyomo katika silaha za ulimwengu yangepiga mahali fulani.

Hakika, uwezekano wa “yasiyowazika” kuweza kutokea unatoa sababu nzuri ya kufikiri juu ya hali ya ulimwengu. Nao watu wengi wanafikiri. Ripoti maalum katika toleo la Februari 11, 1980, la gazeti U. S. News & World Report ilichanganua nguvu za kijeshi za mataifa yenye kuongoza duniani, kwa maneno haya ya mwanzo: “Mbele ya ulimwengu wenye kutazama kwa woga, Urusi leo inaonekana kama nguvu kubwa ya kijeshi, inayosonga mbele bila kuzuiliwa kwenye kuutawala ulimwengu mzima.” Hakika huu ni ulimwengu wenye kutazama kwa woga, kwa kuwa namna ya mauaji makubwa ambayo yangefuatana na vita vya makombora ya nuklea ni makubwa sana. Na hakuna shaka kwamba utawala wa dunia yote limekuwa ndilo suala kubwa katika nyakati zetu.

Je! kuna njia ya kusuluhisha hali hiyo ya siku ya maangamizi? Watu wengi wa-natazama kwa kukata tumaini. Wanaona mataifa yakiongeza hali hiyo kwa kuongeza maroketi, mizinga inayolipuka yenye kutupwa na manowari zinazopita chini ya maji, ndege zenye kutupa makombora zenye kuruka umbali mrefu, makombora ya nuklea na kadhalika. Wanapotazama, wanafahamu kwa kusikitisha kwamba hatari zenye kuogopesha sasa zinatisha toka mbinguni na baharini, kama alivyotabiri Bwana, Yesu, juu ya siku za mwisho wa taratibu mbovu ya mambo katika dunia hii. Yesu alisema hivi:

‘‘Kutakuwa na vituko vya kutisha na ishara kubwa kutoka angani. Kutakuwa na ishara katika jua na mwezi na nyota. Mataifa duniani yatakuwa na dhiki kwa sababu ya wasiwasi kutokana na mshindo wa mawimbi ya bahari. Watu watazirai kwa sababu ya woga, wakitazamia mambo yatakayoupata ulimwengu; kwa maana nguvu za anga zitatikiswa.”​—⁠Luka 21:​11, 25, 26, HNWW.

‘INUENI VICHWA VYENU JUU’

Mambo yalivyo yaweza kuwa yenye kuogopesha sana kwa wale wanaotazama matukio kwa maoni ya kilimwengu tu. Hata hivyo Yesu aliendelea kusema hivi:“Wakati mambo hayo yatakapoanza kutendeka, simameni na kuinua vichwa vyenu juu, kwa maana ukombozi wenu umekaribia.” (Luka 21:​28, HNWW)

Kwa hiyo hakuna sababu ya kuogopa kwa upande wa wale wanaotazama matukio ya ulimwengu kwa maoni ya imani katika Neno la kiunabii la Yehova. Mahali pa kuwa na mawazo yenye woga juu ya yale yanayoweza kutokea katika mauaji makubwa ya makombora ya nuklea, wanatazamia kwa uhakika ukombozi wa Mungu ulioahidiwa.

Je! wewe ni mmoja anayetumainia kurudi kwa hali zilizo salama zaidi kati ya wanadamu? Basi wapaswa kukaza fikira kwenye maelezo ya Yesu juu ya maana ya nyakati zetu. Tangu kutokea kwa Vita ya Ulimwengu ya Kwanza, taabu ya mataifa, uvunjaji wa sheria, uhalifu, upungufu wa chakula, matetemeko ya ardhi, magonjwa ya kuenea na taabu nyingine zimekuwa zikiongezeka sana duniani, kama vile tu Yesu alivyotabiri zingetokea, ili kuonyesha ‘ishara ya kuwapo kwake na ya mwisho wa taratibu ya mambo.’ (Mt. 24:​3-12, NW; Luka 21:​10, 11) Walakini aliongeza maneno haya: “Mtakapoona mambo hayo yanatendeka, mtatambua kwamba Utawala wa Mungu umekaribia. Nawaambieni hakika, kizazi hiki cha sasa hakitatoweka kabla ya hayo yote kutendeka. Mbingu na dunia vitapita, lakini maneno yangu hayatapita.”​—⁠Luka 21:​31-33, HNWW.

Baadhi ya watu wa kizazi kilichoona mwanzo wa kipindi hiki cha uvunjaji wa sheria katika mwaka 1914 wanatazamia kuwapo kimalizikapo. Huo utakuwa wakati wa kutimizwa kwa Danieli 2:​44, kwa habari ya “wafalme” au watawala ambao sasa wanashindania kwa choyo utawala wa ulimwengu: “Katika siku za wafalme hao Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaangamizwa milele, . . . bali utavunja falme hizi zote vipande vipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele.” Silaha za nuklea za mataifa hazitafaa kitu zitakapokutana na uwezo wa ufalme wa Mungu chini ya Kristo Yesu. Huyu “Mfalme wa wafalme” atawahukumu mataifa kwa haki, akiwaharibu waovu na kuwalinda wapole ambao wameweka ulinzi. Lo! baraka za Ufalme zitakazofuata zitakuwa bora kama nini! “Wenye upole watairithi [dunia], watajifurahisha kwa wingi wa amani.”​—⁠Zab. 37:​10, 11; Ufu. 19:​11-21.

KESHENI!

Kuelekea mwishoni mwa unabii wake juu ya mwisho wa taratibu ya mambo, Yesu alitoa onyo hili: “Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafula, kama mtego unasavyo, kwa kuwa ndivyo itakavyowajilia watu wote wakaao juu ya uso wa dunia nzima.” Katika siku hiyo ya kisasi cha Mungu juu ya mataifa maovu na watu wenye kuvunja sheria, watu peke yake watakaosalimika ni wale watakaopata hukumu inayofaa kutoka kwa “Mwana wa Adamu,” Kristo Yesu. Watu wote wanaotaka kuokoka wanapaswa kutii shauri la Yesu: “Kesheni ninyi kila wakati, mkiomba, ili mpate kuokoka katika hayo yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.”​—⁠Luka 21:​34-36.

Katika kumalizia unabii uo huo, kulingana na masimulizi ya Marko, Yesu alisema hivi: “Angalieni, kesheni, kwa kuwa hamjui wakati ule utakapokuwapo. . . . [Lindeni] basi, . . . asije [Bwana] akawasili ghafula akawakuta mmelala. Na hilo niwaambialo ninyi, nawaambia wote, [Lindeni].” (Marko 13:​10, 33-37) Linaloshiriki katika kazi hii kubwa ya kutoa ushuhuda ulimwenguni pote ni gazeti Mnara wa Mlinzi, ambalo sasa linaingia katika mwaka wake wa 102 wa kuchapwa (Kiingereza). Inatumainiwa kwamba kurasa hizo zitaendelea kufariji mamilioni ya wasomaji wetu, likiwatia moyo wote ‘LINDENI.’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki