Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 5/1 kur. 10-14
  • Unganishweni Na Lugha Iliyo Safi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Unganishweni Na Lugha Iliyo Safi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Lugha Yenye Kupewa na Mungu Leo!
  • Lugha Iliyo Safi Inaelezwa Wazi
  • Jifunze Lugha Iliyo Safi Sasa!
  • Lugha Safi Kwa Ajili Ya Mataifa Yote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Semeni Lugha Iliyo Safi Mkaishi Milele!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Je, Unazungumza Ile “Lugha Safi” kwa Ufasaha?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Lugha ya Watu Wote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 5/1 kur. 10-14

Unganishweni Na Lugha Iliyo Safi

“Ndipo nitakapowarudishia mataifa lugha iliyo safi, wapate kuliitia jina la BWANA [Yehova, NW], wamtumikie kwa nia moja.”—SEFANIA 3:9.

1. Je! watu wamepata kumsikia Yehova akisema?

LUGHA ya Yehova Mungu ni safi. Lakini je! watu wamepata kumsikia akisema? Ndiyo! Jambo hilo lilitukia wakati Mwana wake, Yesu Kristo, alipokuwa duniani karne 19 zilizopita. Kwa mfano, Yesu alipobatizwa, Mungu alisikiwa akisema: “Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye.” (Mt. 3:13-17) Hiyo ilikuwa taarifa ya ukweli safi, iliyosikiwa na Yesu na Yohana Mbatizaji kwa lugha ya kibinadamu.

2. Ni nini imeonyeshwa na rejezo la mtume Paulo kwenye “lugha za . . . malaika”?

2 Miaka mingine baadaye mtume Mkristo Paulo alisema juu ya “lugha za wanadamu na za malaika.” (1 Wakorintho 13:1) Hiyo inaonyesha nini? Inaonyesha kwamba si wanadamu tu bali watu wa kiroho pia wana lugha na usemi! Bila shaka, Mungu na malaika hawawasiliani kwa kutumia sauti na lugha ambazo tunaweza kusikia na kuelewa. Kwa nini? Kwa sababu anga kama lile liizungukalo dunia li-nahitajiwa ili kueneza mawimbi ya sauti ya usemi ambayo wanadamu wanaweza kusikia na kuelewa.

3. Lugha ya kibinadamu ilianzaje?

3 Lugha ya kibinadamu ilianzaje? Wengine husema kwamba wazazi wetu wa kwanza walijitahidi kuwasiliana kwa kutumia miguno na mikoromo. Chasema kitabu Evolution (Life Nature Library): “Mtu-nyani wa karibu miaka milioni moja iliyopita . . . yawezekana alijifunza sauti chache za usemi.” Lakini Ludwig Koehler mtungaji wa kamusi mwenye kujulikana sana alisema hivi: “Usemi wa kibinadamu ni siri; ni zawadi ya kimungu, mwujiza.” Ndiyo, ‘usemi wa kibinadamu ni zawadi ya kimungu,’ kwa kuwa Mungu alimpa Adamu, mwanadamu wa kwanza, lugha. Kwa wazi ilikuwa ile ambayo hatimaye ilikuja kuitwa Kiebrania. Lugha hiyo ilisemwa na wazao Waisraeli wa “Abramu Mwebrania,” mzee wa ukoo mwaminifu ambaye mzazi wake wa jadi Shemu alikuwa mwana wa Noa yule mjenga-safina. (Mwanzo 11:10-26; 14:13; 17:3-6) Kwa sababu ya baraka ya Mungu ya kiunabii juu ya Shemu, inapatana na akili kukata maneno kwamba lugha yake haikuathiriwa na jambo ambalo Yehova alifanya kimwujiza karne 43 zilizopita.—Mwanzo 9:26.

4. Nimrodi alikuwa nani, naye alitumiwaje na Shetani Ibilisi?

4 Wakati ule “nchi yote ilikuwa na lugha moja na usemi mmoja.” (Mwanzo 11:1) Mwanamume Nimrodi alikuwa akiishi wakati ule, “mwindaji mwenye nguvu katika kupingana na Yehova.” (Mwanzo 10:8, 9, NW) Nimrodi alitumiwa hasa na Shetani, adui mkuu asiyeonekana wa ainabinadamu, aanzishe sehemu ya kidunia ya tengenezo la Ibilisi. Nimrodi alitaka kujifanyia jina, nao mtazamo huo wa kiburi ukaenea kwa wafuasi wake, ambao walianza mradi wa pekee wa ujenzi katika bara la Shinari. Kulingana na Mwanzo sura ya 11, mstari wa 4, walisema: “Haya, na tujijengee mji, na mnara, na kilele chake kifike mbinguni, tujifanyie jina; ili tusipate kutawanyika usoni pa nchi yote.” Mradi huo, uliopinga amri ya Mungu ya ‘kuijaza nchi’ ulifikia mwisho wakati Mungu alipovuruga lugha ya waasi. “Basi,” usimulizi wa Biblia wasema, “BWANA [Yehova, NW] akawatawanya kutoka huko waende usoni pa nchi yote; wakaacha kuujenga ule mji.” (Mwanzo 9:1; 11:2-9) Mji huo uliitwa Babeli, au Babuloni (kumaanisha “Mvurugo”), “kwa sababu huko Yehova alichanganya usemi wa dunia yote.”—Byington.

5. (a) Ni jambo gani lililozuiwa wakati Mungu alipovuruga lugha ya ainabinadamu? (b) Tunaweza kukata shauri gani juu ya lugha ya Noa na Shemu?

5 Mwujiza huo—mvurugo wa lugha ile moja ya wanadamu—uliongoza kwenye kuijaza dunia kama vile Mungu alivyokuwa amemwamuru Noa, na ulizuia mpango wowote ambao huenda Shetani angekuwa nao wa kuanzisha ibada iliyounganika isiyo safi ya kuabudiwa na wanadamu ambao walikuwa wameasi dhidi ya Bwana Mwenye Enzi Kuu wa mbingu na dunia. Kweli, kwa kuzoea dini bandia ya aina yoyote, watu hao walikuwa watekwa wa Ibilisi, na walikuwa wanatumikia roho waovu wakati walipofanya miungu ya kiume na ya kike, kuipa majina katika lugha zao mbalimbali na kuiabudu. (1 Wakorintho 10:20) Lakini tendo lililochukuliwa na yule Mungu wa pekee wa kweli huko Babeli lilizuia kuanzishwa kwa dini moja ya uongo iliyounganika ambayo ingempa Ibilisi ibada ambayo yaonekana alitamani sana. Bila shaka, Noa mwadilifu na mwana wake Shemu hawakuhusika kamwe katika kitukio hicho katika bara la Shinari. Kwa sababu hiyo, kupatana na akili inaweza kukatwa shauri kwamba lugha yao ilibaki ikiwa ile iliyosemwa na Abramu (au Abrahamu) mwaminifu—ile lugha ambayo Mungu aliongea na mwanadamu Adamu katika bustani ya Edeni.

6. Katika siku ya Pentekoste ya 33 W.K., Yehova alionyeshaje kwamba angeweza kutoa uwezo wa kuongea katika lugha mbalimbali?

6 Yehova, aliyevuruga lugha ya kwanza ya ainabinadamu, aweza kutoa uwezo wa kusema katika lugha mbalimbali pia. Kwani, alifanya jambo ilo hilo katika siku ya Pentekoste katika mwaka 33 Wakati wa Kawaida wetu! Kulingana na Matendo 2:1-11, wafuasi wa Yesu Kristo wapatao 120 walikuwa wamekusanyika katika chumba cha ghorofa katika Yerusalemu wakati huo. (Matendo 1:13, 15) Ghafula, kulikuwa na uvumi toka mbinguni “kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi.” ‘Ndimi kama za moto’ zikaonekana na zikagawanyika huku na huku. Ndipo, wanafunzi ‘wakajazwa roho takatifu na kuanza kunena kwa lugha nyingine, kama roho ilivyowajalia kutamka.’ Kwa lugha hizo walizopewa kimungu, walisema juu ya “matendo makuu ya Mungu.” Na huo ulikuwa mwujiza kama nini wakati Wayahudi na waongofu wa lugha tofauti-tofauti kutoka mahali palipotapakaa sana kama vile Mesopotamia, Misri, Libya, na Roma, walipoelewa ule ujumbe wenye kutoa uhai!

Lugha Yenye Kupewa na Mungu Leo!

7. Ni matumaini gani yangeweza kuwako ikiwa lugha moja tu ilikuwa ikisemwa na kueleweka ulimwenguni pote?

7 Kwa kuwa Mungu aweza kuwapa watu lugha tofauti-tofauti kimwujiza, je! halingekuwa jambo zuri ajabu kama angefanya iwezekane lugha moja tu isemwe na ieleweke ulimwenguni pote? Hiyo ingeendeleza ufahamiano mkubwa zaidi katika familia ya kibinadamu. Kama The World Book Encyclopedia kinavyolisema jambo hilo: “Kama vikundi vyote vya watu vingesema lugha ile ile moja, vifungo vya kitamaduni na kiuchumi vingekuwa karibu zaidi, na nia njema ingeongezeka kati ya nchi.” Basi, kumekuwa na lugha za ulimwengu wote angalau 600 zilizopendekezwa muda wa miaka iliyopita. Kati ya hizo, Esperanto imekuwa ndiyo yenye kufanikiwa zaidi kwa sababu watu wapatao 10,000,000 wamejifunza hiyo tangu ilipoundwa katika mwaka 1887. Hata hivyo, jitihada za kibinadamu za kuunganisha ainabinadamu kwa njia ya lugha ya ulimwenguni pote hazijapata kamwe kufanikiwa. Kwa hakika, matatizo mengi na mengi zaidi yanasababisha mgawanyiko katika ulimwengu huu kadiri ‘watu wabaya wazidivyo kuwa waovu.’—2 Timotheo 3:13.

8. Hata ikiwa lugha ya ulimwengu wote ingechaguliwa katika ulimwengu wa leo, ni jambo gani lingekuwako bado, na kwa nini?

8 Kusema kidini, kuna mvurugo mkubwa. Lakini, je, tusitarajie hivyo, kwa kuwa kitabu cha Biblia cha Ufunuo huita milki ya ulimwengu ya dini bandia “Babuloni Mkubwa”? (Ufunuo 18:2, NW) Ndiyo, kwa maana “Babuloni” humaanisha “Mvurugo.” Hata kama lugha ya kubuniwa au lugha fulani ya kiasili, kama vile Kiingereza, Kifaransa, Kijerumani, au Kirusi ingekubaliwa kuwa lugha ya ulimwengu wote mzima katika ulimwengu wa leo, ukosefu wa muunganiko bado ungekuwako kidini na vinginevyo. Kwa nini? Kwa sababu “dunia [ulimwengu mzima, NW] yote pia hukaa katika yule mwovu,” Shetani Ibilisi. (1 Yohana 5:19) Yeye ndiye mfano hususa wa ubinafsi, naye hutamani sana kwa pupa aabudiwe na ainabinadamu wote, kama vile alivyofanya katika siku za Nimrodi na Mnara wa Babeli. Kwani, lugha ya ulimwengu wote mzima ikisemwa na wanadamu wenye dhambi hata ingempa Shetani fursa ya kuanzisha ibada ya Ibilisi iliyounganika! Lakini Yehova hataruhusu hilo kamwe; kwa kweli, karibuni atamaliza dini zote bandia zenye kuongozwa na Ibilisi.

9. Watu wa mataifa na jamii zote wanaunganishwaje sasa?

9 Hata hivyo, uhakika wenye kushangaza ni kwamba watu wema wa mataifa yote na jamii wanaunganishwa sasa hivi. Jambo hilo linatukia kwa masharti ya Mungu na kwa ajili ya ibada yake. Leo, Mungu anawezesha wanadamu kujifunza na kusema lugha iliyo safi pekee duniani. Na kwa kweli hiyo ni lugha ya ulimwengu wote mzima. Kwa kweli, Yehova Mungu anafundisha watu wengi kutoka kwa mataifa yote ya duniani leo lugha hiyo safi. Hilo ni katika utimizo wa ahadi ya Mungu ya kiunabii kupitia nabii na shahidi wake Sefania: “Maana hapo ndipo nitakapowarudishia mataifa lugha iliyo safi [kihalisi, “mdomo safi”], wapate kuliitia jina la BWANA [Yehova, NW], wamtumikie kwa nia moja.” (Sefania 3:9) Ni nini hiyo “lugha iliyo safi”?

Lugha Iliyo Safi Inaelezwa Wazi

10. Lugha iliyo safi ni nini?

10 Lugha iliyo safi ni ukweli wa Mungu una-opatikana katika Neno lake mwenyewe, yale Maandiko Matakatifu. Hasa ni ukweli kuhusu Ufalme wa Mungu, ambao utaleta amani na baraka nyinginezo kwa ainabinadamu. Lugha safi huondolea mbali makosa ya kidini na ibada bandia. Huunganisha wote ambao huisema katika ile ibada yenye utakato, iliyo safi, iletayo hali njema, ya yule Mungu aishiye na wa kweli, Yehova. Leo, lugha zipatazo 3,000 hutenda kama kizuizi cha uelewevu, na mamia ya dini bandia huvuruga ainabinadamu. Kwa hiyo tunaterema kama nini kwamba Mungu anawapa vikundi vya watu badilisho kwenye hii lugha safi iliyo nzuri ajabu!

11. Lugha iliyo safi imewafanyia nini watu wa mataifa na jamii zote?

11 Ndiyo, watu wa mataifa na jamii zote wanajifunza lugha iliyo safi. Ikiwa ndiyo lugha pekee ya kiroho iliyo safi duniani, inatumika ikiwa kani yenye uweza wa kuunganisha. Inawezesha wote wanaoisema ‘kuliitia jina la Yehova, ili wamtumikie kwa nia moja,’ au kihalisi, “kwa bega moja.” Hivyo wanatumikia Mungu “kwa ukubali mmoja,” “kwa ukubali mmoja wa mapatano ya wote na bega moja lililounganishwa.” (The New English Bible; The Amplified Bible) Tafsiri ya Steven T. Byington husomwa hivi: “Ndipo mimi [Yehova Mungu] nitageuza midomo ya vikundi vyote vya watu kuwa safi, kwamba wote waweze kuita juu ya jina la Yehova na kushirikiana katika utumishi wake.” Ushirikiano kama huo wa ulimwenguni pote wa lugha nyingi katika utumishi wa Mungu umo tu miongoni mwa Mashahidi wa Yehova. Katika nchi 212 leo, hao wapiga mbiu ya Ufalme zaidi ya milioni nne wanahubiri habari njema katika lugha nyingi za kibinadamu. Hata hivyo, Mashahidi ‘husema kwa mwafaka’ na ‘wameunganika kwa kufaa katika akili moja na mstari mmoja wa fikira.’ (1 Wakorintho 1:10, NW) Iko hivyo kwa sababu, hata wawe wapi duniani, Mashahidi wa Yehova wote husema ile lugha moja iliyo safi, kwa sifa na utukufu wa Baba yao wa kimbingu.

Jifunze Lugha Iliyo Safi Sasa!

12, 13. (a) Kwa sababu gani uhangaikie kusema lugha iliyo safi? (b) Kwa nini maneno katika Sefania 3:8, 9 ni yenye maana leo?

12 Kwa sababu gani uhangaikie kusema hiyo lugha iliyo safi? Jambo moja, ni kwa sababu uhai wako wategemea kujifunza na kuisema. Kabla tu ya Mungu kuahidi ‘kuwarudishia mataifa lugha iliyo safi,’ alionya hivi: “Basi ningojeni, asema BWANA [Yehova, NW], hata siku ile nitakapoondoka kuteka mateka; maana nimeazimia kuwakusanya mataifa, ili nizikutanishe falme, nipate kuwamwagia ghadhabu yangu; naam, ukali wote wa hasira yangu; kwa maana dunia yote itateketezwa kwa moto wa wivu wangu.”—Sefania 3:8.

13 Maneno hayo ya Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu yalisemwa kwanza karne 26 zilizopita katika Yuda, ambayo Yerusalemu ulikuwa mji mkuu wayo. Lakini taarifa hiyo ilimaanishwa hasa kwa ajili ya siku zetu kwa sababu Yerusalemu ulikuwa kifani cha Jumuiya ya Wakristo. Na wakati wetu, tangu Ufalme wa Mungu wa kimbingu usimamishwe katika 1914, ni siku ya Yehova ya kuleta pamoja mataifa na kukusanya falme. Ameyaleta yote pamoja chini ya uangalio wake kwa njia ya kazi kubwa ya ushahidi. Hilo nalo, limeyasukuma kupinga kusudi lake. Hata hivyo, kwa rehema Yehova Mungu anawezesha baadhi ya watu wa mataifa yote waungane katika kusema lugha iliyo safi. Wakiwa nayo, wote wanaotafuta uhai katika ulimwengu wake mpya ulioahidiwa waweza kumtumikia kwa sauti moja kabla ya mataifa yote kuliwa na wonyesho wenye moto wa ghadhabu ya kimungu kwenye “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi,” ambayo kwa kawaida huitwa Har–Magedoni. (Ufunuo 16:14, 16; 2 Petro 3:13) Kwa furaha, wale wanaosema lugha iliyo safi na kuita juu ya jina la Yehova kwa imani wakiwa waabudu wa kweli waliounganika wataonea shangwe kinga ya kimungu wakati wa joto la msiba huo wa ulimwengu. Mungu atawaleta wakiwa salama katika ulimwengu mpya, ambamo hatimaye ni lugha iliyo safi pekee itakuwa midomoni mwa ainabinadamu yote.

14. Kupitia Sefania, Mungu alionyeshaje kwamba kuokoka mwisho wa mfumo huu wa mambo kunahitaji tendo la sasa hivi?

14 Kupitia nabii wake Sefania, Yehova huelewesha wazi kwamba wale wanaotumaini kuokoka mwisho wa mfumo mwovu wa mambo uliopo lazima wachukue hatua sasa hivi. Kulingana na Sefania 2:1-3, Mungu asema hivi: “Jikusanyeni, naam, jikusanyeni, Ee taifa lisilo na haya; kabla haijazaa hiyo amri, kabla haijapita siku ile kama makapi, kabla haijawajilia hasira kali ya BWANA [Yehova, NW], kabla haijawajilia siku ya hasira ya BWANA [Yehova, NW]. Mtafuteni BWANA [Yehova, NW] enyi nyote mlio wanyenyekevu wa dunia, ninyi mliozitenda hukumu zake; itafuteni haki, utafuteni unyenyekevu; huenda mtafichwa katika siku ya hasira ya BWANA [Yehova, NW].”

15. (a) Utimizo wa kwanza wa Sefania 2:1-3 ulikuwa gani? (b) Ni nani waliookoka tekelezo la hukumu la Mungu juu ya Yuda, na ni nini itakayokuwa sawa na wokovu huo katika siku yetu?

15 Maneno hayo yalikuwa na utimizo wa kwanza juu ya Yuda na Yerusalemu ya kale. Watu wenye dhambi wa Yuda hawakuitikia ifaavyo kwa kusihi kwa Yehova, kama ionyeshwavyo na utekelezo wa hukumu yake juu yao mikononi mwa Babuloni katika mwaka 607 K.W.K. Kama vile Yuda lilivyokuwa “taifa lisilo na haya” mbele za Mungu, ndivyo Jumuiya ya Wakristo imekuwa “taifa” lisilo na haya mbele za Yehova. Hata hivyo, kwa sababu ya kutii neno la Yehova, baadhi ya Wayudea na wengine waliokoka, miongoni mwao nabii mwaminifu wa Yehova Yeremia. Waokokaji wengine walikuwa Mwethiopia aitwaye Ebed-meleki na wazao wa Yehonadabu. (Yeremia 35:18, 19; 39:11, 12, 16-18) Vivyo hivyo leo, “mkutano mkubwa” wa “kondoo wengine” wa Yesu waliokusanywa kutoka mataifa yote wataokoka Har–Magedoni waingie ndani ya ulimwengu mpya wa Mungu. (Ufunuo 7:9; Yohana 10:14-16) Wale tu ambao hujifunza na kuisema lugha iliyo safi ndio watakuwa waokokaji wenye shangwe.

16. Ni lazima mtu afanye nini ili kufichwa ‘katika siku ya hasira ya Yehova’?

16 Kama vile ilivyokuwa amri ya Yehova kwamba Yuda na Yerusalemu ifutiliwe mbali, ndivyo ilivyo lazima Jumuiya ya Wakristo ipotelee mbali. Kwa kweli, uharibifu wa dini zote bandia uko karibu, na wale wanaotaka kuokoka lazima watende mara moja. Ni lazima wafanye hivyo “kabla haijapita siku ile kama makapi,” ikipeperushwa kasi na upepo, kama wakati nafaka inaporushwa hewani kwenye sakafu ya kupuria. Ili tukombolewe na ghadhabu ya Mungu, lazima sisi tuseme lugha iliyo safi na kuitikia onyo la Mungu kabla siku ya hasira kali ya Yehova haijatujilia. Katika siku ya Sefania na leo, “wanyenyekevu” hutafuta Yehova, pamoja na uadilifu na unyenyekevu. Kutafuta kwetu Yehova kunamaanisha kumpenda kwa moyo wetu wote, nafsi yetu yote, akili zetu zote, na nguvu zetu zote. (Marko 12:29, 30) ‘Huenda wale wanaofanya hivyo wakafichwa katika siku ya hasira ya Yehova.’ Lakini kwa nini unabii wasema “huenda”? Kwa sababu wokovu wategemea uaminifu na uvumilivu. (Mathayo 24:13) Wale wanaojipatanisha na viwango vya uadilifu vya Mungu na huendelea kusema lugha iliyo safi watafichwa katika siku ya hasira ya Yehova.

17. Ni maswali gani yanayobaki ya kufikiriwa nasi?

17 Kwa kuwa siku ya hasira ya Yehova i karibu na wokovu wategemea kujifunza na kutumia lugha iliyo safi, sasa ndio wakati wa kujihusisha sana katika kujifunza na kuisema. Lakini mtu aweza kujifunzaje hiyo lugha iliyo safi? Na unawezaje kunufaika kutokana na kuisema?

Ungejibuje?

◻ Lugha ya kibinadamu ilianzaje?

◻ Lugha iliyo safi ni nini?

◻ Kwa nini maneno katika Sefania 3:8, 9 ni yenye maana leo?

◻ Ni lazima tufanye nini ili tufichwe ‘katika siku ya hasira ya Yehova’?

[Picha katika ukurasa wa 10]

Huko Babeli, Mungu alitawanya ainabinadamu kwa kuvuruga lugha yao

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki