Wapiga Mbiu ya Ufalme Waripoti
‘Vuno Limeiva’ Katika Burma
◻ Bara zuri la Burma lina wapiga mbiu zaidi ya 1,500 wa habari njema. Mikusanyiko yao ya hivi majuzi ilifanywa kwa lugha za Kiburma, Kilushai, na Kihaka Chin, ikiwa na hadhirina ya jumla ya 2,273. Maono yanayofuata yanafunua kupendezwa na ujumbe wa Ufalme kwa watu walio kama kondoo na yanakazia kile ambacho Yohana aliona katika njozi: “Vuno la dunia limeiva kabisa.”—Ufunuo 14:15, NW.
Ilitukia Katika Dinam
◻ Akiwa katika huduma ya nyumba kwa nyumba katika Matupi, painia wa pekee mmoja alikuta mwanafunzi mwenye kupendezwa hususa kujua habari za helo (moto wa mateso). Alipoelezwa kwamba helo ya Biblia ni kaburi la ujumla la aina ya wanadamu, yeye alishangaa sana. Alishindwa kujiwekea mwenyewe mambo hayo akataka kuambia watu wa ukoo wake kule nyumbani katika kijiji cha Dinam. Wakati wa likizo la shule, yeye alirudi kwenye kijiji cha kwao na kueneza ukweli kuhusu helo. Ndugu-shemeji yake alipendezwa sana kujua mengi zaidi, kwa hiyo akaandamana na mwanafunzi huyo kurudi Matupi akaongee yeye mwenyewe na painia yule. Alikaa katika Matupi kwa majuma kadhaa na kujifunza pamoja na painia huyo. Baadaye, wakati wa ziara yake ya pili ya kuwa Matupi, alisisitiza kwamba mapainia wazuru kijiji cha kwao, kwa maana, kama yeye alivyosema, kulikuwa na watu wengi wenye kupendezwa huko. Mapainia wote watatu wakakubali mwaliko huo kwa mteremo. Iliwachukua saa 12 za jasho kufika Dinam.
Kulikuwa na maziko katika Dinam siku waliyofika mapainia, na watu kutoka vijiji vya karibu walikuwako pia kusikia mengi zaidi kuhusu hii helo ya Biblia. Wote walifanya haraka kwenda kuwaona watu hao wenye kuzuru. Likafuata zungumzo la Biblia lililochukua muda wa kuanzia saa 1:00 jioni hadi saa 5:00 usiku. Mtu mmoja mwenye uelewevu katika umati huo alisimamisha zungumzo hilo saa 5:00 usiku, hiyo ikiruhusu mapainia wale kupumzika kidogo kwa ajili ya kesho yake. Asubuhi iliyofuata, walianza zungumzo lile la Biblia karibu saa moja na kuendelea mpaka saa nne usiku, kukiwa na vipumziko vifupi tu vya kupata milo. Mapainia walipoondoka kijiji hicho, watu walio kama kondoo waliwaomba warudi na kutumia wakati mwingi zaidi wakiwa pamoja nao. Lo, ni pendeleo lililoje kusaidia watu wenye kufundishika jinsi hiyo kwa habari njema za Ufalme zilizo na thamani kubwa. Kweli kweli, vuno ‘limeiva’ katika Burma!
Kupata Ukweli Kutokana na Kitabu Kilichotupiliwa Mbali
◻ Mwanamume mmoja katika Burma alikuwa akizuru rafiki yake ambaye huuza vitabu na karatasi-habari za zamani kwa matumizi ya hivi hivi naye akaona kitabu cha zamani kisicho na jalada miongoni mwa zile karatasi za matumizi ya hivi hivi. Alikiokota na kuanza kukisoma. Muda si muda fikira zake zote zikazama humo. Kumbe hicho kilikuwa kitabu Kumsikiliza Mwalimu Mkuu cha Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi. Yeye aliandikia ofisi ya tawi ya Sosaiti ili apate vitabu zaidi. Ofisi ya tawi ikatuma painia mara hiyo akamtembelee. Funzo lilianzwa pamoja naye, na baada ya mafunzo machache tu, yeye alitambua huo kuwa ukweli na akaanza kusafisha maisha yake ya tabia mbaya-mbaya na baadaye akaondolea mbali sanamu zake za dini ya Kihindu. Punde si punde, yeye na binti yake mwenye umri mkubwa zaidi walijiweka wakfu kwa Yehova na kubatizwa. Sasa yeye ni painia wa kawaida.
Kweli kweli, “mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache” katika shamba lenye matunda la Burma—Mathayo 9:37, 38.