Sasa Ndio Wakati wa Kulihubiri Neno
“Kila siku katika hekalu na kutoka nyumba kwa nyumba waliendelea bila kuacha kufundisha na kutangaza habari njema juu ya Kristo, Yesu.”—Matendo 5:42, NW.
1, 2. (a) Katika Biblia tuna maandishi ya matokeo gani ya karne ya kwanza ya kuhubiriwa kwa Ufalme? (b) Yesu alionyeshaje katika Mathayo 28:19, 20 na Matendo 1:8 kwamba kuhubiri ndiko kungekuwa kazi ya wafuasi wake?
BAADA ya kumiminwa kwa roho takatifu siku ya Pentekoste, wafuasi wa Yesu Kristo walitiwa nguvu na uhodari wa kuendelea bila kuacha kufundisha na kutangaza habari njema juu ya Kristo Yesu. Matokeo yalikuwa nini katika karne hiyo ya kwanza? Tunaelezwa kwamba wengi kati ya wale waliokuwa wamesikiliza ujumbe huo wa wafuasi wa Yesu walipata kuwa waamini. Kwa kweli, hesabu ya wanaume walioamini jumla yake ilipata kuwa 5,000. (Matendo 4:4) Katika pindi nyingine maandishi ya Biblia yanasema kwamba waamini katika Bwana waliendelea kuongezwa, umati wa wanaume na wanawake.—Matendo 5:14.
2 Baada ya muda mfupi sana, baada ya Pentekoste, kwa halisi maelfu walikuwa waamini ikiwa ni matokeo ya wafuasi wa Yesu kutokuacha kufundisha habari njema juu ya Kristo. Inasisimua kusoma matendo ya wale walioshiriki katika utangazaji huo wa “habari njema” katika karne ya kwanza ya Wakati wa Kawaida wetu muda mfupi tu baada ya kifo na kufufuliwa kwa Yesu, na kumiminwa kwa roho takatifu ili watimize kazi hiyo nzuri ajabu. Ndugu na dada zetu waaminifu wa karne ya kwanza walikuwa wafanya kazi kweli kweli, wafanya kazi wenye bidii, walifanya jambo walilogawiwa na Bwana Yesu Kristo.—Mathayo 28:19, 20, NW; Matendo 1:8, NW.
3, 4. (a) Katika nyakati za kisasa, ni wakati gani mambo yalipotayarishwa ili kuanzisha tena kazi ya kuhubiri? (b) Yehova alihakikishaje kazi yake imetimizwa, Jumuiya ya Wakristo ijapozuia utendaji wa kuuhubiri Ufalme, na matokeo yalikuwa nini katika wakati wenye msukosuko zaidi katika historia ya wanadamu?
3 Je! hayo yamepungua katika kame hii ya 20? Ebu tuyachunguze mambo ya hakika. Kumbuka jambo hili juu ya karne ya kwanza na juu ya mwanzo wa Ukristo: Ulianzwa na mtu mmoja, Bwana Yesu Kristo. Kwa muda mfupi wa miaka mitatu na nusu ulikua kwa kadiri kubwa hata wapinzani wake wa kidini wakasema: “Tazameni, ulimwengu umekwenda nyuma yake.” (Yohana 12:19) Katika siku zetu, sana-sana kuelekea mwisho wa karne ya 19, wakati ulikuwa unakaribia ili kazi kubwa ya kuvuna ya Yehova Mungu kupitia Kristo Yesu ianze. (Mathayo 13:24-30, 36-43) Jumuiya ya Wakristo ilikuwa imekuwa uwanjani kwa karne nyingi, walakini badala ya kusitawisha nuru ya kweli kuhusu habari njema juu ya Kristo Yesu na ufalme ambao Wakristo walipaswa kuwa wakiomba na kuutazamia, ilikuwa ikificha nuru hiyo kwa mafundisho mengi ya uongo yayo. Hata hivyo, Yehova hangeweza kuzuiwa wakati ulipokaribia ili Mwanaye atwae uwezo wa Kifalme. Kupitia kikundi cha wanafunzi wa Biblia wenye bidii roho takatifu ya Yehova ilianza kuwapa ufahamu wale wenye kupenda haki na wenye kutaka kwa unyofu kufanya mapenzi na kazi yake. Matokeo yamekuwa yenye kusisimua tangu siku hizo za mapema, kama vile yalivyokuwa katika karne ya kwanza. Imekadiriwa kwamba katika miaka iliyotangulia kidogo tu karne ya 20, kulikuwako 4,000 waliokuwa wakishiriki katika kutangaza waziwazi tumaini lao.
4 Miaka 80 hivi tangu mapambazuko ya mwaka 1900, tunaona kwamba katika kipindi chote chenye msukosuko zaidi katika historia ya kibinadamu Yehova ameendelea kuongeza hesabu ya wahudumu wale wanaotangaza habari njema juu ya Kristo na ufalme wake. (Linganisha Matendo 16:5.) Na mwaka wa utumishi wa 1981 wa utendaji wa Mashahidi wa Yehova umeleta baraka nyingi kwa watangazaji wa Ufalme ulimwenguni pote.
NI MAMBO GANI YAMEKUWA YAKITOKEA?
5. (a) Ni kupendezwa gani wakati wa mwaka 1981 kulikoonyeshwa katika kukikumbuka Chakula cha Jioni cha Bwana na Mashahidi wa Yehova na watu wenye kupendezwa? (b) Kati ya wale waliohudhuria, ni wangapi walioshiriki kadiri fulani katika kutangaza waziwazi Ufalme katika mwaka huo?
5 Tukielekeza fikira zetu kwanza kwenye siku ya maana zaidi kwenye kalenda ya Kikristo, mwadhimisho wa Chakula cha Jioni cha Bwana katika kukumbuka kifo cha Kristo, katika makundi 43,870 ulimwenguni pote wakati wa mwaka 1981 kulikuwako watu 5,987,893 waliokusanyika katika Jumapili, Aprili 19 (Nisani 14, katika kalenda ya Kiyahudi), kwa mwadhimisho huo. Mamilioni hao walisikia maana ya kweli na iliyo sahihi ya kifo cha Bwana kama inavyofundishwa na Biblia ikizungumzwa. Kati ya hesabu hiyo ulimwenguni pote katika mwaka wa utumishi wa 1981, kulikuwa 2,247,486 walioshiriki kwa ukawaida katika kuhubiri na kufundisha habari njema za Ufalme katika nchi na visiwa 206. Na kulikuwako kilele cha Mashahidi 2,361,896 ambao wakati fulani mwakani walishiriki katika huduma hiyo waliyogawiwa na Mungu. Walitimiza mambo gani? Ujumbe wao wa kusaidia watu ni wenye matokeo kadiri gani? Ebu tuone.
KUENEZA NENO LILE
6. (a) Ni mafundisho ya kidini ya nani yametawala katika Amerika ya Kati na ya Kusini kwa karne nyingi na jambo hilo limetokeza matokeo gani? (b) Hata hivyo, ni badiliko gani limekuwa likitokea katika nchi hizo?
6 Ukatoliki wa Roma umetawala kuwaza kwa Waamerika wa Kati na Kusini kwa karne nyingi, na hilo likafanya wengi wa watu wathamini kidogo sana mafundisho ya kweli ya Biblia. (2 Wakorintho 4:4) Kwa sababu hiyo, pasipo maarifa ya Kristo Yesu na habari njema za Ufalme, watu hao wametendewa bila huruma na kwa ukatili, sawa na hali ambayo Yesu aliona kati ya Wayahudi wa siku zake waliokuwa chini ya uongozi wa kikatili wa waandishi na Mafarisayo. (Mathayo 9:36) Hata hivyo, kwa sababu ya baraka ya Mungu juu ya utendaji wa kuhubiri wa karne ya 20 katika nchi hizo za Amerika ya Kati na Kusini, badiliko la ajabu linatokea. Kwa kadiri ambavyo nuru imeng’aa kati ya giza la kiroho linaloifunika dunia, maelfu ya watu wenye mioyo minyofu wamekusanywa kwenye tengenezo la Yehova.—Isaya 60:1, 2, 8.
7. Simulia jambo zuri lililoonwa la msichana mmoja mwenye umri wa miaka 12 katika Argentina.
7 Kweli ya Biblia inaletea badiliko watu wa umri wote, na kuwasaidia waunge mkono ufalme wa Yehova. (Zaburi 119:129, 130) Mhubiri mmoja mwenye umri wa miaka 12 katika Argentina, ambaye bado hajabatizwa, alieleza juu ya furaha nyingi ya kuongoza mafunzo ya Biblia ya nyumbani manane. Yeye aliandika hivi: “Sana-sana wakati wa likizo ninatumia wakati mwingi iwezekanavyo katika kazi ya mlango kwa mlango, ziara za kurudia na kazi ya mafunzo ya Biblia. Utendaji huo wote unanifanya nijisikie mwenye furaha sana na mwenye kupendelewa sana kutumiwa na Yehova nikiwa chombo mikononi mwake cha kuwasaidia watu wengi wapate kumjua yeye kuwa Mungu wa kweli. Ninaomba kwamba sikuzote niwe na pendeleo hilo.” Yeye anapanga kubatizwa karibuni na kuendelea afikie mradi wake awe painia. Wazia hayo yote yakifanywa na kisichana cha miaka 12! Tuna msukumo mkubwa kama nini katika Neno la Mungu wa kuleta mawazo yanayofaa!
8. Ni upanuzi gani mzuri ajabu wa watangazaji wa Ufalme umetokea katika Amerika ya Kati na ya Kusini tangu mwaka 1945?
8 Katika mwaka 1945, mwishoni mwa vita ya ulimwengu ya pili, iliyokuwa imeharibu dunia yote, katika Amerika ya Kati na Kusini, kutia Mexico, kwa jumla kulikuwa watu 4,720 walioshiriki kuhubiri habari njema za Ufalme. Katika mwaka wa utumishi wa 1981 katika nchi izo hizo “habari njema” zilikuwa zikihubiriwa na kilele cha wahubiri 373,919. Kweli kweli maji ya kweli yametolewa katika nchi hizo kavu na wenye kiu wameitikia kwa njia nzuri ajabu.—Linganisha Yohana 7:37, 38.
9. Hali ya watangazaji wa Ufalme katika Ulaya imekuwa nini tangu mwanzo wa karne ya 20?
9 Habari njema za Ufalme zimetia mizizi sana katika nchi nyingi za Ulaya. Tangu siku za mapema za karne ya 20, na hata kabla ya hapo katika nchi fulani, Mashahidi wa Yehova, wakati huo wakijulikana kama Wanafunzi wa Biblia wa Mataifa Yote, walikuwa wakieneza habari njema za Ufalme kati ya watu. Kwa mfano, maandishi ya kwanza ya kutolewa kwa ushuhuda wo wote katika Ujeremani ni ya mwanzoni mwa karne ya 20. Msimamizi wa kwanza wa Sosaiti, Charles T. Russell, alizuru Ujeremani katika mwaka 1891, na baada ya hapo mipango ilifanywa ili kuchapisha vitabu na vikaratasi fulani katika lugha ya Kijeremani. Makundi yenye kusema Kijeremani yalianzishwa kwa mara ya kwanza muda mfupi baada ya mwaka 1901 katika Ujeremani.
10. Ni jambo gani lililoonwa kutoka Ujeremani linaloonyesha huduma ya nyumba kwa nyumba imeendelea kuwa na matokeo?
10 Mpaka leo hii watu wa Yehova katika Ujeremani wanaona kwamba kazi ya nyumba kwa nyumba ni njia yenye matokeo zaidi katika kueneza habari njema hizi za ufalme wa Yehova kwa watu. (Luka 9:1-6) Baada ya kutoa ushuhuda kwa wenzi wa ndoa katika kazi ya nyumba kwa nyumba, watu 12 kufika 14 walikusanyika baadaye kwa funzo la Biblia la nyumbani lililokuwa limeanzishwa. Baadaye jamaa hiyo ilihamia Australia na huko jamaa yote, isipokuwa binti mmoja aliyeolewa, iliendelea kujifunza na Mashahidi wa Yehova. Wakati huu mama na baba wamekwisha kubatizwa.
11. Shahidi mmoja wa Yehova mzee-mzee na aliyelemaa katika Berlin ya Magharibi anaonaje juu ya huduma yake?
11 Maelezo ya dada mmoja mwenye umri wa miaka 84 katika Berlin ya Magharibi ambaye, ingawa amelemaa sana, anaweza kushiriki katika kazi ya upainia msaidizi, yatatoa ufahamu fulani juu ya kuthamini kwake kweli na uhitaji wa kuhubiri Neno la Mungu sasa. Yeye alisema hivi: “Ninampenda Yehova sana hata kwamba inakuwa lazima nishiriki katika utumishi na kuhudhuria mikutano ili nithibitishe jambo hilo kwake.”—Linganisha Zaburi 122:1.
12. (a) Ni kwa kadiri gani Italia imepokea habari njema za Ufalme tangu mwaka 1945 sana-sana? (b) Tuna habari gani zenye kutia moyo juu ya kazi ya Ufalme katika nchi za Italia, Ureno, na Spania?
12 Katika Italia, ambako Kanisa Katoliki ya Roma limekuwa likiongoza maisha ya kidini ya watu kwa karne nyingi, matukio ya miaka ya karibuni yameitokeza mbele kazi ya Mashahidi wa Yehova zaidi ya wakati mwingine wote uliopita. Kutoka hesabu ndogo sana ya watu 90 katika mwaka 1945, Mashahidi wa Yehova wamekua wakawa tengenezo la kidini la pili kwa ukubwa katika Italia. (Isaya 60:22) Katika mwaka wa utumishi wa 1981 tawi huko liliripoti kilele cha wahubiri watangazaji wa Ufalme 90,553. Sasa zaidi ya wakati mwingine wote, wakati unafaa kwa habari njema za Ufalme kuhubiriwa katika Italia na nchi nyingine za Kilatini za Ulaya. Katika Italia mwaka 1945, kama ilivyotajwa, kulikuwa wahubiri 90 hivi, walakini katika Spania na ureno mwaka huo hakuna maandishi yanayoonyesha kuwapo kwa mashahidi wa Yehova wo wote wakiwa wanatangaza habari njema za Ufalme. Hata hivyo, mwaka 1981 jumla katika nchi hizo tatu imefika wahubiri 159,972. Kama Yesu alivyosema: “Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache.”—Mathayo 9:37.
UVUNAJI KATIKA SEHEMU NYINGINE
13. (a) Maandishi yanaonyesha nini juu ya kuenezwa kwa “habari njema” katika kontinenti ya Afrika? (b) Ni jambo gani lililoonwa linaloonyesha kwamba kwa kweli wakati unafaa wa kuvuna watu zaidi wenye kupenda haki?
13 Katika sehemu nyingi za Afrika, maelfu mengi wameitikia ujumbe wa kweli unaotangazwa huko na mashahidi waaminifu wa Yehova wakati wa hii karne ya 20. Katika sehemu fulani, kama Nigeria, Afrika ya Kusini, Zambia, Zimbabwe na Malawi, mbegu za kweli zilipandwa huko-o-o nyuma miaka ya 1923 mpaka 1927, ambapo katika nchi nyingine, kama Mali, Mauritania, Upper Volta na Rwanda, ujumbe huo haukutokeza wahubiri wa Ufalme mpaka kipindi cha miaka ya kati ya 1962 na 1970. Hakika wakati unafaa kufanya lo lote liwezekanalo kuwasaidia wenye kiu wapate maji ya kweli kabla Yehova hajasema kazi imekamilika. Katika Zambia painia wa pekee mmoja alimtembelea mkuu wa kijiji (chifu) aliyeonyesha kupendezwa sana na ujumbe wa Ufalme. Mkuu wa kijiji huyo alikuja na wengine kwenye mazungumzo hayo hata kwamba, kwa jumla, watu 18 walisikiliza ujumbe wa huyo painia wa pekee, jambo ambalo lilisababisha hesabu kadha ya mafunzo za Biblia yaanzishwe. Baada ya muda mfupi kundi la mahali hapo likawa na ongezeko la wahubiri toka 65 mpaka 86. Leo kuna sehemu chache sana katika kontinenti ya Afrika ambako hakuna Mashahidi wa Yehova wanaohubiri “habari njema.”
14. Ni jambo gani lililoonwa lenye kupendeza zaidi linaloripotiwa kuwa lilitokea katika visiwa vya Milango-Bahari ya Torres?
14 Ripoti kutoka sehemu nyingine za ulimwengu wakati wa mwaka uliopita zimekuwa zenye baraka na zenye maendeleo. Kando ya ncha ya kaskazini kabisa ya Australia kuna visiwa vya Milango-Bahari ya Torres. Kuna visiwa 100 katika kikundi hicho, 20 kati yavyo vikiwa vinakaliwa na watu. Kisiwa kimoja kati ya hivyo, Kisiwa cha Thursday, kina kundi lenye kusitawi la Mashahidi wa Yehova. Mwangalizi wa mzunguko mmoja na ndugu wawili wa Kisiwa cha Thursday walizuru kisiwa kimoja kinachoitwa Sue, ambako walikaribishwa kwa uchangamfu. Mwenyekiti wa Kisiwa hicho, kama anavyoitwa, alikuwa amewaalika ndugu hao waje kwa kuwa yeye anapendezwa na kweli ya Biblia na kazi ya Mashahidi wa Yehova. Ndugu hao walishangaa kama nini walipopata kujua kwamba mwenyekiti huyo alikuwa anafuatia sana usafi na unadhifu kati ya watu hao wa kisiwa hicho pamoja na mwenendo wao. Kwa ukawaida yeye hupanga watu hao wapate ushirika fulani wa kiroho. Wakati wa ziara ya ndugu hao, walisikiliza nyimbo zilizoimbwa wakati wa mkusanyiko mmoja, maneno yake yalikuwa yametolewa katika vitabu fulani vya Sosaiti. Waliweza kutolea watu hao hotuba, hesabu yao ikiwa 40, na kuwatia moyo katika funzo lao la Biblia pamoja na kutumia vitabu vya Sosaiti.
USHUHUDA WA ULIMWENGUNI POTE
15. Kwa hiyo, daraka la wahudumu wa Yehova wa Ufalme linaendelea kuwa nini?
15 Mara nyingi sana tumeyataja maneno ya Yesu ya Mathayo 24:14, NW kwamba “habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja”! Ushuhuda wa Ufalme unatolewa kwa njia ya maneno na ya matendo na watumishi waaminifu wa Yehova. Ushuhuda wa kutosha ukiisha kutolewa—na mwenye kufanya uamuzi ni Yehova Mungu—ndipo mwisho utakapokuja. Basi, mgawo wetu wenye kuendelea ni kuzidi kutoa ushuhuda mpaka wakati wa tukio kuu zaidi ambalo ulimwengu utapata kuliona, kuja kwa ufalme wa Yehova ukiwa mikononi mwa Mfalme wake anayetawala, Bwana yetu Yesu Kristo.
16. (a) Ni tarakimu gani zinatolewa kuonyesha kwamba Mashahidi wa Yehova wanatambua kwamba sasa ndio wakati wa kulihubiri Neno? (b) Basi ni ulizo gani la kibinafsi analoulizwa kila mmoja wetu?
16 Katika nchi na visiwa 206 za ulimwengu wakati wa mwaka uliopita saa zaidi ya 358,581,547 zilitumiwa kwenye utumishi na wahubiri wa habari njema za Ufalme 2,361,896 katika kueneza ujumbe huo wenye kusisimua. Waliongoza mafunzo ya Biblia ya nyumbani 1,475,177 na kugawanya vitabu na vijitabu 31,444,062 na nakala za Mnara wa Mlinzi na Amkeni! 234,163,921 duniani pote. Hayo, pamoja na ushuhuda mwingi ambao umetolewa katika miaka hii mingi ya karne ya 20, yanatoa uthibitisho mwingi wa tamaa ya watu wa Yehova kutimiza mgawo wao wa ‘kutangaza habari njema kwa wapole, kufunga mioyo iliyovunjika, kutangaza uhuru kwa wale waliotekwa, kutangaza mwaka wa nia njema upande wa Yehova na siku ya kisasi upande wa Mungu wetu, kufariji wote wanaougua.’ (Isaya 61:1, 2, NW) Je! SASA unashiriki katika kuhubiri Neno la Mungu na ufalme wake ulioahidiwa?
17. Halafu tunachunguza ushuhuda gani zaidi wa baraka ya Yehova?
17 Wakati wa mwaka wa utumishi wa 1981, watu 119,836 walijiunga na wale ambao wameweka wakf maisha zao kwa Yehova na ambao wameonyesha hivyo kwa ubatizo wa maji. Tunawakaribisha wote hawa kwenye udugu wa Kikristo. Unapochunguza orodha iliyomo katika gazeti hili, inayoonyesha utendaji wa kuuhubiri Ufalme wa Mashahidi wa Yehova katika mwaka wa utumishi wa 1981, utaona kwamba katika nchi za Mashariki na nchi za Magharibi maelfu mengi wamepata maji ya uzima na ya kweli yanayotolewa katika Neno la Mungu, nao wamejiunga kutangaza habari njema za Ufalme huo.
18. Kwa kuwa kila siku wakati uliobaki unapunguka, hiyo inamaanisha nini kuhusu umaana wa kazi yetu ya kuhubiri, na kwa hiyo tunapaswa kuazimia nini?
18 Kila siku, wakati unaobaki wa hii taratibu mbovu ya mambo unapunguzwa, hiyo ikimaanisha kwamba nafasi zetu za kuhubiri “habari njema” zinakuwa zenye umaana mwingi zaidi na zaidi. Kila siku na itupate tukijitahidi sana kujionyesha wenyewe kuwa wafuasi waaminifu wa Yesu, tukijaribu kuiga mwendo wake wa maisha akiwa msitawishaji wa ibada safi. Kama ilivyokuwa kwa Daudi mwaminifu, bidii kwa ajili ya nyumba ya Yehova, ibada yake safi na yenye kutakata, hayo na yatufanye tusimame imara katika ukamilifu wetu na kuendelea kuwa watangazaji wa Ufalme mpaka Yehova aseme kazi hiyo imekamilishwa.—Zaburi 69:9, NW—Kutoka The Watchtower, January 1, 1982.
[Sanduku/Picture katika ukurasa wa 10]
Ukuzi wa wahubiri wa lile Neno katika AMERIKA YA KATI na YA KUSINI—
1945 . . . wahubiri 4,720
1981 . . . wahubiri 373,919
[Sanduku/Picture katika ukurasa wa 17]
Ongezeko la watangazaji wa Ufalme katika SPANIA, URENO na ITALIA—
1945 . . . wahubiri 90
1981 . . . wahubiri 159,972
[Sanduku/Picture katika ukurasa wa 17]
Ongezeko la Mashahidi katika AFRIKA—
1945 . . . wahubiri 19,083
1981 . . . wahubiri 300,989
[Chati katika ukurasa wa 12-15]
1981 RIPOTI YA MWAKA WA UTUMISHI WAWA MASHAHIDI WA YEHOVA ULIMWENGUNI POTE
(Ona nakala iliyochapwa)