Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 12/1 kur. 22-24
  • Wamisionari wa Gileadi—Wamejitoa kwa Kusudi Moja

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wamisionari wa Gileadi—Wamejitoa kwa Kusudi Moja
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Habari Zinazolingana
  • Wamishonari Wasukuma Mpanuko wa Ulimwenguni Pote
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Wanafunzi Wenye Kuhitimu wa Neno la Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Wamisionari Wapya Wanajitahidi Kufanikiwa Kweli Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Makao Mapya kwa Ajili ya Shule ya Umisionari ya Gileadi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 12/1 kur. 22-24

Wamisionari wa Gileadi​—Wamejitoa kwa Kusudi Moja

“JUMA lililopita ninyi mlikuwa wanafunzi, juma linalokuja ninyi mtakuwa wamisionari!” Maneno hayo yalionyesha vizuri maoni ya wanafunzi 23 wenye kuhitimu darasa la 81 la Shule ya Biblia ya Gileadi ya Mnara wa Mlinzi. Kwao, na pia kwa wale watu wengine 4,262 wenye kuhudhuria, mazoezi ya kuhitimu yaliyofanywa katika Jumba la Mkusanyiko la Mashahidi wa Yehova Mjini Jersey, Septemba, 7, 1986, yatakuwa siku ya kukumbukwa kwa muda mrefu.

Martin Poetzinger alifungua kwa sala na ndipo Carey Barber, mwenyekiti wa hayo mazoezi ya kuhitimu, akatoa utangulizi wa programu kwa kusema kwamba katika muda wa miaka iliyopita maelfu ya hawa waeneza-evanjeli wamemaliza mazoezi yao ya Gileadi wakiwa wamejitoa kwa kusudi moja: kutumwa kwenye miisho ya dunia wakiwa wamisionari wa kweli wanaolihuburi tumaini la Ufalme. Sisi tunafurahi kama nini kwamba wamisionari wapya hao, wakiwa na roho ya lile jina “Gileadi” watakuwa sehemu ya ‘rundo la ushahidi’!

Akiianzisha programu, Milton Henschel alieleza kwamba wahitimu hao, kama mitume wa siku za Yesu, wametayarishwa kwa ajili ya kazi kubwa. Mfanya kazi-mmisionari Paulo alieleza vizuri maoni yake kuelekea kazi hiyo aliposema: “Kwa maana, ingawa mimi niko huru kutoka kwa watu wote, mimi nimejifanya mwenyewe niwe ndimi mtumwa kwa wote, kwamba mimi niweze kupata watu walio wengi zaidi.”​—1 Wakorintho 9:19, NW.

Maneno hayo ya Paulo yanaonyesha nini? Kwamba wamisionari hawa wapya lazima wapendezwe na watu. Inapasa kuwa tamaa yao kusaidia watu wa aina zote kwa ujumbe wa ukweli unaookoa uhai​—hata wale ambao huenda wakawa wanashirikiana kwa ukaribu sana pamoja na tengenezo jingine la kidini.

Msemaji aliyefuata, Theodore Jaracz, alikumbusha wamisionari hawa wapya kwamba, tofauti na watalii wanaoenda mahali-mahali ili kuona mazingira, wao walikuwa wakitumwa wakaingie miji mingi tofauti-tofuati ya ulimwengu ili kuzihubiri habari njema. Yeye aliwatia moyo wakumbuke mfano wa Yesu na wale wanafunzi wa kwanza na pia ule wa wamisionari wa kisasa, ambao wengi wao wanaendelea kutumikia kwa uaminifu katika migawo yao mbalimbali. “Mwe na akili moja tu,” yeye akaeleza. “Msiruhusu ufuatiaji wa mambo ya kimwili upotoshe fikira zenu. Mkiwa na jicho ‘rahisi,’ basi ninyi mna akili moja tu.” (Luka 11:34, NW) “Ninyi mkiwa wamisionari wa Gileadi,” yeye akaongeza, “mmejitoa kwa kusudi moja​—kutafuta-tafuta wenye kustahili na kuzihubiri habari njema.”

Shauri la wakati unaofaa lilitolewa na Max Larson wa Halmashauri ya Kiwanda juu ya hatua zinazopasa kuchukuliwa wakati matatizo yanapotokea katika mgawo wa mtu wa umisionari. “Msikate tamaa na kuacha,” yeye akaeleza. “Tafuteni njia za kutatua matatizo yenu.” Jinsi gani? “Kwa kupata akili ya Mungu juu ya mambo.” (1 Wakorintho 2:11-16, NW) Larson alikazia umaana wa kupelekea Yehova sala kuomba msaada wake kisha akakazia uhitaji kwa wamisionari kukadiri kwa ukawaida waone jinsi uhusiano wao na Mungu ulivyo.

Lon Schilling wa Halmashauri ya Mashamba ya Mnara wa Mlinzi alikazia ubora wa kukuza na kudumisha mwelekeo wa akilini unaofaa. “Akili zenu zitafanya kazi namna gani wakati mtakapokabiliwa na tatizo au hali inayotaka rekebisho fulani lifanywa?” yeye akauliza. “Sisi tukiwa watu wenye uhuru wa hiari, mmoja mmoja tuna daraka la kujibu kwa jinsi mambo yanavyokuwa.” Yeye alisema kwamba Mungu “hatuongozi sisi kwa kutumia mfumo fulani wa kimbingu wa kuongozea.” Hivyo, wamisionari wasitazamie mengi kutoka kwa Mungu kuliko yaliyo ya kiasi kile cha akili. Wale wanaoonyesha nia ya kupewa mwongozo na Yehova Mungu kupitia Neno lake, roho yake, na tengenezo lake wataweza kudumisha mwelekeo wa akilini unaofaa.

“Maoni yako juu ya mambo bora ni mepesi kadiri gani?” Ulizo hilo lilitokezwa na Ulysses Glass, mmoja wa walimu wa Gileadi. Kupitia mfululizo wa mifano, mwalimu huyo ambaye amefundisha kwa muda mrefu alionyesha kwamba “maoni juu ya mambo bora kwa usawaziko, utambuzi, na bila kuyumba-yumba, yatawezesha [wamisionari] sikuzote waendelee kukaza fikira kwenye faida za Ufalme tu.” Akiinua juu stampu moja ya posta ili wote waione, yeye alisema kwamba, ingawa haina ubora mwingi, mafaa ya stampu ya posta ni uwezo wayo wa kushikamana na kitu kimoja mpaka kifike kule kinakoenda. “Jifanye mwenyewe uwe kama hiyo stampu ya posta,” yeye akasema “na ushikamane na kitu kimoja​—agizo ulilopewa la kuhubiri​—mpaka ufike kwa usalama kule unakoenda, upande ule mwingine wa dhiki kubwa.”

Jack Redford, mwalimu wa Shule ya Gileadi ambaye yeye mwenyewe alikuwa mmisionari, alizungumza katika hotuba yake ya mwisho baadhi ya matatizo ambayo wamisionari wapya hao wangekabili. Alikazia kwamba kwa kuwa na tumaini kamili katika Yehova wanaweza kushinda kipingamizi cho chote, kiwe ni kujifunza lugha mpya, kutamani sana kurudi kwao, kuishi pamoja na watu wengine, kujirekebisha wapatane na utamaduni tofauti, au kutatua tofauti-tofauti za utu. Maana ya jambo alilosema ni hii: “Usijaribu kufanya hivyo kwa kutegemea nguvu zako mwenyewe. Andiko la 1 Wakorintho 3:9 (NW) linasema, ‘Sisi ni wafanya kazi wenzi wa Mungu.’” Yeye aliwahakikishia hivi: “Fanyeni sehemu yenu nanyi mnaweza kuwa na uhakika Yehova atafanya sehemu yake.”

“Shule ya Biblia ya Gileadi ya Mnara wa Mlinzi ni zawadi kutoka kwa Mungu!” Kwa maneno hayo Frederick W. Franz, msimamizi wa Sosaiti, alifungua hotuba ya mwisho asubuhi hiyo, Shule ya Gileadi, yeye akasema, “ilikuwa na kusudi la kuandaa watu ambao wangetumikia wakiwa mashahidi, ushuhuda ulio hai kwa uhakika wa kwamba Ufalme wa Mungu kupitia Yesu Kristo unatenda kazi sasa.” Ndipo alipokumbusha darasa hilo la 81 kwamba kujitoa kwao kwa kusudi moja kunaweka juu yao daraka kubwa “kwa sababu ninyi mnaingia katika shamba la ushahidi wakati ulio hatari zaidi katika historia ya wanadamu. Basi Yehova ameweka juu yetu lile daraka la kuzitangaza habari njema za Ufalme huu na kuonyesha wanadamu wote katika pembe za mbali za dunia njia ya Mungu ya kuokokea.”

Furaha na shukrani kwa pendeleo la kuihudhuria Shule ya Gileadi zilionekana wazi wakati wanafunzi wenye kuhitimu walipopokea shahada zao. Kusudi lao la kuwa wamisionari likiisha kuwa limeelezwa wazi, darasa hilo la 81 la Gileadi liliazimia, katika barua waliyoandikia Baraza Linaloongoza na jamaa ya Betheli, kutumikia kwa ushikamanifu faida za Yehova Mungu na ‘kufanya wimbo mtamu kwa jina lake’ kati ya mataifa. (2 Samweli 22:50, NW) Alasiri, baada ya wonyesho wa tamasha za kutoa ushahidi katika migawo ya wakati uliopita, Mjini New York na katika shamba la umisionari, na pia mchezo wa kuigiza wa kisasa wenye kusisimua, programu ya Gileadi ilimaliziwa kwa sala na Lyman Swingle.

Wanafunzi hao wenye kuhitimu 23 wanatazamia kwa makini ile furaha kubwa ya utumishi wa misionari. Kwa sababu gani? Ni kama vile mhitimu mmoja alivyoeleza:

“Yesu alisema, ‘Uza mali zako, uje uwe mfuasi wangu, . . . na utangaze kote kote Ufalme wa Mungu.’[Mathayo 19:21; Luka 9:60, NW] Mradi wa utumishi wa misionari ulitokezwa na tamaa yetu ya kutaka kusaidia watu wengi kiroho, kama tunavyoweza, mahali ko kote tunakohitajiwa na ambako tungeweza kutumiwa kwa kadiri kubwa zaidi.”​—Fredrick Steiner, mgawo wake ni Guatemala.

Je! wewe ungeweza kupanua utumishi wako kwa Mungu na kuufanya uwe wenye mazao zaidi? Ikiwa ndivyo, basi jitahidi, kama vile wanafunzi hao wenye kuhitimu walivyofanya ili waweze kustahili hilo shamba la umisionari. Furaha yao iliyo kubwa zaidi, na yako wewe pia, itapatikana katika kuwa na maisha kamili ya utumishi uliowekwa wakfu Yehova.​—Malaki 3:10.

[Sanduku katika ukurasa wa 22]

“Hotuba ya Ndugu Larson ilikaza katika akili zangu kweli kweli uhitaji wa kuwa na nia ya kufanya marekebisho. Ili nitimize sehemu yangu nikiwa mmisionari, ni lazima niepuke kuwa na ‘muundo wa kimwili wa akili,’ na badala ya hivyo, nitafute akili ya Yehova na ile ya Mwana wake, Yesu.”​—Alain Saint-Jean, mgawao wake ni New Caledonia.

[Sanduku katika ukurasa wa 23]

“Hotuba ya Ndugu Glass ilinisaidia nione umuhimu wa kuwa na maoni juu ya mambo bora. Hatupaswi kupotoshwa na mambo yasiyo na maana. Lazima tusawazike.”​—Humphrey Hermanus, mgawo wake ni Suriname.

[Sanduku katika ukurasa wa 24]

“Nilipokuwa ninamsikiliza Ndugu Redford, nilihisi maoni ya usalama nikijua kwamba matatizo tutayokabili si mapya. Wengine wamefanikiwa kuyashinda, kwa hiyo hata sisi tunaweza kuyashinda tukitegemea nguvu za Yehova wala si zetu wenyewe.”​—Veronica Lipham, mgawo wake ni Papua New Guinea.

[Sanduku katika ukurasa wa 24]

TAKWIMU ZINAZOHUSU DARASA:

Hesabu ya nchi zilizowakilishwa: 7

Hesabu ya nchi walikopewa mgawo: 12

Wastani wa umri: 30.3

Wastani wa miaka katika ukweli: 13.4

Wastani wa miaka katika huduma ya wakati wote: 9.3

[Picha katika ukurasa wa 23]

COSTA, Alan and Betty United States

GANSLMEIER, Anton and Rita Germany

GONZALES, John and Cynthia United States

GRAULICH, Uwe and Katherine Germany

HERMANUS, Humphrey and Ludmila Netherlands Antilles

JOHANSEN, Bård and Ester Norway

KLOOSTERMAN, Otto and Yvonne Netherlands

LARSON, Gary and Annette Canada

LIPHAM, Mark and G. Veronica United States

SAINT-JEAN, Alain France

STEINER, Fredrick and Helen United States

SZYMANSKI, Cynthia United States

WILKE, David United States

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki