Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 1/1 kur. 10-19
  • Pata Kimbilio Katika Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Pata Kimbilio Katika Yehova
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Korasi Yenye Nguvu ya Wapiga Mbiu ya Ufalme
  • Ngome Tuwezamo Kukaa
  • Kuhubiri kwa Uhakika
  • ‘Hazina ya Wema’
  • 1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • ‘Pata Kimbilio Katika Jina la Yehova’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • “Umtazame Mtu Mnyofu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Kutembea kwa Nafsi Yote katika Njia ya Uzima
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 1/1 kur. 10-19

Pata Kimbilio Katika Yehova

“Katika wewe, Ee Yehova, nimepata kimbilio.”—ZABURI 31:1, NW.

1. Zaburi 31 huonyeshaje uhakika katika uwezo wa Yehova wa kuandaa kimbilio?

SAUTI tamu yaimba juu ya mtu ambaye, ingawa amechoka akilini na mwilini, ajitwisha kwa Yehova. Imani yashinda, ndivyo maneno ya wimbo huo mtakatifu yasema. Katika mikono yenye kungojea ya Mweza Yote, mtu huyo apata ulinzi kutoka wanyanyasi wamwindao. “Katika wewe, Ee Yehova, nimepata kimbilio,” zaburi yake yasema. “Ee nisipate kamwe kuaibika. Katika uadilifu wako niandalie wokovu.”—Zaburi 31:1, NW.

2. (a) Twaweza kumtumaini Yehova kuwa ngome yetu kwa kutegemea nguzo zipi mbili? (b) Yehova ni Mungu wa aina gani?

2 Mtunga-zaburi ana kimbilio moja—lile lililo bora zaidi! Acha mambo mengine yatilike shaka, lakini jambo hili la hakika labaki: Yehova ndiye ngome yake, boma lake. Uhakika wake wategemea nguzo mbili za hakika. Moja, imani yake, ambayo Yehova hataaibisha, na pili, uadilifu wa Yehova, umaanishao kwamba hataacha kamwe mtumishi Wake daima. Yehova si Mungu ambaye huwaaibisha watumishi wake waaminifu; yeye si mvunjaji wa ahadi. Badala ya hivyo, yeye ni Mungu wa kweli na mthawabishaji wa wale wamtumainio sana. Mwishowe, imani itathawabishwa! Wokovu utakuja!—Zaburi 31:5, 6.

3. Mtunga-zaburi amwadhimishaje Yehova?

3 Atungapo muziki wake uwe na sauti mbalimbali zinazoinuka kutoka majonzi na ole mzito hadi kufikia vilele vya uhakika, mtunga-zaburi apata nguvu za ndani. Yeye amwadhimisha Yehova kwa ajili ya upendo wake mwaminifu-mshikamanifu. “BWANA [Yehova, NW] ahimidiwe,” yeye aimba, “kwa maana amenitendea fadhili [fadhili-upendo, NW] za ajabu katika mji wenye boma.”—Zaburi 31:21.

Korasi Yenye Nguvu ya Wapiga Mbiu ya Ufalme

4, 5. (a) Ni korasi gani yenye nguvu inayomsifu Yehova leo, nayo imefanyaje hivyo katika mwaka wa utumishi uliopita? (Ona chati kwenye kurasa 12-15.) (b) Hudhurio la Ukumbusho linaonyesha kwa njia gani kwamba kuna watu wengine mmoja-mmoja walio na nia ya kujiunga na ile korasi ya wapiga mbiu ya Ufalme? (Ona chati.) (c) Ni kikundi kipi katika kutaniko lenu ambacho chaweza kujiunga na ile korasi?

4 Leo, maneno ya zaburi hiyo yamepata umaana hata zaidi. Nyimbo za sifa kwa Yehova haziwezi kukatizwa na mpinzani yeyote mwovu, msiba wowote wa asili, au ole wowote wa kiuchumi; kwa kweli, fadhili-upendo wa Yehova umekuwa wa ajabu kwa watu wake. Kotekote ulimwenguni katika mwaka wa utumishi uliopita, korasi yenye nguvu, yenye kilele cha 4,709,889 katika mabara 231, iliimba ujumbe wa Ufalme wa Mungu. Serikali ya Yehova ya kimbingu kupitia Kristo Yesu ni kimbilio ambalo halitawakatisha tamaa. Mwaka jana, wapiga mbiu ya Ufalme hao kutoka makutaniko 73,070 walitumia jumla ya muda wa saa 1,057,341,972 katika kazi ya kueneza evanjeli. Hilo lilitokeza watu 296,004 waliofananisha wakfu wao kwa Mungu kwa ubatizo wa maji. Na wote waliohudhuria Ufundishaji wa Kimungu Mkusanyiko wa Kimataifa uliofanywa katika Kiev, Ukrainia, Agosti uliopita walishangaa kama nini! Waliona tukio la maana zaidi ikitokea katika historia ya Mashahidi wa Yehova, wakishuhudia ubatizo mkubwa zaidi ya wote ambao umepata kurekodiwa wa Wakristo wa kweli! Kama ilivyotolewa unabii kwenye Isaya 54:2, 3, watu wa Mungu wanaendelea kuongezeka kwa idadi zisizo na kifani.

5 Hata hivyo, raia wengine wa Ufalme wa Mungu walio na nia wanangojea zamu yao kujiunga na korasi hiyo. Mwaka jana, Ukumbusho wa kifo cha Yesu ulihudhuriwa na jumla ya kustaajabisha ya watu 11,865,765. Yatumainiwa kwamba, wengi wa hao watastahili kuimba wimbo wa Ufalme nyumba kwa nyumba katika mwaka huu wa utumishi. Ni lazima iwe taraja hilo lamjaza hasira kama nini yule adui wa kweli, Shetani Ibilisi!—Ufunuo 12:12, 17.

6, 7. Eleza jinsi mtu mmoja mwenye kupendezwa alivyoshinda usumbufu wa roho waovu kwa msaada wa Yehova.

6 Shetani atajaribu kuwazuia wengine wasiongeze sauti zao kwenye korasi hiyo yenye nguvu. Kwa kielelezo, wahubiri katika Thailand hupata watu wanaozidi kuongezeka ambao husumbuliwa na mashetani. Hata hivyo, wengi wenye mioyo myeupe wamewekwa huru kwa msaada wa Yehova. Baada ya kutembelea mchawi kwa sababu ya udadisi, mtu mmoja alikuwa chini ya nguvu za roho waovu kwa muda wa miaka kumi. Alijitahidi kujiweka huru na nguvu zao kwa msaada wa kasisi, lakini hakupata hali bora halisi. Mhudumu wa wakati wote wa Mashahidi wa Yehova alianzisha funzo la Biblia pamoja na mtu huyo akamfundisha kutoka Biblia njia pekee ya kujiweka huru na nguvu za roho waovu—kutwaa ndani ujuzi sahihi juu ya kweli, kutia imani katika Yehova Mungu, na kumwomba katika sala.—1 Wakorintho 2:5; Waefeso 4:6, 7; 1 Timotheo 2:3, 4.

7 Usiku baada ya mazungumzo hayo, mtu huyo aliota ndoto ambamo babake mfu alimtisha ikiwa asingerudi kuwa mwasiliani-roho. Familia yake ilianza kuteseka. Akikataa kukengeushwa, mtu huyo aliendelea na masomo yake ya Biblia akaanza kuhudhuria mikutano. Katika mojayapo mafunzo hayo, painia alieleza kwamba nyakati nyingine vitu vinavyotumiwa katika desturi za uwasiliani-roho vyaweza kuwapa roho waovu njia ya kuwasumbua watu wanaojaribu kujiweka huru na nguvu zao. Mtu huyo alikumbuka kwamba alikuwa na mafuta aliyokuwa ametumia yakiwa hirizi. Sasa aling’amua kwamba alipaswa kuyamwagilia mbali. Tangu wakati alipoyamwagilia mbali, hajapata kusumbuliwa tena na roho waovu. (Linganisha Waefeso 6:13; Yakobo 4:7, 8.) Yeye na mke wake wanaendelea vizuri na funzo lao nao huhudhuria mikutano kwa ukawaida ili kupata maagizo ya Biblia.

8, 9. Ni vizuizi gani vingine ambavyo vimeshindwa na wapiga mbiu ya Ufalme wengine?

8 Vizuizi vingine vyaweza kuziba sauti ya habari njema. Kwa sababu ya hali mbaya sana ya kiuchumi katika Ghana, wafanyakazi wameondoshwa kazini. Gharama za maisha zimepanda sana, jambo linalofanya kupata riziki za msingi za maisha liwe tatizo kwelikweli. Watu wa Yehova wamekuwa wakikabilianaje? Kwa kumtumaini Yehova, wala si wao wenyewe. Kwa kielelezo, siku moja mtu fulani aliacha bahasha iliyofungwa kwenye dawati la mapokezi la ofisi ya tawi. Kulikuwa na dola 200 katika bahasha hiyo, au mshahara wa chini zaidi wa miezi mitatu. Bahasha hiyo ilitoka kwa mpaji zawadi asiyejulikana, lakini karatasi ya kufungia ilikuwa na mwandiko huu: “Nilipoteza kazi yangu, lakini Yehova ameniandalia nyingine. Namshukuru yeye na Mwanae, Yesu Kristo. Ili kusaidia katika kueneza habari njema za Ufalme kabla ya mwisho kuja, ninatia ndani mchango wa kiasi.”—Linganisha 2 Wakorintho 9:11.

9 Kuhudhuria mikutano kwawazoeza wale wanaojiunga na ile korasi yenye nguvu ya kumsifu Yehova. (Linganisha Zaburi 22:22.) Hivyo, katika sehemu ya kusini ya Honduras, kuna kutaniko liitwalo El Jordán. Ni nini lililo la pekee sana juu ya kikundi hicho kidogo? Ni kule kuhudhuria kwao mikutano kwa uaminifu. Ili kuhudhuria mikutano kila juma wahubiri 12 kati ya wale 19, hulazimika kuvuka mto mpana. Hilo si tatizo kubwa katika majira yenye ukavu, kwa kuwa wao waweza kuuvuka mto kwa kutumia miamba ikiwa mawe ya kukanyagia. Hata hivyo, wakati wa majira ya mvua, hali hubadilika. Ule ambao wakati mmoja ulikuwa mtiririko wa maji machache waja kuwa furiko linaloondolea mbali kila kitu njiani mwalo. Ili kupita kizuizi hicho, ndugu na dada walazimika wawe waogeleaji hodari. Kabla ya kuvuka, wao huweka nguo zao za mkutano katika tina (pipa la chuma) kisha hulifunika kwa mfuko wa plastiki. Mwogeleaji aliye na nguvu zaidi ya wote huitumia tina hiyo kama chelezo na kuongoza kikundi hadi ng’ambo ile nyingine. Wafikapo salama kwenye upande ule mwingine, wao hujikausha, huvaa nguo, na kuwasili kwenye Jumba la Ufalme wakiwa wachangamfu na safi kabisa!—Zaburi 40:9.

Ngome Tuwezamo Kukaa

10. Kwa nini twaweza kumgeukia Yehova katika nyakati za mkazo?

10 Uwe washambuliwa na roho waovu moja kwa moja au wahisi mkazo kutoka vyanzo vingine, Yehova aweza kuwa ngome yako. Mwite katika sala. Yeye husikiliza kwa uangalifu hata yale mauguo ya kimya zaidi ya watu wake. Mtunga-zaburi aliona hilo kuwa kweli na kuandika hivi: “Unitegee sikio lako, uniokoe hima. Uwe kwangu mwamba wa nguvu, nyumba yenye maboma ya kuniokoa. Ndiwe genge langu na ngome yangu; kwa ajili ya jina lako uniongoze, unichunge. Utanitoa katika wavu walionitegea kwa siri, maana Wewe ndiwe ngome yangu.”—Zaburi 31:2-4.

11. Eleza ni kwa nini ngome ya Yehova si mahali pa muda tu.

11 Yehova haandai kimbilio la muda tu bali pia ngome imara tuwezamo kukaa kwa usalama. Watu wake hawajakosa mwongozo na mwelekezo wake. Nguvu za kimungu zitabatilisha vitendo vya ufundi vya Shetani na wazao wake. (Waefeso 6:10, 11) Tumtumainipo Yehova kwa moyo wote, yeye atatuvuta mbali kutoka mitego ya Shetani. (2 Petro 2:9) Katika ile miaka minne iliyopita, kazi ya kuhubiri ya Mashahidi wa Yehova imefunguliwa katika nchi 35 hivi. Pia, katika maeneo ya ulimwengu ambamo hali za kijamii, za kiuchumi, au za kisiasa huzuia kazi ya kuhubiri habari njema, watu fulani wenye mfano wa kondoo wamehamia mahali ambapo wao waweza kufikiwa kwa urahisi zaidi. Japani ni mahali pa jinsi hiyo.

12. Painia mmoja katika Japani alimfanyaje Yehova awe ngome yake?

12 Wafanyakazi wengi wa kigeni wamehamia Japani kutoka ng’ambo, na makutaniko mengi ya lugha za kigeni yameanzishwa. Ono la ndugu mmoja katika kutaniko la Japani laonyesha jinsi shamba hilo la kigeni lilivyo na matokeo mengi. Alitaka kwenda kutumikia mahali ambapo kuna uhitaji mwingi zaidi. Hata hivyo, alikuwa tayari anaongoza mafunzo kumi ya Biblia alikokuwa. Mmoja wa marafiki wake alisema hivi kwa kutania: “Ukienda mahali ambapo kuna uhitaji mkubwa zaidi, utapaswa kuongoza mafunzo ya Biblia 20 huko!” Alipokea mgawo akaenda Hiroshima. Hata hivyo, baada ya miezi minne, alikuwa na funzo la Biblia moja tu. Siku moja alimtembelea mtu mmoja kutoka Brazili aliyeongea Kireno pekee. Kwa kuwa ndugu huyo hakuweza kuwasiliana na mtu huyo, alinunua kitabu cha kufundisha Kireno. Baada ya kujifunza baadhi ya semi sahili za kimazungumzo, alimzuru mtu huyo tena. Ndugu huyo alipomsalimu katika lugha ya Kireno, mtu huyo alishangaa na, kwa tabasamu kubwa, akafungua mlango wazi na kumwalika ndani. Funzo la Biblia lilianzishwa. Upesi ndugu huyo alikuwa akiongoza jumla ya mafunzo 22, 14 katika Kireno, 6 katika Uhispania, na 2 katika Kijapani!

Kuhubiri kwa Uhakika

13. Kwa nini mtu asijaribu kutuaibisha ili tumtumikie Yehova?

13 Watu wa Yehova huimba wimbo wa Ufalme kwa uhakika wakiwa na imani kamili kwamba Yehova ndiye kimbilio lao. (Zaburi 31:14) Wao hawataaibishwa—Yehova hatawatahayarisha, kwani yeye atalitimiza neno lake. (Zaburi 31:17) Ibilisi na majeshi yake ya kishetani wataaibishwa. Kwa kuwa watu wa Yehova wamepewa utume wa kuhubiri ujumbe usio na aibu, wao hawaaibishwi na watu wengine ili wahubiri. Hiyo si njia ambayo Yehova, au Mwana wake, huwachochea watu wake wamwabudu Yeye. Mioyo ya watu inapojaa imani na uthamini kwa ajili ya wema na fadhili-upendo ya Yehova, ni ile hali nzuri ya mioyo yao ichocheayo midomo yao iseme. (Luka 6:45) Hivyo, hata iwe ni muda gani tunaotumia katika utumishi kila mwezi, huo ni mzuri, si wenye kuaibisha, hasa ikiwa muda huo wawakilisha kadiri tuwezavyo kufanya. Je! visarafu vya yule mjane havikuthaminiwa sana na Yesu na Baba yake?—Luka 21:1-4.

14. Waweza kutoa maelezo gani kuhusu kazi ya painia? (Ona chati pia.)

14 Kwa idadi yenye kuongezeka ya wahubiri, kuwa wenye nafsi yote katika ibada yao hutia ndani kutumikia wakiwa mapainia—890,231 kikiwa kilele cha mwaka jana! Maendeleo ya mwaka uliopita yakidumishwa, yaelekea tarakimu hiyo itapita 1,000,000. Ono lifuatalo laonyesha jinsi dada mmoja katika Naijeria alivyoingia upainia. Yeye aandika hivi: “Nilipokuwa karibu kumaliza shule ya upili, nilienda kusaidia kuwapikia wale waliohudhuria shule ya painia ya Mashahidi wa Yehova. Nilikutana na dada wawili huko waliokuwa wenye umri mkubwa kuliko nyanya yangu. Nilipopata kujua kwamba walikuwa mapainia wakihudhuria shule, nilifikiri hivi moyoni, ‘Ikiwa hao wawili waweza kupainia, kwa nini mimi nisiweze?’ Kwa hiyo baada ya kumaliza shule, mimi pia nilikuwa painia wa kawaida.”

15. Ni kwa njia gani kutoa ushahidi vivi hivi kwaweza kuwezesha wengine wapate kimbilio katika Yehova?

15 Si wote wawezao kupainia, lakini wao waweza kutoa ushahidi. Katika Ubelgiji dada mmoja mwenye umri wa miaka 82 alienda kununua nyama. Aliona kwamba mke wa mchinja-nyama alikuwa amefadhaika sana juu ya misukosuko ya kisiasa ya hivi karibuni. Kwa hiyo dada huyo aliweka trakti Mashahidi wa Yehova Wanaamini Nini? pamoja na fedha taslimu alipolipia gharama yake. Dada huyo aliporudi duka hilo, mke wa mchinja-nyama, bila kusita hata kidogo, alimuuliza yale Biblia husema juu ya uwezekano wa vita ya ulimwengu ya tatu. Dada huyo alimletea kitabu Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje? Siku chache baadaye, dada huyo mzee-mzee alipoingia duka hilo, mke wa mchinja-nyama alikuwa na maswali zaidi ya kumuuliza. Dada huyo alimwonea huruma mwanamke huyo; hakuwa na budi kumtolea funzo la Biblia, na hilo likakubaliwa. Sasa, mke wa mchinjanyama ataka kubatizwa. Namna gani mchinja-nyama? Yeye alisoma ile trakti na sasa anajifunza Biblia pia.

‘Hazina ya Wema’

16. Yehova amewekaje kando hazina ya wema kwa ajili ya watu wake?

16 Katika siku hizi za mwisho zenye mkazo, je, Yehova ‘hajawapa fadhili-upendo wa ajabu’ (NW) wale ambao wamepata kimbilio katika yeye? Kama vile baba mwenye upendo, atoaye ulinzi, Yehova ameweka kando hazina ya wema kwa ajili ya watoto wake wa kidunia. Amekuwa akimimina furaha juu yao mbele ya watazamaji wote, kama vile mtunga-zaburi asemavyo: “Jinsi zilivyo nyingi fadhili zako [wema wako, NW] ulizowawekea [hazina, NW] wakuchao; ulizowatendea wakukimbiliao mbele ya wanadamu!”—Zaburi 31:19, 21.

17-19. Katika Ghana, kuhalalisha ndoa kwa mtu mmoja aliyezeeka kulikuwa na tokeo jipi zuri?

17 Kwa hiyo, walimwengu hujionea wenyewe ufuatiaji haki wa wale wanaomwabudu Yehova, na wao hustaajabu. Kwa kielelezo, katika Ghana mtu mmoja mwenye umri wa miaka 96 alienda kwenye ofisi ya msajili wa ndoa akaomba kwamba ndoa yake ya kienyeji ya miaka 70 isajiliwe sasa. Ofisa wa ndoa alishtuka na kuuliza hivi: “Je! una hakika hivyo ndivyo wataka kufanya? Ukiwa na umri huo?”

18 Mtu huyo alieleza hivi: “Nataka kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova na kushiriki katika kazi iliyo ya maana zaidi kabla ya mwisho wa ulimwengu—kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu. Kazi hiyo huongoza kwenye uhai wa milele. Mashahidi wa Yehova hutii sheria ya serikali, kutia ndani sheria juu ya usajili wa ndoa. Kwa hiyo nifanyie usajili huo.” Ofisa huyo aliduwazwa. Alifanya usajili huo, na mtu huyo mzee-mzee aliondoka akiwa amefurahi kwamba sasa alikuwa na ndoa halali.—Linganisha Warumi 12:2.

19 Baada ya hilo, msajili wa ndoa aliyafikiria sana mambo yale aliyokuwa amesikia. “Mashahidi wa Yehova . . . kazi iliyo ya maana zaidi . . . mwisho wa ulimwengu . . . Ufalme wa Mungu . . . uhai wa milele.” Akiwa ametatanika kuhusu jinsi yote hayo yalivyokuwa na maana maishani mwa mtu mwenye umri wa miaka 96, aliamua kuwatafuta Mashahidi ili kuchunguza jambo hilo zaidi. Alikubali funzo la Biblia nyumbani akafanya maendeleo ya haraka. Leo, msajili huyo wa ndoa ni Shahidi aliyebatizwa. Hivyo, tunapomtii Yehova hata katika yale ambayo huenda watu wakaona kuwa mambo madogo, yaweza kuwa na matokeo mengi mazuri kwetu sisi na kwa wale waliojionea wenyewe mwenendo wetu.—Linganisha 1 Petro 2:12.

20. Katika Myanmari, ufuatiaji haki wa dada mmoja mchanga uliongozaje kwenye ushahidi mzuri?

20 Wale wenye umri mkubwa zaidi ambao wameruhusu kweli iwafinyange kuwa watu wenye kufuatia haki huwekea kielelezo chema wale wenye umri mdogo zaidi walio katika ulimwengu huu usiofuatia haki. Kuna dada mchanga wa jinsi hiyo anayeishi Myanmari. Yeye atoka familia maskini na ya hali ya chini yenye watoto kumi. Baba, ambaye hupokea malipo ya uzeeni, ni painia wa kawaida. Siku moja akiwa shuleni, dada huyo alipata pete ya almasi, ambayo alimpelekea mwalimu wake upesi. Darasa lilipoanza siku ifuatayo, mwalimu aliambia darasa jinsi pete hiyo ilivyopatikana na kukabidhiwa ili irudishwe kwa mwenyewe. Kisha akamwomba yule dada mchanga asimame mbele ya darasa nzima na kueleza kwa nini alikuwa amefanya hivyo, akijua kwamba wale watoto wengine wangaliweza kuamua kuiweka. Dada huyo alieleza kwamba yeye alikuwa Shahidi wa Yehova na kwamba Mungu wake hapendi wizi wala kutofuatia haki kwa aina yoyote. Shule nzima ilisikia juu ya hilo, hilo likimpa dada yetu mchanga fursa nzuri ya kutolea ushahidi walimu na wanafunzi vilevile.

21. Vijana wanapomtumaini Yehova, mwenendo wao humpa sifa gani?

21 Katika Ubelgiji mwalimu mmoja alisema jambo lenye kupendeza juu ya Mashahidi wa Yehova. Alikuwa ameona mwenendo wa mmoja wa wanafunzi wake, ambaye pia alikuwa dada mchanga, na kusema hivi: “Sasa nina maoni tofauti juu ya Mashahidi wa Yehova. Chuki isiyo na sababu ilikuwa imeniongoza nifikiri kwamba wao wasingekuwa wenye uvumilivu hata kidogo. Walithibitika kuwa wenye uvumilivu zaidi ya wote, huku wakiwa hawaridhiani kanuni zao.” Kila mwaka zawadi hutolewa na walimu kwa wanafunzi wao bora zaidi. Miongoni mwa zawadi nyingine kuna moja kwa ajili ya mtalaa wa maadili. Kwa miaka mitatu mfululizo, zawadi kwa ajili ya maksi za tatu za juu zaidi zilitolewa na mwalimu huyo kwa watoto wa Mashahidi wa Yehova. Ndivyo itokeavyo mara nyingi kwa wale ambao tumaini lao lenye uaminifu-mshikamanifu limewekwa katika Yehova.—Zaburi 31:23.

22. Ni nini umalizio wenye ushindi wa Zaburi 31, na huo hutusaidiaje katika siku za mwisho za mfumo huu wa mambo?

22 Zaburi 31 yavuma ikiwa na umalizio huu wenye ushindi: “Iweni hodari, mpige moyo konde, ninyi nyote mnaomngoja BWANA [Yehova, NW].” (Zaburi 31:24) Kwa hiyo, tukabilipo siku za mwisho za mfumo mwovu wa Shetani, mbali sana na kutuacha, Yehova atatukaribia sana na kuweka ndani yetu nguvu zake mwenyewe. Yehova ni mwaminifu naye hashindwi. Yeye ndiye kimbilio letu; yeye ndiye mnara wetu.—Mithali 18:10.

Je! Wakumbuka?

◻ Kwa nini twaweza kwa hakika kumfanya Yehova awe kimbilio letu?

◻ Kuna ithibati gani kwamba korasi yenye nguvu inaimba sifa za Ufalme kwa moyo mkuu?

◻ Kwa nini twaweza kuwa na hakika kwamba wavu wa Shetani hautawanasa watu wa Yehova?

◻ Yehova ameweka kando hazina gani kwa ajili ya wale wapatao kimbilio katika yeye?

[Chati katika kurasa za 12-15]

RIPOTI YA MWAKA WA UTUMISHI WA 1993 YA MASHAHIDI WA YEHOVA ULIMWENGUNI POTE

(Ona buku lililojalidiwa)

[Picha katika kurasa za 16, 17]

Wale wapatao kimbilio katika Yehova hufanyiza korasi yenye nguvu ya wapiga mbiu ya Ufalme—yenye watu 4,709,889!

1. Senegal

2. Brazili

3. Chile

4. Bolivia

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki