Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 10/15 uku. 21
  • Kujua Yaliyo Katika Habari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kujua Yaliyo Katika Habari
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Si za Kizamani
  • Hukumu Nzito Zaidi
  • Kutukuza Mungu
  • Kanisa Anglikana la Australia—Nyumba Iliyogawanyika
    Amkeni!—1993
  • Jifunze na Uwafundishe Wengine Maadili ya Kikristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Roho ya Kujitolea Huleta Baraka
    Huduma ya Ufalme—2006
  • Je! Dini za Ulimwengu Zinatoa Uongozi Unaofaa?
    Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 10/15 uku. 21

Kujua Yaliyo Katika Habari

Si za Kizamani

Kwa muda mrefu watu wengi wameshikilia ile rai ya kwamba kanuni za maisha mema zilizopangwa katika Biblia ni za kizamani na haziwezi kutumiwa kwa matokeo mazuri. Hata hivyo, machunguzi ya hivi majuzi yamesababisha wanamamlaka fulani wa kitiba wafikirie upya thamani ya ushauri wa Biblia juu ya kuwatendea mema watu wale wengine.

Kulingana na American Health, madaktari wawili wanadai kwamba “kutenda wema huenda kukautendea wema moyo wako, mfumo wako wa kujikinga na maambukizo​—na siha yako kwa ujumla.” Katika Michigan kikoa kingine cha wanatiba kiliongoza uchunguzi wa miaka kumi kupambanua ni kwa kadiri gani mahusiano ya kijamii yaliathiri afya. Jambo la kushangaza ni kwamba walipata kuwa kufanya kazi ya kujitolea mtaani kuliongezea ajabu tazamio la mtu la kuishi muda mrefu zaidi na pia siha yake. Uchunguzi huo ulifunua kwamba wanaume ndio walioathiriwa hasa. Wale ambao hawakufanya kazi yoyote ya kujitolea walisemwa kuwa na uelekeo wa mara 2 1/2 wa kufa wakati wa kipindi hicho cha uchunguzi kuliko wanaume waliofanya aina fulani ya kazi ya kujitolea angalau mara moja kwa juma.

Daktari mmoja katika Kalifornia anaripoti kwamba mpango alioufanya ili wagonjwa wawili wasiopendana wafue kila mmoja nguo za mwenzake ulikuwa na tokeo zuri ajabu la kupunguza vipimo vya kileo-damu mwilini mwao na maumivu ya kifua.

Karne kadhaa zilizopita mtume Paulo aliambia Timotheo ‘awaagize walio matajiri wa ulimwengu wa sasa wasijivune, wala wasiutumainie utajiri usio yakini,’ bali, “watende mema, wawe matajiri kwa kutenda mema, wawe tayari kutoa mali zao, washirikiane na wengine kwa moyo.” Baadaye, yeye alikumbusha Wakristo Waebrania wasisahau “kutenda mema na kushirikiana.” Sababu ikiwa nini? “Utukufu na heshima na amani kwa kila mtu atendaye mema.” Wakristo wa kweli wamejua kwamba kutii shauri hilo linalopatana hata na hali za sasa huleta manufaa kimwili na kiroho pia.​—1 Timotheo 6:17, 18; Waebrania 13:16; Warumi 2:10.

Hukumu Nzito Zaidi

Washiriki wa Mkutano Mkuu wa Viongozi wa Kanisa la Kianglikana walijikuta hivi majuzi wakiwa katika muhali mgumu. Wao walikuwa wamenena wazi kwa umoja wakipendelea “fundisho la kimapokeo juu ya usafi na uaminifu katika mahusiano ya kibinafsi.” Hata hivyo, wakati padri wa mtaa Tony Higton alipotokeza pendekezo la kuomba huo mkutano wa viongozi utangaze kwamba viongozi wa kidini wanapaswa kuwa “vielelezo vyema katika pande zote za maadili, kutia ndani maadili yanayohusu ngono, na hilo liwe ni sharti la kuwekwa rasmi au kubaki katika cheo,” pendekezo hilo lilikataliwa. Sababu ilikuwa nini? Ecumenical Press Service inaripoti kwamba washiriki wa huo mkutano wa viongozi waliona pendekezo hilo kuwa “limezidisha ukali kidogo,” ikiongezea kwamba “Michael Baughen, askofu wa Chester, alidokeza kwamba jambo hilo lingetaka maaskofu wote wa kanisa na viongozi wengine wa kidini wajiuzulu hapo kwa hapo.”

Badala ya hivyo, pendekezo la Higton lilirekebishwa kidogo na washiriki wa huo mkutano wa viongozi liwe la kutokeza mwito kwa Wakristo wote, “hasa . . . viongozi wa Kikristo,” wawe vielelezo “katika pande zote za maadili, kutia ndani maadili yanayohusu ngono.” Ile Press Service, ilitaarifu pia kwamba huo mkutano wa viongozi ulibatilisha mwito wa kutaka “nidhamu inayofaa” miongoni mwa viongozi wa kidini katika visa vya ukosefu wa adili katika ngono.

Ingawa huenda hatua hizo za kutia nidhamu zikawa ‘zimezidisha ukali’ kwa wengi wa viongozi wa kidini wa leo, Neno la Mungu linasema wazi: “Ninyi mwondoeni yule mbaya miongoni mwenu.” (1 Wakorintho 5:13) Mungu anaelekeza kwamba kitendo imara kichukuliwe dhidi ya wote wanaozoea lililo baya ili kuhami usafi wa kiadili na wa kiroho wa kundi la Kikristo. Kweli kweli, “nidhamu” inafaa hata zaidi kwa viongozi wa Kikristo, kwa maana mwanafunzi Yakobo aliandika hivi: “Si wengi kati ya ninyi ambao wanapaswa kuwa walimu, ndugu zangu, mkijua kwamba sisi tutapokea hukumu nzito zaidi.”​—Yakobo 3:1, NW.

Kutukuza Mungu

“Ubora wa kiwango ambacho mwanariadha anatimiza unaweza kufunua ubora wa upendo wake kwa Mungu.” Je! dai hilo la Wes Neal, msimamizi wa Taasisi ya Ukamilifu wa Kiuanariadha (IAP), kama lilivyoripotiwa katika Christianity Today ni la kweli? IAP (Institute for Athletic Perfection), ambacho ni chombo kinachotumiwa na waevanjeliko ‘kutakasa michezo ya ushindani,’ kimeendeleza wazo la kwamba wanariadha walio katika uwanja wa michezo wanapaswa kuiga bidii ile ile kali sana ambayo Yesu alionyesha kuelekea ‘kutimiza kusudi la Baba yake.’ Njia hiyo ya kufikiria mambo, inayojulikana kuwa Jitihada ya Bidii Kamili, imekuwa fundisho linalofuatwa na wengi katika “dini ya chumba cha kubadilishia nguo” cha waevanjeliko na imekuwa “neno la kuzingatiwa sana na wanariadha waevanjeliko,” inataarifu Christianity Today. Kwa uhakika, makala hiyo inadondoa kielelezo cha mchezaji mmoja anayecheza mpira wa kulipwa ambaye “alichora-chora misalaba kwa rangi juu ya viatu vyake na vijitambaa vyenye kufungiliwa kwenye viwiko vya mkono ili viwe kikumbusha cha kwamba yeye alikuwa akicheza ili kumtukuza Kristo.” Mwanariadha mwingine alisema kwamba yeye “alikuwa ameahidi kwamba jambo hilo lingekuwa kwa ajili ya heshima na utukufu wa Mungu, tuwe au tusiwe tulishinda.”

Hata hivyo, je! inaweza kusemwa kwamba ushiriki katika mchezo ulio na mashindano au jeuri nyingi sana unatukuza Mungu? Hasha! Kama vile Psychology Today inavyotaarifu: “Hali yenyewe ya mashindano yale inataka kwamba mwanariadha apendezwe na ubinafsi wakati anapojitahidi kushinda.” Hata hivyo Biblia inasema Wakristo wanapaswa ‘wahesabu wenzao kuwa bora’ kuliko wao wenyewe, ‘wasiangalie mambo yao wenyewe tu, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.’ (Wafilipi 2:3, 4) Wakristo wa kweli wanatukuza Mungu kwa kufanya mapenzi yake, si yao wenyewe.​—Linganisha Isaya 58:13, 14.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki