Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 8/1 kur. 3-4
  • Wewe Huenda Wapi Kutafuta Ushauri?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wewe Huenda Wapi Kutafuta Ushauri?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Akili Zilizofungika—Kwa Nini?
  • Jinsi ya Kutoa Ushauri
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2025
  • Kwa Nini Tunahitaji Kutafuta Ushauri?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2025
  • Tafuta Mashauri Mazuri
    Amkeni!—2007
  • Ibada Ambayo Mungu Anakubali
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 8/1 kur. 3-4

Wewe Huenda Wapi Kutafuta Ushauri?

JE! MTU yeyote amepata kukupa pesa za bandia? Labda sivyo, lakini ungetendaje kama mtu fulani angekuambia kwamba pesa za bandia zinazungushwa miongoni mwa watu? Je! ungeudhika? Bila shaka hungeudhika! Yaelekea zaidi kuwa ungeshukuru kwamba umetiwa chonjo kisha ujiangalie usitoe kiasi fulani cha pesa ulizopata kwa jasho kwa kubadilishana na zile za bandia.

Walio wengi kati yetu hupokea ushauri au maonyo mara kwa mara. Ni kweli kwamba maonyo fulani yana mafaa kuliko mengine. Lakini hata ikiwa hatuoni thamani ya kibinafsi ya ushauri fulani au shauri, je! hiyo ni sababu ya kuudhika kwa sababu umetolewa?

Ukweli ni kwamba, kila mmoja huhitaji msaada na ushauri mara kwa mara. Hakuna mtu aliye na majibu yote. Kwa sababu ya ukosefu wa uhakika wa kiuchumi na wa kisiasa ambao watuzunguka, kila mmoja ahitaji tumaini thabiti kwa wakati ujao. Mwongozo wenye kutumika vizuri na ulio timamu wahitajiwa hima katika ulimwengu ambamo karibu nusu ya ndoa zifungwazo huishia katika talaka, ambamo mimba za vijana matineja zimeenea sana, na ambamo magonjwa yenye kuambukizwa kingono yamesambaa kweli kweli. Wazazi wahitaji msaada kuamua njia bora zaidi ya kulea watoto wao katika mfumo huu wa mambo ambao unavuruga akili. Vijana matineja wahitaji msaada wajue watafanya nini kuhusu hisia-moyo zinazohitilafiana ndani yao na kuhusu mibano ambayo huenda ikaonekana kuwa yenye kulemea mno. Kila mtu huhitaji msaada atafute kanuni za maadili katika ulimwengu ambamo kutofuata haki, ukosefu wa adili, na jeuri ni mambo yenye kukubaliwa zaidi na zaidi.

Msaada huo waweza kupatwa wapi? Chanzo bora zaidi cha ushauri unaohusu maisha ni Biblia, Neno la Mungu lililovuviwa. Mtunga zaburi wa kale aliandika hivi: “Neno lako ni taa ya miguu yangu, na mwanga wa njia yangu.” (Zaburi 119:105) Wale ambao husoma na kulitumia Neno la Mungu huepuka mengi ya matumbukio yaliyopo leo. Hiyo ni sababu moja ya Mashahidi wa Yehova kutumia mamia ya mamilioni ya saa kila mwaka wakizuru jirani zao na kuzungumza Biblia pamoja nao. Hata hivyo, watu wengi hawasikilizi, na baadhi yao hata huudhika. Kwa nini?

Akili Zilizofungika—Kwa Nini?

Ni kwamba, watu wengi hugusika upesi hisia yao ya kuudhika kuhusu kupokea ushauri, hasa juu ya habari ya dini. Hata si sikuzote ambapo washiriki wa kanisa hutaka kusikiliza shauri ambalo wahubiri wao huwatolea. Kasisi mmoja Mwingereza aliomboleza hivi: “Kila mtu ana mawazo yake mwenyewe na huyaona kuwa mema kama yale ya mhubiri.” Kwa sababu hiyo, haishangazi kwamba watu hawataki kumsikiliza mtu wasiyemjua ajapo kwenye milango yao.

Zaidi ya hilo, ingawa tunaishi katika muda wa kutia-tia mashaka, watu wengi wangali wamefungamana na kanisa lao kwa hisia-moyo zenye shauku nyingi. Kama ilivyosema ensaiklopedia moja, “dini hugusa hisia zilizo za kina kirefu zaidi za watu wasiohesabika.” Huenda watu hao wasione uhitaji wa kunena na mtu wa dini nyingine kuhusu Biblia, hata wakati zungumzo linapohusika na kutafuta utatuzi wa matatizo yao.

Wengine hawataki kuzungumza juu ya Biblia kwa sababu wameona unafiki na ufisadi mwingi katika dini. Wao huudhiwa na jambo la kwamba viongozi fulani wa kidini huachilia ukosefu wa adili, au huchukizwa sana na pupa ambayo waevanjeli wengi wa televisheni huonyesha bila aibu. Labda wao huchukizwa wakati kasisi atumiapo mamlaka yake kuunga mkono upande mmoja dhidi ya mwingine katika mzozo wa kisiasa. Kwa maoni yao, dini huonekana kuwa ikisababisha matatizo mengi zaidi kuliko yale ambayo huyatatua.

Matatizo yenye kulalamikiwa na watu hao ni halisi. “Pesa za bandia” zinazungushwa kwa wingi miongoni mwa watu, yaani kuhusiana na mambo ya kidini. Lakini kwa uhakika, kukataa msaada wenye thamani kubwa kutokana na Biblia kwa sababu hii ni kukosa akili sawasawa na kukataa pesa zilizo halisi eti kwa sababu kuna noti bandia za kutoka benki zinazozungushwa miongoni mwa watu!

Na kama ilivyokwisha kutajwa, sisi sote twahitaji shauri katika ulimwengu huu ambamo ni vigumu kujua machaguo yapasayo kufanywa na ulio na hali za hatari. Je! kuna njia yoyote ya kuelekezwa kwa hekima katika jambo hili la kukubali ushauri? Je! ni jambo lisilohitajiwa kabisa au hata lenye makosa kuongea na mtu wa dini tofauti kuhusu Biblia? Je! yawezekana mtu afungue akili yake kwa kadiri inayotosha kumwezesha akubali shauri jema na bado asidanganywe na ushauri wa bandia? Biblia yasema nini juu ya jambo hili?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki