Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 7/1 uku. 31
  • Alipata Kusudi Maishani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Alipata Kusudi Maishani
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Habari Zinazolingana
  • Sababu kwa Nini Watu wa Namna Zote Wanakuwa Mashahidi wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • “Umtazame Mtu Mnyofu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Biblia Inabadili Maisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Kupata Kusudi Katika Maisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 7/1 uku. 31

Wapiga Mbiu ya Ufalme Waripoti

Alipata Kusudi Maishani

YESU asema kwamba awajua kondoo wake. (Yohana 10:14) Ikiwa mtu ana moyo mzuri na apenda amani na uadilifu, huyo atavutwa kwa wafuasi wa Yesu. Mtu wa jinsi hiyo atapata kusudi maishani, kama vile mwanamke mmoja katika Ubelgiji. Masimulizi yake ndiyo haya:

“Mashahidi wa Yehova walipobisha mlangoni pangu, nilikuwa nimeshuka moyo sana na nilikuwa nikifikiria kukomesha maisha yangu. Nilipenda yale ambayo Mashahidi walisema juu ya suluhisho la matatizo ya ulimwengu huu mgonjwa lakini sikupenda wazo la kwamba Mungu alihusika nayo. Nilikuwa nimeacha kwenda kanisani miaka minane kabla ya hapo, kwa kuwa nilichukia unafiki nilioona huko. Lakini, nikiwa na Mashahidi wa Yehova, nilitambua ukweli katika yale waliyosema nikaja kung’amua kwamba, kwa vyovyote, ni vigumu kuishi bila Mungu.

“Kwa kusikitisha, baada ya ziara chache, nilipoteza uwasiliano pamoja na Mashahidi. Nilihuzunika. Nilivuta paketi mbili za sigareti kila siku hata nikageukia dawa za kulevya. Nikitaka kuwasiliana na babu yangu aliyekufa, nilijihusisha katika uwasiliani-roho. Likiwa tokeo la hilo, nilihofu kama nini nilipopatwa na mashambulio ya kishetani nikiwa peke yangu usiku! Hilo lilidumu miezi kadhaa. Kila jioni nilihofu sana wazo la kuwa peke yangu.

“Halafu, siku moja nilienda matembezi, nikipitia njia iliyo tofauti na yangu ya kawaida, nikafikia mahali pa ujenzi mkubwa. Kwa mshangao wangu niliona umati mkubwa hapo. Nilipokaribia, niliona kwamba walikuwa Mashahidi wa Yehova wakijenga Jumba la Ufalme. Nilizikumbuka ziara ambazo Mashahidi walikuwa wamenifanyia nyumbani kwangu, nikafikiri jinsi ambavyo ingalikuwa vizuri ajabu kama ulimwengu mzima ungeweza kuishi kama vile watu hawa walivyoishi.

“Nilitamani kwelikweli kwamba Mashahidi wangerudi nyumbani kwangu, kwa hiyo nilisema na baadhi ya wale waliokuwa wakifanyia kazi jumba hilo. Nilisali kwa Mungu, na siku kumi baadaye yule mwanamume aliyekuwa amenitembelea mara ya kwanza alikuwa mlangoni pangu. Alidokeza kwamba tuendelee na funzo la Biblia, nikakubali kwa furaha. Mara hiyo alinialika mikutanoni kwenye Jumba la Ufalme. Nikakubali. Sikuwa kamwe nimeona jambo kama hilo! Nilikuwa nimetafuta kwa muda mrefu sana watu waliopendana na waliokuwa na furaha. Nao walikuwa hapa hatimaye!

“Baadaye nilihudhuria mikutano yote. Baada ya karibu majuma matatu, niliacha ile tabia mbaya ya kuvuta sigareti. Niliyatupia mbali vitabu vyangu vya unajimu na santuri zangu zenye muziki wa kishetani, na nikaweza kuhisi kwamba mashetani walikuwa wakiniacha. Nilipatanisha maisha yangu kulingana na viwango vya Biblia vya Yehova, na baada ya miezi mitatu nilianza kuhubiri habari njema. Baada ya miezi sita nikabatizwa. Siku mbili baada ya ubatizo wangu, nikaanza kufanya upainia msaidizi.

“Namshukuru Yehova kwa mambo yale yote mazuri ambayo amenifanyia. Maisha yangu yana kusudi hatimaye. Naam, jina la Yehova ni mnara imara ambamo nilipata kimbilio na himaya. (Mithali 18:10) Nahisi kwa kweli kama mtunga zaburi alivyohisi alipoandika Zaburi 84:10: ‘Hakika siku moja katika nyua zako ni bora kuliko siku elfu. Ningependa kuwa bawabu nyumbani mwa Mungu wangu, kuliko kukaa katika hema za uovu.’”

Mwanamke huyo mwenye moyo msikivu alipata kusudi maishani. Ndivyo na yeyote anayejitahidi kumtafuta Yehova kwa moyo mwema.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki