Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w84 3/1 uku. 23
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Habari Zinazolingana
  • Musa na Haruni Wanamwona Farao
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Mapigo Matatu ya Kwanza
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Yehova Ni Nani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Mapigo Sita Yaliyofuata
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
w84 3/1 uku. 23

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

◼ kwa sababu gani Mungu alimwagiza Musa amwombe Farao ruhusa ya ‘kufunga safari siku tatu jangwani,’ hali yeye alikuwa amekusudia Waisraeli waondoke Misri kabisa?

Kwenye kichaka chenye moto, Mungu alisema kwamba angemtumia Musa kukomboa Waisraeli Misri na kuwaongoza kwenye nchi inayomiminika kwa maziwa na asali. Mungu alimwambia kwamba Farao alipaswa kujulishwa hivi: “[Yehova], Mungu wa Waebrania, amekutana nasi; basi sasa twakuomba, tupe ruhusa twende mwendo wa siku tatu jangwani, ili tumtolee dhabihu [Yehova], Mungu wetu.”​—Kutoka 3:18.

Kwa kuwa Mungu alikuwa amekwisha kumwambia Musa muda mfupi tu uliopita kwamba Waisraeli wangekwenda kwenye Nchi ya Ahadi, huenda ikaonekana ni kama hakuwa akimpasha Farao habari zote za uhakika. Lakini kutokana na namna mambo yalivyokwenda, inaonekana wazi kwamba njia ya Mungu ya kushughulikia mambo ilikuwa ya haki na ilitimiza kusudi lake.

Waisraeli walikuwa wamekuwa katika Misri miaka zaidi ya 200 na walikuwa wakitendwa kama taifa la watumwa. Lakini Mungu, kulingana na ahadi yake isiyoweza kubadilishwa aliyompa Abrahamu, angefanya Israeli wawe taifa kuu. Wangekaa kwa uhuru katika nchi ambayo Mungu alikuwa amemwonyesha Abrahamu, nchi ya Kanaani. (Mwanzo 12:1,2, 7; 18:18; 22:17, 18) Je! Farao angekuwa na moyo wa kupenda kuonyesha ushirikiano kwa kusudi la Mungu?

Hapana, Yehova alitangulia kujua kwamba Farao angekataa kwa kichwa kigumu kuruhusu Waisraeli waondoke Misri, hata kwa muda mfupi. Kama Mungu, kupitia Musa na Haruni, angalionyesha kwamba mapenzi Yake yalikuwa kwamba Israeli waondoke kabisa, Farao angaliweza kutokeza makatazo ambayo yangalielekea kuwa ya kweli, kama vile uwezekano wa nchi kuwa na mfarakano watu zaidi ya milioni moja wakiondoka safari moja kabisa. Na wengine wangaliweza kuwa na maelekeo ya kukubaliana na nia ya Farao au kumwunga mkono kwa kumsikitikia. Lakini kuondoka kwa Israeli katika eneo la Gosheni muda wa siku chache tu kusingeonekana kuwa hasara kubwa kwa Wamisri.

Wakati Farao alipokataa kwa kichwa kigumu kuwaruhusu Waisraeli waende, hata kwa siku tatu, ilionekana wazi kabisa isiweze kukanwa kwamba moyo wake ulikuwa mgumu. Hakukuwa na udhuru (kisababu) wo wote wa kuwa na nia hiyo ya ugumu, wala wa lile ongezo la uonezi ambalo Farao aliagiza lifanywe baada ya kuombwa ruhusa ya kuondoka.​—Kutoka 5:1-9.

Hata baada ya kufululiziwa mapigo, Farao mwenye moyo mgumu hakuruhusu Israeli waondoke Misri. Mwishowe, pigo la kumi lilileta maafa makubwa sana Misri mpaka Farao akamwambia Musa awatwae hao watu na kwenda zao​—bila kufanya mapatano ya kwamba warudi baada ya siku tatu. Hata hivyo, Israeli walipokuwa wakiendelea kutoka katika nchi hiyo, Farao alijaribu kuwanasa Israeli na kuwateka tena. Lakini wapi. Hata Farao mwenyewe alikufa katika Bahari Nyekundu (ya Shamu).​—Kutoka 12:31-39; 14:5-9, 21-28; Zaburi 136:15.

Kwa hiyo, kuambiwa kwa Musa na Mungu apeleke ombi hilo lenye kiasi la kutaka ruhusa ya siku tatu kulikuwa kama jaribu kwa Farao. Kulifunua yaliyokuwa ndani ya moyo wake.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki