Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 6/15 kur. 17-24
  • ‘Kuzaa Matunda Katika Kila Kazi Njema’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Kuzaa Matunda Katika Kila Kazi Njema’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MAONGEZEKO YENYE KUTIA MOYO
  • MAMBO YALIYOONWA SHAMBANI
  • VIJANA WANAZAA MATUNDA
  • USHINDI WA KISHERIA
  • 1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Sehemu ya 4—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Sehemu ya 5—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • “Kutetea na Kuthibitisha Kisheria Habari Njema”
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 6/15 kur. 17-24

‘Kuzaa Matunda Katika Kila Kazi Njema’

KWA SABABU ya kufuata maagizo ya Kimaandiko yaliyokaziwa katika makala mbili zilizotangulia, kweli kweli Mashahidi wa Yehova wamekuwa wenye “kuzaa matunda katika kila kazi njema.” (Kol. 1:10 NW) Si kwamba tu wanahubiri na kufundisha kwa juhudi, lakini pia wanaripoti utendaji wao ili watangazaji wengine wa Ufalme wafurahie.

Kwa kufanya hivyo wana mifano mizuri iliyotangulia ya Kimaandiko. Kwa mfano, katika Matendo 2:41 twasoma kwamba, baada ya hotuba yenye kuamsha ya Petro, pamoja na kuhubiri kwa wanafunzi wale wengine, “siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu.” Kisha, muda mfupi baadaye, kuhubiri zaidi kwa juhudi kulitokeza ongezeko la wanafunzi wakawa “kama elfu tano.” (Matendo 4:4) Na wakati waongofu wapya Wakristo walipobatizwa katika Efeso, masimulizi ya Biblia yanasema hivi: “Jumla yao walipata wanaume kumi na wawili.”—Matendo 19:2-7.

MAONGEZEKO YENYE KUTIA MOYO

Mwaka wa utumishi wa 1980 wa Mashahidi wa Yehova, ulioanza Septemba 1, 1979, na kumalizika Agosti 31, 1980, kwa hakika umekuwa mzuri sana. Ulimwenguni pote pamekuwako ongezeko la asilimia (%) 3.7 katika hesabu ya wanaohubiri ujumbe wa Ufalme. Hakika inasisimua kuona namna nchi baada ya nchi ilivyoonyesha maongezeko, kwani mwaka uliopita kulikuwako upungufu. Kwa mfano, mwaka uliopita kazi huko Paraguay ilikuwa na upungufu wa asilimia 11, bila shaka kwa ajili ya magumu yaliyoongezeka ya kisheria. Mwaka huu kazi huko ilikuwa na ongezeko la asilimia 13, ikasawazisha na kupita upungufu wa mwaka jana. Katika Filipino, baada ya kuwa na upungufu wa miaka kadha, walikuwa na ongezeko la asilimia 2. Mwaka jana Korea ilikuwa na upungufu wa asilimia 1 walakini mwaka huu ilikuwa na ongezeko la asilimia 6. Uruguay ilikuwa na upungufu wa asilimia 2 mwaka jana na mwaka huu ikawa na ongezeko la asilimia 9.

Nchi nyingine nyingi zilikuwa na maongezeko mazuri kuliko mwaka uliopita. Kwa hiyo, katika Bolivia kulikuwako ongezeko la asilimia 1 mwaka uliopita, walakini mwaka huu kulikuwako ongezeko la asilimia 7. United States mwaka jana pia ilikuwa na ongezeko la asilimia 1, walakini mwaka huu ongezeko limekuwa asilimia 4. Mwaka jana Jamaica ilikuwa na ongezeko la asilimia 1 walakini mwaka huu ikawa na ongezeko la asilimia 11. Venezuela, ambayo mwaka jana iliripoti ongezeko la asilimia 3, mwaka huu iliripoti ongezeko la asilimia 9. Japan, ambayo mwaka jana ilikuwa na ongezeko la ajabu la asilimia 10, ilifanya vema zaidi kwa kuwa na ongezeko la asilimia 11.

Katika Ubelgiji Mashahidi Waitalia wanaonyesha juhudi yenye kutokeza sana nao wanakuwa na matokeo yenye kutokeza sana. Sasa kuna makundi ya Kiitalia 31 yakiwa na jumla ya Mashahidi 2,500. Hiyo inamaanisha kwamba 1 kati ya kila Waitalia 100 wa Ubelgiji sasa ni Shahidi. Kwa kweli, wakati mwingi Shahidi anapata Mwitalia mwenye jirani, rafiki au mtu wa ukoo ambaye ni Shahidi.

MAMBO YALIYOONWA SHAMBANI

Zenye kuburudisha hasa ni ripoti za mambo yaliyoonwa na Mashahidi walipokuwa wakishiriki katika kazi ya kuhubiri. Katika Ireland vipande vya kusanyiko vilivyovaliwa na Mashahidi vilivuta fikira za walevi sita waliokuwa wakiishi katika vibanda vilivyokuwa katika bustani. Mmoja wao alionyesha kupendezwa kweli kweli naye akajipatia kitabu Life Does Have a Purpose. Aliacha kutumia vileo baada ya mazungumzo zaidi ya Biblia.

Kwa kufahamiana na kanuni za Biblia, mtu huyo aliona uhitaji wa kufanya kazi na hivyo akatafuta kazi, pia akahamia kwenye nyumba ya kukodisha katika bustani hiyo. Sura yake ikabadilika sana alipofupisha nywele zake akanunua suti. Alipofika mahakmani, kwa ajili ya kosa alilokuwa amefanya kabla ya kujifunza kweli, alionekana mwenye kuheshimika sana hata kwamba hakimu akamwachilia kwa shtaka hilo naye akamsifu kwa ajili ya sura yake.

Alipokuwa akihudhuria “Upendo wa Kimungu” Kusanyiko la Mashahidi wa Yehova katika Dublin, mlevi huyo wa zamani alitembelea watu wa ukoo wake, ambao mbeleni walikuwa wamemkataza asiingie nyumbani mwao. Wasingeweza kuamini waliyoona nao wakaona vigumu kuamini kwamba ndiye yule yule. Sasa anahudhuria mikutano ya Mashahidi kwa ukawaida naye anaendelea kuhubiri mapolisi, wakuu wa mahakma na wafanya kazi wenzake.

Jambo lililoonwa lifuatalo linatoka kwa Shahidi mmoja katika Argentina. “Nilikuwa naenda nyumba kwa nyumba na mtu mmoja akaniuliza kama nilikuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Kwanza nikasita kwa sababu sikuwa na hakika alikuwa na kusudi gani, kwa kuwa kazi hapa imewekewa vizuizi vya kisheria. Walakini alipojua kwamba nilikuwa mmoja wao akauliza ajifunze Biblia pamoja nami. Mpango ukafanywa. Kwa kweli, nilirudi siku iyo hiyo na tukaanza funzo la Biblia tukitumia kitabu Kweli Iongozayo kwenye Uzima wa Milele. Katika muda wa juma moja alikuwa amesoma kifaa hicho cha Biblia na kukimaliza naye alikuwa ameanza kusoma Biblia. Nikamwuliza sababu ya kutaka kujifunza Biblia pamoja nami, akaniambia ni kwa sababu ya badiliko kubwa ambalo wenzi wawili wa ndoa jirani zake walikuwa wamefanya maishani mwao. Walikuwa wamekaribia kuachana kwa sababu hawakusikizana. Wakaanza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova, na lo! badiliko likatokea maishani mwao! Sasa wanasikizana. Mara moja mwanamume huyo akaamua kubadili dini yake, na sasa anafunza watoto wake mambo anayojifunza.”

Vilevile “kuzaa matunda katika kila kazi njema” kunatia ndani kuonyesha upendo Wakristo wenzetu. Ndugu mmoja katika Ulaya alisoma hadithi katika toleo la gazeti Mnara wa Mlinzi (Kiingereza la Aprili 15, 1978) ambayo ilisema juu ya Shahidi wa Panama aliyepoteza mikono yake miwili. Akaandikia ofisi ya tawi ya Sosaiti, akasema kwamba angependa kumsaidia ndugu huyo kiwete kwa kumpa mikono ya kutengenezwa, na kwamba angelipa gharama zote. Mipango ikafanywa hilo lifanyiwe Mexico. Ndugu huyo kiwete alipokewa kwa furaha na akina ndugu huko. Sasa amerudi nyumbani, na wazia furaha yake kuweza kushika kalamu katika “mkono” mmoja na kuandika jina lake, jambo ambalo hakuweza kufanya kwa muda wa miaka zaidi ya 30!

Barua ya kutia moyo kazi inayofanywa na Mashahidi wa Yehova ilipokewa na afisi ya tawi ya Austria. Ilisema hivi:

“Nimewaza-waza kwa muda mrefu niandike au nisiandike barua hii. Najua kwamba ninyi huenda nyumba kwa nyumba ili mletee watu habari njema.’ Najua kwamba sikuzote hii si kazi yenye kufurahisha, kukabiliana siku baada ya siku na watu wagumu walakini usipoteze juhudi na urafiki. Huenda wengine wenu mkafikiri kwamba watu hawana shukrani, na kwa hiyo ningependa kuwashukuru, kwa kunitumia mtu. Kama isingekuwa ni utendaji wenu wa kuhubiri, bila shaka ningetembea katika njia pana. [Mt. 7:13, 14] Hata hivyo, kwa sababu yenu nimepata nafasi nzuri ya kujua mapenzi ya Mungu. Kwa hiyo ningependa kusema jambo hili moja: Upendo uliopatikana na shukrani za unyofu zastahilisha milango elfu iliyofungwa. Pamoja na kuvutiwa sana na kazi yenu.”

VIJANA WANAZAA MATUNDA

Mambo yafuatayo yaliyoonwa katika kisiwa cha Jamaica yanaonyesha kwamba watoto wadogo pia wanaweza kuzaa matunda yamletee Mungu sifa: Baba mmoja alienda kumchukua mvulana wake mwenye umri wa miaka mitano baada ya shule. Alipokosa kumwona, baba huyo akaamua atangoja amwache kivulana huyo amtafute. Baada ya muda mfupi aliona kikundi cha watoto wamkusanyika naye akataka kujua waliyokuwa wakifanya. Baba huyo alichunguza na kumpata mvulana wake kati yao akiwahubiri kwa nakala ya My Book of Bible Stories.

Msichana mdogo Shahidi, alipopata shilingi 7 hivi akiwa shuleni, alimpa mwalimu wake. Muda mfupi baada ya hapo fedha fulani ziliibwa naye mwalimu akaonya kwamba darasa zima lingeadhibiwa iwapo fedha hizo zisingerudishwa; wote wangeadhibiwa, isipokuwa msichana huyo Shahidi, maana mwalimu huyo alijua kwamba mtoto huyo Shahidi hangeweza kuchukua fedha hizo.

USHINDI WA KISHERIA

Vilevile kuna sehemu nyingine za “kuzaa matunda katika kila kazi njema.” Mtume Paulo aliandikia kundi alilopenda la Filipi: “Ni haki kabisa kwangu kufikiri haya juu yenu nyote, kwa ajili ya kuwa nanyi katika moyo wangu, ninyi nyote mkiwa washiriki pamoja nami katika fadhili zisizostahilika, katika vifungo vya gereza na katika kutetea na kuimarisha kisheria habari njema.” (Flp. 1:7, NW) Bila shaka baadhi ya ushindi wa kisheria umetokea pia kwa sababu Mashahidi wa Yehova wanafuata shauri la mtume Paulo linalopatikana katika 1 Timotheo 2:1, 2: “Basi, kabla ya mambo yote, nataka dua, na sala, na maombezi, na shukrani, zifanyike kwa ajili ya watu wote; kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, tuishi maisha ya utulivu na amani, katika utauwa wote na ustahivu.”

Ndivyo ilivyokuwa barua iliyopokewa kutoka Bangui, Jamhuri ya Afrika ya Kati, ya tarehe ya Oktoba 1, 1978. Ilisema kwamba katika Septemba 27 radio ya taifa ilikuwa imetangaza waziwazi kwamba marufuku ya Agosti 19, 1976, yaliyopigwa juu ya Mashahidi wa Yehova yalikuwa yameondolewa, na kwamba walikuwa na ruhusa ya kuhubiri tena kwa uhuru katika eneo lote la Jamhuri ya Afrika ya Kati. Hiyo ilikuwa sababu ya kufurahi hasa, maana amri hiyo ilitolewa na serikali ambayo ilikuwa imetawala kwa juma moja tu.

Katika Aprili 1980 kazi ya Mashahidi wa Yehova katika Zaire ilikubaliwa kisheria na serikali. Mwezi mmoja kabla ya hilo Mashahidi wa Yehova walipata ushindi wa kisheria katika Uturuki. Mwaka uliotangulia huo Mashahidi 42 walikuwa wameondolewa shtaka la kufitini serikali na kuvunja Sheria ya Laicism (Amri ya Serikali). Kesi hiyo ilikatwa rufani na mkuu wa sheria na kwa hiyo ikaenda kwenye Mahakma Kuu ya Kukata Rufani ya Uturuki. Nao Mashahidi wakashinda kesi. Kwa sababu ndiyo mahakma kuu katika Uturuki, mahakma nyinginezo zinapaswa na uamuzi wayo. Mojalapo la mambo iliyosema, ni hili:

“Iwapo siku moja yatatokea mambo ambayo washtakiwa wanasadiki nao utawala wa Mungu usimamishwe juu ya ulimwengu, washtakiwa wakiadhibiwa, kwa sababu ya sadikisho hilo, matukio hayo hayatabadilika. Walakini ikiwa tazamio lao ni wazo tu na sadikisho lisilo na ukweli, basi masadikisho yao hayawezi kuharibu utaratibu wetu wa serikali ya Taifa.” Bila shaka huo ni uamuzi mzuri, unaotukumbusha aliyosema Gamalieli juu ya Wakristo wa kwanza na mafundisho yao, kama ilivyoandikwa katika Matendo 5:34-40.

Ripoti na mambo yote hayo yaliyoonwa hakika yanaburudisha kama maji ya baridi kwa mtu mwenye kiu.”(Mit. 25:25) Vilevile yanaonyesha kwamba Yehova anatimiza ahadi yake, kwamba tukileta “zaka” zetu, katika nyumba yake ya ibada atatubariki sana. (Mal. 3:10) Wakristo wote waliojiweka wakf na wajikaze vivyo hivyo, wakikumbuka kwamba “apandaye kwa ukarimu atavuna kwa ukarimu.”—2 Kor. 9:6.

[Chati katika kurasa za 18-21]

REPOTI YA UTUMISHI YA MASHAHIDI WA YEHOVA YA 1980

(Ona nakala yaliyochapwa)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki