Kutumikia Yehova Kwa Shangwe
“Mtumikieni BWANA [Yehova, NW] kwa furaha [mshangilio, NW]; njoni mbele zake kwa kuimba.”—ZABURI 100:2.
1, 2. (a) Ubaguzi wa rangi ulionyeshwaje wazi katika Berlin, Ujeremani, lakini ile shughuli ya kupigania “Milki ya Miaka Elfu Moja” ilikuwa na matokeo gani? (b) Ni tofauti gani na mwaka 1936 iliyoonwa katika Stediamu Olympia katika Julai 1990, na shangwe ya kikundi cha kimataifa kilichokusanyika huko imetiwa nanga katika kitu gani?
TAMASHA yenyewe ni katika Stediamu Olympia, Berlin. Miaka 54 mapema kidogo, stediamu hii nzuri ilipata kuwa kitovu cha ubishanio wakati Adolf Hitler mtawala mtumia nguvu wa Nazi alipovunjia heshima mkimbiaji Mwamerika mweusi aliyekuwa ameshinda medali nne za dhahabu. Hilo lilikuwa pigo la kweli kwa dai la Hitler juu ya “ukuu wa jamii ya Kiarya”!a Lakini sasa, katika Julai 26, 1990, watu weusi, weupe, wa manjano—watu wenye umoja kutoka mataifa 64, wakiwa jumla ya 44,532—wamekusanyika hapa kwa ajili ya “Lugha Iliyo Safi” Mkusanyiko wa Wilaya wa Mashahidi wa Yehova. Lo, ni shangwe iliyoje inayotiririka mchana huo wa Alhamisi! Baada ya hotuba juu ya ubatizo, wataka-ubatizo 1,018 wanapaaza sauti, “Ja!” na tena, “Ja!” kwa kuthibitisha wakfu wao kwa Yehova Mungu, ili kufanya mapenzi yake.
2 Inachukua dakika 19 ili Mashahidi wapya hawa wafuatane kutoka ndani ya ile stediamu wakielekea kwenye kiziwa cha ubatizo. Na wakati wa dakika zote hizo, makofi ya mngurumo yanavuma kotekote katika uwanja mkubwa huo. Washindi kwenye Michezo ya Olimpiki walikuwa hawajapata kamwe makofi ya jinsi ile ambayo sasa yanakaribisha mamia hawa, wa kutoka mataifa mengi, wanaoonyesha imani inayoshinda ulimwengu. (1 Yohana 5:3, 4) Shangwe yao imetiwa nanga imara katika uhakika wa kwamba utawala wa Ufalme wa Mungu mikononi mwa Kristo kwa kweli utaleta miaka elfu moja ya mibaraka mitukufu kwa ainabinadamu.—Waebrania 6:17, 18; Ufunuo 20:6; 21:4, 5.
3. Ni ukweli gani unaokaziwa na uhakika wa wakusanyikaji, na jinsi gani?
3 Hakuna chuki za rangi ya ngozi wala za kitaifa hapa, kwa maana wote wanaongea lugha iliyo safi ya Neno la Mungu, hivyo wakikazia ukweli wa maneno ya Petro: “Hakika natambua ya kuwa Mungu hana upendeleo; bali katika kila taifa mtu amchaye na kutenda haki hukubaliwa na yeye.”—Matendo 10:34, 35; Sefania 3:9.
4. Ni chini ya hali zipi walio wengi wa wakusanyikaji wakawa waamini, na sala zao zimejibiwaje?
4 Kifungu kikubwa cha wakusanyikaji hawa katika Berlin wamekuwa waamini muda wa miaka mingi ya uonevu, inayohusisha ile enzi ya Kinazi (1933-45) na ile enzi ya kiujamaa iliyofuata katika Ujeremani Mashariki, ambako hivi karibuni tu marufuku juu ya Mashahidi wa Yehova imeondolewa kisheria katika Machi 14, 1990. Hivyo, wengi wao ‘wamelipokea neno chini ya dhiki nyingi pamoja na shangwe ya roho takatifu.’ (1 Wathesalonike 1:6, NW) Sasa wao wana uhuru mkubwa zaidi wa kutumikia Yehova, na shangwe yao haina mipaka.—Linganisha Isaya 51:11.
Pindi za Shangwe
5. Israeli waliadhimishaje ukombozi wa Yehova kwenye Bahari Nyekundu?
5 Kuachiliwa kwa ndugu zetu katika Ulaya ya Mashariki, na kwa sasa katika sehemu za Afrika na Esia, kunatukumbusha juu ya makombozi yaliyofanywa na Yehova katika nyakati za zamani. Tunakumbuka kitendo hodari cha Yehova kwenye Bahari Nyekundu, na jinsi wimbo wa Israeli wa utoaji-shukrani ulivyofikia upeo kwa maneno haya: “Ee BWANA [Yehova, NW], katika miungu ni nani aliye kama wewe? Ni nani aliye kama wewe, mtukufu katika utakatifu, mwenye kuogopwa katika sifa zako, mfanya maajabu?” (Kutoka 15:11) Leo, je! sisi hatuendelei kushangilia katika mambo mazuri ajabu ambayo Yehova anafanyia watu wake? Hakika ndivyo!
6. Tunaweza kujifunza nini kutokana na kupaaza kwa Israeli sauti ya shangwe katika 537 K.W.K.?
6 Shangwe ilifurika katika 537 K.W.K. Israeli liliporudishwa kwenye nchi yalo baada ya utekwa katika Babuloni. Kama vile Isaya alivyokuwa amesema kwa unabii, sasa taifa la Yehova lingeweza kujulisha rasmi hivi: “Tazama, Mungu ndiye wokovu wangu; nitatumaini wala sitaogopa; maana BWANA (Yah, NW) YEHOVA ni nguvu zangu na wimbo wangu; naye amekuwa wokovu wangu.” Lo, ni furaha nyingi kama nini! Na taifa hilo lingeonyeshaje shangwe hiyo? Isaya anaendelea hivi: “Katika siku hiyo mtasema, Mshukuruni BWANA [Yehova, NW], liitieni jina lake; yatangazeni matendo yake kati ya mataifa, litajeni jina lake kuwa limetukuka. Mwimbieni BWANA [Yehova, NW]; kwa kuwa ametenda makuu.” Sasa wangeweza ‘kupaaza sauti’ kwa shangwe katika ‘kujulisha makuu yake katika dunia yote,’ kama vile watumishi wakombolewa wa Yehova wanavyofanya leo.—Isaya 12:1-6.
Shangwe Katika Kazi ya Yehova
7. Ni makombozi gani yaliyohitaji kuwe na furaha nyingi sana katika 1919?
7 Katika nyakati za ki-siku-hizi watumishi wa Yehova walianza kupaaza sauti kwa shangwe alipowapa ukombozi mzuri ajabu katika 1919. Katika Machi 26 ya mwaka huo, washi-riki wa Baraza Lenye Kuongoza waliachiliwa kutoka gereza la United States walikokuwa wamefungwa kwa miezi tisa chini ya mashtaka ya uwongo juu ya kufitini serikali. Ni mwadhimisho mkubwa kama nini uliotukia katika kuwakaribisha kurudi Betheli ya Brooklyn! Zaidi ya hilo, wote wale wa mabaki wapakwa-mafuta sasa wangeweza kushangilia kuachiliwa kiroho kutoka Babuloni Mkubwa, ule mfumo wa dini ambamo Shetani amenasa ulimwengu mzima.—Ufunuo 17:3-6; 18:2-5.
8. Ni kitolewa gani kisichotazamiwa kilichotangazwa kwenye Mkusanyiko wa Cedar Point katika 1919, na ukatolewa mwito gani wa kutaka kitendo?
8 Matukio ya kihistoria ya 1919 yalifikishwa kwenye kilele na ule mkusanyiko wa watu wa Mungu uliofanywa huko Cedar Point, Ohio, U.S.A., Septemba 1-8. Katika siku ya tano ya kusanyiko hilo, “Siku ya Wafanya Kazi Wenzi,” msimamizi wa Watch Tower Society, J. F. Rutherford, alihutubia 6,000 katika hotuba yenye kuchochea yenye kichwa “Kuutangaza Ufalme.” Baada ya kuzungumzia Ufunuo 15:2 na Isaya 52:7, aliwaambia wasikilizaji wake kwamba gazeti jipya, The Golden Age (ambalo sasa linajulikana kuwa Amkeni!), lingechapishwa kila majuma mawili, hasa kwa ajili ya mgawanyo wa shambani. Kwa kumalizia alisema hivi: “Wale ambao wamejitoa kikamili kwa Bwana; wale ambao hawahofu, wale ambao mioyo yao ni safi, ambao wanapenda Mungu na Bwana Yesu kwa akili, nguvu, nafsi na uhai wao wote, watashangilia, kwa kadiri nafasi inavyoruhusiwa, kushiriki katika kazi hii. Mwombe Bwana mwongozo na mwelekezo wake ili akufanye wewe balozi [mjumbe] wa kweli, mwaminifu na mwenye matokeo mazuri. Halafu, kwa wimbo wa shangwe moyoni mwako, enenda ukamtumikie.”
9, 10. Ni jinsi gani Yehova ameleta matokeo mazuri kwa uchapaji wa magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni!?
9 Huo “wimbo wa shangwe” umesikiwa kotekote duniani! Wengi wa wasomaji wetu wameshiriki, bila shaka, katika kuongeza mwenezo wa gazeti Amkeni! kufikia nakala za sasa za kila toleo katika lugha . Likiwa chombo chenye nguvu katika kuwaongoza kwenye ukweli watu wanaopendezwa, Amkeni! linatumika likiwa mwandamani wa Mnara wa Mlinzi. Katika nchi moja ya Mashariki, dada painia, akifanya kazi ya kawaida ya kupelekea mtu magazeti, alishangaa kupata kwamba kila mara alipopeleka magazeti ya karibuni zaidi, mwenye nyumba alichanga kiasi kinacholingana na dola 7 (za United States) kwenye kazi ya ulimwenguni pote ya Mashahidi wa Yehova—kwa uhakika hiyo ikionyesha uthamini mzuri kwa ajili ya kazi ya Ufalme!
10 Sasa likiwa linaanza mwaka walo wa 112 wa kuchapishwa, gazeti Mnara wa Mlinzi lina mwenezo wa katika lugha , 58 za chapa hizi zikitokea wakati ule ule ulimwenguni pote zikiwa na habari zile zile. Wakiwa wakili mwaminifu, mabaki wapakwa-mafuta wanaendelea kuwapa wasomaji wenye uthamini “posho [ya kiroho] kwa wakati wake.” (Luka 12:42) Katika 1990 United States pekee iliingiza maandikisho mapya na ya upya 476,033 kwa yale magazeti mawili, ongezeko la asilimia 25.5 zaidi ya 1989.
Shangwe Inakuwa Tele
11. (a) Ni mwito gani uliotolewa kwa watu wa Mungu kule Cedar Point katika 1922? (b) Mpaazo wa sauti ya shangwe umepanuliwaje?
11 Shangwe ilipata kuwa tele pia wakati watu wa Mungu, ambao hesabu yao sasa ilikuwa 10,000, walipokusanyika kwa ajili ya mkusanyiko wa pili huko Cedar Point, katika Septemba 1922, kukiwa na wenye kubatizwa 361. Katika hotuba yake “Ufalme wa Mbinguni U Karibu,” yenye msingi wa Mathayo 4:17, Ndugu Rutherford alielekeza kwenye upeo huu wenye kuamsha: “Ni lazima ulimwengu ujue kwamba Yehova ni Mungu na kwamba Yesu Kristo ni Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana. Hii ndiyo siku ya siku zote. Tazameni, Mfalme anatawala! Nyinyi ndio mawakili wake wa utangazaji. Kwa hiyo, tangazeni, tangazeni, tangazeni, Mfalme na ufalme wake.” Wale waliopaaza sauti ya sha-ngwe iliyotoka kwa kishindo kwenye mkusanyiko huo wameongezeka idadi mpaka ikawa kwamba katika 1989 zaidi ya 6,600,000 walikusanyika katika mikusanyiko 1,210 ya Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote, ambako 123,688 walibatizwa.
12. (a) Leo watu wa Mungu wanashiriki katika shangwe gani isiyokadirika? (b) Tunasawazishaje utumishi wetu kwa Yehova na utii kwa “mamlaka za juu zaidi”?
12 Mashahidi wa Yehova wanathamini sana uhuru wao. Juu ya yote, wanashangilia katika utimizo wa ki-siku-hizi wa maneno ya Yesu: “Tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.” Ni shangwe kama nini kuwekwa huru kutoka mafumbo na hofu za kishirikina za dini ya uwongo! Ni shangwe isiyokadirika kama nini kujua Yehova na Mwana wake na kuwa wafanya kazi wenzao, kwa kuwa na tazamio la uhai wa milele! (Yohana 8:32; 17:3; 1 Wakorintho 3:9-11) Watumishi wa Mungu wanathamini pia wakati ambapo “mamlaka za juu zaidi” za ulimwengu huu, ambazo wanaishi chini yazo, zinaheshimu uhuru wao wa kutangaza lile tumaini tukufu la Ufalme wa Yehova ulio chini ya Kristo. Kwa nia wao ‘wanalipa Kaisari yaliyo ya Kaisari,’ wakati uo huo wakilipa ‘Mungu yaliyo ya Mungu.’—Warumi 13:1-7; Luka 20:25.
13. Mashahidi wa Yehova wameonyeshaje shangwe yao kwa kuachiliwa kutoka kwenye uonevu?
13 Hata hivyo, mamlaka za kibinadamu zikijaribu kuzuilia wajibu huu kwa Mungu, Mashahidi wa Yehova wanajibu kama mitume: “Ni lazima sisi tutii Mungu kuwa mtawala kuliko wanadamu.” Katika pindi hiyo, baada ya watawala kuwaachilia mitume, hawa ‘walishika njia wakishangilia.’ Walionyeshaje shangwe hiyo? “Kila siku katika hekalu na kutoka nyumba kwa nyumba waliendelea bila kuacha kufundisha na kujulisha rasmi habari njema juu ya Kristo, Yesu.” (Matendo 5:27-32, 41, 42, NW) Vivyo hivyo, Mashahidi wa Yehova wa ki-siku-hizi wanashangilia wanapopata uhuru mkubwa zaidi ili kufuatia huduma yao. Katika nchi nyingi ambako Yehova amefungua njia, wao wanaonyesha shangwe nyingi sana kwa kutoa ushahidi kamili kwa jina la Yehova na Ufalme unaokuja ukiwa mikononi mwa Kristo Yesu.—Linganisha Matendo 20:20, 21, 24; 23:11; 28:16, 23.
Kuvumilia kwa Shangwe
14. Shangwe hii iliyo tunda la roho inapitaje ile inayoelezwa na kamusi moja?
14 Ni nini hii shangwe nyingi sana ambayo Wakristo wa kweli wanajionea? Ni yenye kina kirefu na yenye kudumu kuliko shangwe ya muda tu ya mshindi kwenye Michezo ya Olimpiki. Ni tunda la roho takatifu ya Mungu, ambalo Mungu anawapa wale ‘wanaotii yeye kuwa mtawala.’ (Matendo 5:32, NW) Kamusi Webster’s inaeleza shangwe kuwa ‘yenye mizizi ya kina kirefu kuliko upendezo mwingi, yenye uangavu au yenye kuonyeshwa wazi kuliko mteremo [furaha].’ Kwa Mkristo, shangwe ina maana ya ndani hata zaidi. Ikiwa imetiwa nanga katika imani yetu, hiyo ni sifa yenye nguvu, yenye kuimarisha. “Furaha [shangwe, NW] ya BWANA [Yehova, NW] ni nguvu zenu.” (Nehemia 8:10) Shangwe ya Yehova, ambayo watu wa Mungu wanasitawisha, inapita kwa mbali ule msisimuko wa juujuu ambao watu wanapata kutokana na raha za kimwili, za kilimwengu.—Wagalatia 5:19-23.
15. (a) Katika maono ya Wakristo waaminifu, uvumilivu umeambatanaje na shangwe? (b) Taja maandiko fulani yanayotoa uhakikisho imara kuhusiana na kudumisha shangwe.
15 Fikiria ndugu zetu katika Ukraine. Wakati ‘mamlaka ya juu zaidi’ ilipoadhibu maelfu yao kwa kuwahamishia Siberia katika miaka ya mapema ya 1950, walipata magumu makubwa. Baadaye, mamlaka ilipowapa msamaha, walishukuru, lakini si wote waliorudia nchi ya kwao. Kwa nini? Kazi zao za jasho katika Mashariki zilikuwa zimewakumbusha Yakobo 1:2-4, HNWW: “Ndugu zangu, mwe na furaha [shangwe, NW] mnapopatwa na majaribu mbalimbali, kwani mwajua kwamba imani yenu ikisha stahimili, itawapatieni uvumilivu.” Walitaka kuendelea kuvumilia katika mavuno hayo yenye shangwe, nayo imekuwa shangwe kama nini kwenye makusanyiko ya hivi majuzi ya Mashahidi wa Ye-hova katika Polandi kukaribisha Mashahidi wa kutoka mpaka huko kule mbali mashariki kwenye jumuiya za pwani ya Pasifiki. Uvumilivu na shangwe vimeambatana kutokeza tunda hili. Kwa kweli, sisi sote tunaovumilia kwa shangwe katika utumishi wa Yehova tunaweza kusema hivi: “Walakini nitamfurahia BWANA [Yehova, NW], nitamshangilia Mungu wa wokovu wangu. YEHOVA, aliye BWANA, ni nguvu zangu.”—Habakuki 3:18, 19; Mathayo 5:11, 12.
16. Mifano mizuri ya Yeremia na Ayubu inapasa kututiaje moyo katika kazi yetu ya shamba?
16 Ingawa hivyo, tunawezaje kudumisha shangwe yetu tunapotoa ushahidi miongoni mwa wapinzani wenye vichwa vigumu? Kumbuka kwamba manabii wa Mungu waliendeleza maoni yenye shangwe katika hali kama hizo. Yeremia alisema hivi akiwa chini ya jaribu: “Maneno yako yalionekana, nami nikayala; na maneno yako yalikuwa ni furaha kwangu, na shangwe ya moyo wangu; maana nimeitwa kwa jina lako, Ee BWANA [Yehova, NW], Mungu wa majeshi.” (Yeremia 15:16) Ni pendeleo kama nini kuitwa kwa jina la Yehova na kutolea jina hilo ushahidi! Kujifunza kibinafsi kwa bidii ya uendelevu na kushiriki kikamili katika mikutano ya Kikristo kunatujenga tuendelee kushangilia katika ukweli. Shangwe yetu itaonekana wazi katika sura yetu na jinsi tunavyojichukua tukiwa shambani na katika tabasamu yetu ya Ufalme. Hata akiwa chini ya jaribu kali, Ayubu angeweza kusema hivi juu ya adui zake: “Nikacheka nao [nikawa nikitabasamu kwao—wakawa wakishangaa kwa kutoamini hilo, NW]; na mwanga wa uso wangu hawakuuangusha.” (Ayubu 29:24) Kama Ayubu mwaminifu, sisi hatuhitaji kuvunjika moyo wakati wapinzani wanapotufanyia mzaha. Endelea kutabasamu! Hali ya uso wetu inaweza kuonyesha shangwe yetu na hivyo ivute masikio yenye kusikiliza.
17. Uvumilivu ukiwa pamoja na shangwe unawezaje kuzaa tunda?
17 Tunapomaliza eneo tena na tena, uvumilivu na shangwe yetu unaweza kuvutia watu wenye mwelekeo wa uadilifu na kuwatia moyo wachunguze tumaini tukufu tulilo nalo. Ni shangwe kama nini kuongoza mafunzo ya Biblia pamoja nao kwa ukawaida! Nao wanapoingiza mioyoni mwao zile kweli za Neno la Mungu zenye thamani kubwa, sisi tunaona shangwe kama nini wakati mwishowe wanapokuwa waandamani wetu katika utumishi wa Yehova! Ndipo tunaweza kusema, kama vile mtume Paulo alivyoambia waamini wapya katika siku yake: “Maana tumaini letu, au furaha yetu, au taji ya kujionea fahari, ni nini? Je! si ninyi, mbele za Bwana wetu Yesu, wakati wa kuja [kuwapo, NW] kwake? Maana ninyi ndinyi utukufu wetu, na furaha yetu.” (1 Wathesalonike 2:19, 20) Kwa kweli, shangwe inayoridhisha inapatikana katika kuongoza wapya kwenye ukweli wa Neno la Mungu na kuwasaidia wawe Mashahidi waliojiweka wakfu na kubatizwa.
Shangwe Inayotegemeza
18. Ni nini kitatusaidia tuelekeane na majaribu mbalimbali ya ki-siku-hizi?
18 Katika maisha zetu za kila siku, hali nyingi zinahitaji uvumilivu. Ugonjwa wa kimwili, mshuko wa moyo, na ugumu wa kiuchumi ni chache tu kati ya hizo. Mkristo anawezaje kudumisha shangwe yake ili kukabili majaribu hayo? Hilo linaweza kufanywa kwa kuendea Neno la Mungu kupata faraja na mwongozo. Kusoma au kusikiliza usomaji wa zaburi kunaweza kuandaa burudisho jingi wakati wa jaribu. Na angalia ushauri wa Da-udi wenye hekima: “Umtwike BWANA [Yehova, NW] mzigo wako naye atakutegemeza, hatamwacha mwenye haki aondoshwe milele.” (Zaburi 55:22) Kwa kweli Yehova ndiye “Msikiaji wa sala.”—Zaburi 65:2, NW.
19. Kama Daudi na Paulo, tunaweza kuwa na uhakika gani?
19 Tengenezo la Yehova, kupitia vichapo vyalo na wazee walo wa kundi, linakuwa tayari daima kutusaidia, sisi wanadamu wanyonge, ili kushindana na matatizo yetu. Daudi anashauri hivi kwa uchangamfu: “Umkabidhi BWANA [Yehova, NW] njia yako, pia umtumaini, naye atafanya.” Angeweza pia kusema hivi: “Nalikuwa kijana nami sasa ni mzee, lakini sijamwona mwenye haki ameachwa, wala mzao wake akiomba chakula.” Kwa kushirikiana na kundi la Kikristo, tutafahamu kwamba “wokovu wa wenye haki una BWANA [Yehova, NW]; yeye ni ngome yao wakati wa taabu.” (Zaburi 37:5, 25, 39) Sikuzote acheni tufuate ushauri wa Paulo: “Kwa hiyo hatulegei; . . . tusiviangalie vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele.”—2 Wakorintho 4:16-18.
20. Tunaona nini kwa jicho la imani, na hiyo inatuchocheaje?
20 Kwa macho yetu ya imani, tunaweza kuona mfumo mpya wa Yehova ukiwa pale mbele tu. Lo, kutakuwako shangwe na mibaraka kama nini! (Zaburi 37:34; 72:1, 7; 145:16) Kwa kujitayarisha kwa ajili ya wakati huo mtukufu, acheni tutii maneno ya Zaburi 100:2: “Mtumikieni BWANA [Yehova, NW] kwa furaha; njoni mbele zake kwa kuimba.”
[Maelezo ya Chini]
a Kwa habari ya “ukuu wa jamii ya Kiarya,” The New York Times la Februari 17, 1940, lilinakili mshikilia-cheo mmoja Mkatoliki wa Chuo Kikuu cha Georgetown kuwa akisema kwamba “alikuwa amemsikia Adolf Hitler akisema kwamba ile Milki Takatifu ya Kiroma, iliyokuwa milki ya Kijeremani, ni lazima ianzishwe upya.” Lakini mwanahistoria William L. Shirer anaeleza tokeo: “Milki ya Tatu iliyozaliwa katika Januari 30, 1933, Hitler alijisifu, ingedumu kwa miaka elfu moja, na katika kawaida ya usemi wa Kinazi ilitajwa mara nyingi kuwa ile ‘Milki ya Miaka Elfu Moja.’ Ilidumu kwa miaka kumi na miwili na miezi minne.”
Kwa Kupitia:
◻ Ni ushinde gani wa ubaguzi wa rangi unaoonekana leo kwa shangwe?
◻ Ni nini kilichofanya watu wa kale wa Mungu waimbe na kupaaza sauti kwa shangwe?
◻ Shangwe ya kweli imeongezekaje katika nyakati za ki-siku-hizi?
◻ Uvumilivu na shangwe zinaambatanaje?
◻ Tunaweza kutegemezaje shangwe yetu?