Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 10/1 uku. 19
  • ‘Wanapamba Mafundisho ya Mungu Wetu’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Wanapamba Mafundisho ya Mungu Wetu’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Habari Zinazolingana
  • Kutoka Mshuko wa Moyo Hadi Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Mwishowe Mbegu Ilichipuka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • “Mtakuwa Watakatifu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • “Kutoka Kinywani mwa Watoto Wachanga”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 10/1 uku. 19

Ripoti ya Watangazaji wa Ufalme

‘Wanapamba Mafundisho ya Mungu Wetu’

URAHISI na uwazi wa ukweli wa Ufalme unaweza ‘kupambwa’ na wale wanaoutangaza kwa wengine. Jinsi gani? Kwa mwenendo wao mwema. Angalia jinsi mtume Paulo alivyoonyesha hilo. Watumwa Wakristo walishauriwa “wauonyeshe uaminifu mwema wote, ili wayapambe mafundisho ya Mwokozi wetu Mungu katika mambo yote.” (Tito 2:10) Mambo yaliyoonwa yafuatayo katika Argentina yanaonyesha uhalisi wa shauri hilo.

◻ Mashahidi wa Yehova sita walikuwa wameajiriwa katika duka la bidhaa nyingi ambamo wanunuzi wanajitumikia. Mwenye duka hilo alikuwa anaonwa kuwa mwenye kuchunga kazi yake kwa ukali mwingi. Walipoomba wapewe wakati wa kuhudhuria Ukumbusho wa kifo cha Kristo, waliambiwa, “Amueni kama mnataka kazi yenu au mikutano yenu.” Ingawa kazi ilikuwa haba, waliamua kuhudhuria Ukumbusho. Siku iliyofuata, walienda kazini wakifikiri watafukuzwa kazi. Walistaajabu kama nini kazi yao ilipoendelea na pia wanne wao waliokuwa wafanya kazi wa kibarua wakapewa kazi za kudumu. Na wote sita wakaongezwa mshahara! Baadaye, wawili kati yao waliamua kuwa mapainia wa kawaida, kwa hiyo mwenye duka hilo la bidhaa nyingi akawafanyia mpango unaowafaa wa kufanya kazi kwa zamu. Sababu yake ya kuwatendea fadhili ilikuwa nini? Hakutaka wafanya kazi wake wanyofu, wenye bidii, waondoke.

Kwa hiyo unyofu na tabia nzuri za kazi za Mashahidi hao sita ‘zilipamba’ mafundisho yao ikawa kwa heshima ya Yehova.

◻ Dada mmoja alikuwa akifanya kazi katika duka la dawa, lakini kwa sababu ya saa nyingi za kazi, hakuwa akihudhuria mikutano yote ya Kikristo, wala hangeweza kuwa painia kama alivyotamani. Mwenye duka hilo la dawa alikataa kumpangia ratiba ya kazi aliyotaka, kwa hiyo dada huyo akaacha kazi yake. Halafu akafanya kazi akiwa yaya, na kufanya hivyo kukamruhusu afanye upainia msaidizi. Miezi michache baadaye, mwenye duka hilo la dawa alikuja nyumbani mwake akampa toleo la kazi “pamoja na ratiba yo yote ya kazi aliyotaka dada huyo.” Kwa sababu gani? “Kwa sababu ya mwenendo wake bora sana,” yasema ripoti hiyo.

◻ Mwenendo mwema wa Shahidi mmoja wa kike ‘ulipamba’ mafundisho yake kwa njia tofauti. Ripoti hiyo inayotoka Argentina inaeleza kwamba wakati Mashahidi wawili walipokaribia nyumba maridadi yenye starehe kukiwa na motokaa kubwa ya kisasa nje, waliogopa kidogo kwa sababu ilionekana wazi huo ulikuwa wonyesho wa utajiri. Walishangaa kama nini kukaribishwa kwa mikono miwili. Mazungumzo ya saa mbili yakafuata, wakijibu maulizo. Mashahidi hao walisema: “Tulikubali kurudi juma linalofuata. Tuliondoka tukiwa tumefurahi sana lakini tumeshangaa kidogo kwa sababu hatukujua sababu yenyewe ya kukaribishwa hivyo. Juma lililofuata tukajua sababu ni nini.”

Mamsahib huyo akaeleza: “Nilikuwa nikiishi katika Mar del Plata nami nilimjua mwanamke kijana aliyekuwa akiishi maisha ya ukosefu mwingi wa adabu. Muda si muda akaanza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova, na upesi badiliko likaonekana wazi katika utu wake. Majirani nami tulistaajabu sana kwa ajili ya kubadilika kwake kwa sababu halikuonekana hata doa moja la utu wake wa kwanza wa ukosefu mwingi wa adabu. Sasa yeye ni mwanamke mwenye kuheshimika, mke wa mzee, kama mnavyowaita, na sasa ana jamaa ambayo ni mfano kwa wote.”

Mwenendo uliobadilika wa kijana huyo alipokuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova sasa ulimsukuma mamsahib huyo afikirie kwa uzito mafundisho ya Mashahidi wa Yehova. Funzo la Biblia lilipangwa papo kwa hapo na wenzi hao wa ndoa, nao wakaanza kuhudhuria mikutano kwenye Jumba la Ufalme. Mashahidi hao walimalizia jambo hilo lililoonwa kwa kusema: “Jambo hilo linaonyesha kwamba mwenendo wetu unaweza pia kutoa ushuhuda, iwe kwa utukufu na heshima ya jina la Yehova.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki