Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 11/15 uku. 21
  • Kujua Yaliyo Katika Habari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kujua Yaliyo Katika Habari
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kanisa Likiwa Wakili wa Kupindua Mamlaka
  • Sinema ya Salamu Maria Yakataliwa
  • “Sababu za Kuwa na Hasira”
  • Kwa Nini Kanisa Linapoteza Uvutano?
    Amkeni!—1996
  • Kanisa—Mabadiliko na Mvurugo
    Amkeni!—1993
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 11/15 uku. 21

Kujua Yaliyo Katika Habari

Kanisa Likiwa Wakili wa Kupindua Mamlaka

Makanisa ya Jumuiya ya Wakristo yanajiingiza kwa uwazi zaidi na kwa ugomvi katika masuala ya kisiasa yenye kubadilika-badilika. Katika makala moja kuu yenye kichwa “Kutoka Kwenye Jukwaa za Makanisa na Kuingia Barabarani,” The Toronto Star la Kanada lilielekeza fikira juu ya “hesabu inayoongezeka ya visa vya viongozi wa kanisa kujiingiza [katika mambo ya kisiasa].” Mwandikaji Jack Cahill alisema kwamba Kanisa Katoliki la Roma lilikuwa ‘limeshiriki sehemu ya maana sana katika kupinduliwa kwa Ferdinand Marcos katika Ufilipino’ na katika kukomesha utawala wa Jean-Claude Duvalier katika Haiti. Cahill aliongeza hivi: “Katika Afrika ya Kusini, Askofu Mkuu Mwagilikana Desmond Tutu . . . na washiriki wengine walio mapadri wameionya serikali kwamba watatia watu moyo “kupambana na serikali” juu ya lile suala la ubaguzi wa rangi.

Wengine wana maoni ya kwamba kupambana kwa njia hiyo ni utendaji wa Kikristo unaofaa ikiwa unafanywa kwa kutafuta badiliko la tawala au sheria zisizopendwa na wengi. Ingawa ni kweli kwamba Yesu Kristo alituma wafuasi wake waingie barabarani, kusudi halikuwa kusaidia kuleta mabadiliko ya kisiasa. Bali, wao walienda mahali penye watu wengi na penye milango ya watu ili kutangaza Ufalme wa kimbingu kuwa ndiyo njia ya kubariki wanadamu. (Mathayo 10:5-7; 24:14) Wakati Yesu Kristo alipofanyiwa mashtaka juu ya kuhusika na harakati za kisiasa​—akijifanya mwenyewe kuwa mfalme ati​—yeye alionyesha wazi kwamba harakati za namna hiyo hazikupasa kutazamiwa zifanywe naye wala na wafuasi wake. Yeye alimwambia mwenye kuhukumu kwamba “wangu si ufalme wa ulimwengu huu.” Kupatana na hilo, sikuzote wafuasi wa kweli wa Yesu wamechukua msimamo wa kutokuwamo katika mambo ya kisiasa, kwa maana yeye alikuwa amesema hivi juu yao: “Wao si sehemu ya ulimwengu.”​—Yohana 18:36, Jerusalem Bible ya Katoliki; Yohana 17:14, NW.

Sinema ya Salamu Maria Yakataliwa

Ile hatua ya hivi majuzi isiyopata kuonekana tena iliyochukuliwa na Rais wa Brazili Jose Sarney, kupiga marufuku uonyeshaji wa sinema “Hail Mary” (Salamu Maria) yenye kutokeza ugomvi ilitokeza wimbi la mateto ndani na nje ya Kanisa Katoliki. “Mimi sikubali,” akatangaza Askofu Mauro Morelli, “kwamba Kanisa Katoliki linapaswa kuiomba serikali ichukue hatua za kuitetea imani, kama vile lilivyofanywa wakati wa lile Baraza Kuu la Kuhukumu Wazushi wa Dini.” Na naibu wa kiserikali Eduardo Matarazzo Suplicy alilalamika kwamba rais wa Brazili alikuwa “akiacha aongozwe na mikazo ya upande ule usiotaka mabadiliko ya Kanisa.” “Tumerudia muungano wa uanadini na uanasiasa,” akaandika profesa Roberto Romano wa Chuo Kikuu cha Campinas katika gazeti Folha de S. Paulo. “Jambo hilo limetukia bila kuwapo mapatano ya waziwazi kabisa, kama vile ilivyokuwa katika Mkataba wa Kikanisa uliofanywa pamoja na Mussolini na yale Mapatano ya Kifalme yaliyofanywa pamoja na Hitler. Hapana, yote hayo yametukia kwa siri katika afisi za serikali.”

Mbinu hizi za kidini za kutumia mikazo ili kutumia mambo, na maoni ambayo watu wanakuwa nayo kwa kukazwa hivyo, zinaleta akilini yale masimulizi ya mfano juu ya mwanamke aliye mfano wa kahaba wa kidini ‘mwenye ufalme juu ya wafalme wa dunia.’ Masimulizi hayo yanasema watawala hao mwishowe watakuja ‘kumchukia yule kahaba, nao watamfanya kuwa mkiwa na uchi, na kumteketeza kwa moto kabisa.’​—Ufunuo 17:1, 2, 15-18.

“Sababu za Kuwa na Hasira”

Katika kitabu chake Raisons de la colère (Sababu za Kuwa na Hasira), Rene Dumont, Mfaransa aliye mtaalamu mashuhuri wa kilimo, analaumu kile anachokiita “kushindwa kabisa” kwa ustaarabu [wetu] wa kutokeza mazao.” Marudio ya kitabu kimoja yaliyoandikwa katika gazeti la kila siku la Paris Le Monde yanatoa kwa muhtasari mifano fulani iliyotajwa na Dumont: “Ili kuutimiza uhitaji mkubwa sana wa karatasi za kuchapia magazeti, kila mwaka Kanada inakata miti mingi zaidi ya ile ambayo nchi hiyo inaweza kukuza; Urusi imefyeka sehemu mbili kwa tatu za nchi yao inayoweza kulimwa. Na imesemekana kwamba, kwa kutumia kemikali za kuongeza rutuba badala ya zile za asili, hata Ufaransa ‘inaharibu nguvu za kuzaa za udongo wayo, ambazo umepata muda wa karne nyingi kwa kutiwa mbolea na kupandwa majani ya kuliwa na mifugo.”

Dumont anayalaumu mataifa yenye viwanda pia juu ya ‘kuipotosha’ sayari kwa kutumia vitu ovyo-ovyo na kusimamia vibaya ugawaji wavyo, akiongeza hivi: “Sisi tumesimamia uchumi wa ulimwengu vibaya sana hivi kwamba tunastahili kupoteza mamlaka kuu yetu.” Yeye anadai kwamba kielelezo cha usitawi wa nchi za magharibi “kimeharibu uchumi wa nchi zinazositawi” na kimefyonza watu kwa kuwaondoa katika usitawishaji wa kilimo na kuwaingiza katika “majiji yenye sura mbaya” ambayo yamepanuka katika mataifa yale ambayo hayajasitawi sana.

Ikiwa hali kama hizo zinatoa “sababu za kuwa na hasira” kwa wanadamu wanaotangulia kuona hatari iliyopo, je, mambo hayo hayapasi kumtolea sababu zaidi ya kuwa na hasira Yeye aliyeiumba sayari hii? Hivyo Biblia inaeleza kwa unabii wakati unaokuja mbio ambapo harakati zenye uharibifu wa wanadamu zitaleta ‘hasira ya Mungu mwenyewe,’ ikimfanya “kuwaharibu hao waiharibuo [dunia].”​—Ufunuo 11:18.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki