Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 1/1 kur. 3-4
  • Lile Taifa Lenye Shangwe

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Lile Taifa Lenye Shangwe
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Taifa Lenye Shangwe Kweli Kweli
  • Lile Taifa la Ki-Siku-Hizi Lenye Shangwe
  • Yehova Ni Mfalme Wetu!
    ‘Mwimbieni Yehova kwa Shangwe’
  • Yehova Ni Mfalme Wetu!
    Mwimbieni Yehova
  • Mtumikie Yehova kwa Moyo Wenye Kujaa Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Tumikia Yehova kwa Shangwe ya Moyo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 1/1 kur. 3-4

Lile Taifa Lenye Shangwe

LILE taifa lenye shangwe! Je! elezo hili linalingana na taifa lolote la ainabinadamu leo? Je! taifa lolote linaweza kudai kwa shangwe kwamba limekomesha jeuri, uhalifu, umaskini, uchafuzi, magonjwa yenye kulemaza, ufisadi wa kisiasa, chuki za kidini? Je! taifa lolote linatoa tumaini halisi la kufikia miradi hiyo? Hata kidogo!

Namna gani hali ya duniani pote? Mikhail Gorbachev, rais wa Urusi, alisema hivi Julai 16 iliyopita: “Sisi tunaacha kipindi kimoja katika mahusiano ya kimataifa, na kuingia kingine, kipindi, ambacho mimi nafikiri, ni chenye amani yenye nguvu, ya muda mrefu.” Hata hivyo, gazeti Time la tarehe iyo hiyo liliripoti kwamba United States ingali imeelekeza shabaha Moscow kwa vichwa 120 vya silaha za nyukilia, ambavyo chochote kimoja kati yavyo kingeteketeza kabisa mji huo. Na bila shaka Warusi wako tayari kulipa kisasi. Sasa kukiwa na hesabu fulani ya washiriki wa Umoja wa Mataifa walio na ujuzi wa kufanyiza silaha za nyukilia, hakuna shangwe nyingi katika kufikiria ni nani angeweza kuwa wa kwanza kufurahia kufyatua.

Taifa Lenye Shangwe Kweli Kweli

Wakati mmoja katika historia—kama miaka 3,500 iliyopita—kulikuwako taifa lenye shangwe kweli kweli. Hilo lilikuwa Israeli la kale. Mungu alipokomboa kikundi hicho cha watu kutoka uonevu wa Misri, walijiunga na Musa katika wimbo wa ushindi wa furaha nyingi, na waliendelea kushangilia kwa muda walipotii Mungu aliye Mkombozi wao.—Kutoka 15:1-21; Kumbukumbu 28:1, 2, 15, 47.

Chini ya utawala wa Sulemani “Yuda na Israeli walikuwa wengi kama mchanga wa pwani kwa wingi, wakila, na kunywa, na kufurahi.” Huo ulikuwa wakati wa mshangilio mkubwa, ambao kilele chao kilikuwa kusimamishwa kwa lile ambalo labda ndilo lilipata kuwa jengo tukufu zaidi katika historia yote, lile hekalu la ibada ya Yehova katika Yerusalemu.—1 Wafalme 4:20; 6:11-14.

Lile Taifa la Ki-Siku-Hizi Lenye Shangwe

Israeli la kale lilitangulia kuwa kivuli cha taifa fulani la ki-siku-hizi. Jipi? Je! ni Israeli la kisiasa la Mashariki ya Kati? Ripoti za habari zinaonyesha kwamba taifa hilo lenye kung’ang’ana halina shangwe kamwe. Je! ule unaoitwa eti Umoja wa Mataifa umeleta shangwe ya kweli kwa mataifa yaliyo washirika wake? Sivyo, shangwe ya kweli haipatikani popote miongoni mwa mataifa yenye kufanya siasa. Pupa, ufisadi, na kutofuata haki ni tele, na katika nchi nyingi watu wa kawaida wanang’ang’ana bila furaha ili waendelee kuishi.—Mithali 28:15; 29:2.

Hata hivyo, leo kuna taifa moja la kusifika lenye shangwe nyingi mno. Hilo si la kisiasa, kwa maana Kichwa chalo, Kristo Yesu, alisema hivi juu ya watu walo: “Ninyi si wa ulimwengu.” (Yohana 15:19) Ingawa Umoja wa Mataifa umeshindwa kuleta umoja wa washiriki wao, taifa hili linavuta waambatani walo kutoka “watu wa kila taifa, na kabila, na jamaa, na lugha.” (Ufunuo 7:4, 9) Sasa hesabu yalo ni karibu milioni nne, hivi kwamba jumla ya watu walo ni kubwa kuliko 60 hivi kati ya mataifa yale 159 yaliyo washiriki wa UM. Lugha za kienyeji za watu hawa milioni nne ni karibu 200; hata hivyo wote wana umoja katika kusema “lugha [moja] iliyo safi.”—Sefania 3:9.

Je! si ajabu kwamba watu hao wa asili tofauti wanasema lugha moja ya ujumla? Sivyo hasa, kwa maana lugha moja hii yenye kuleta umoja inahusisha ujumbe wa Ufalme wa Mungu unaokuja wa uadilifu. Taifa hili lenye shangwe ‘linatoka miisho ya dunia’ na linajulikana ulimwenguni pote kuwa ‘Mashahidi wa Yehova.’ (Isaya 43:5-7, 10; Zekaria 8:23) Karibu mahali popote unaposafiri katika uso wa dunia hii, utawakuta.

Kwenye Isaya 2:2-4, nabii wa Mungu anaeleza juu ya songamano linalomiminika kutoka mataifa yote, likisema: “Njoni, twende juu mlimani kwa BWANA [Yehova, NW], nyumbani kwa Mungu wa Yakobo, naye atatufundisha njia zake, nasi tutakwenda katika mapito yake.” Kwa bidii, hawa wanaalika wengine wapokee maagizo kutoka kwa Yehova kupitia Neno lake, Biblia, ili wapate kujifunza kufanya mapenzi yake. Taifa moja hili linafuata pito la amani ya kweli, watu walo wakiwa tayari wamefua ‘panga zao kuwa majembe na mikuki kuwa miundu, wasijifunze vita tena kamwe.’ Taifa lenye shangwe kweli kweli!

Wewe pia unaweza kushiriki katika shangwe hii. Unaweza kujifunza juu ya ile siku inayokaribia upesi sana wakati ambapo Mfalme, Kristo Yesu, ataondoa wanadamu na serikali zenye uharibifu na kurudisha Paradiso kwenye dunia. (Danieli 2:44; Mathayo 6:9, 10) Hata sasa, wakiwa taifa lenye umoja kweli kweli, Mashahidi wa Yehova wanapata shangwe kubwa katika kazi yao ya kutayarisha kwa ajili ya kipindi hicho kitukufu cha amani ya kweli, kama vile kurasa zinazofuata zitaonyesha.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki