Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 7/15 kur. 8-9
  • Mashahidi wa Yehova Ulimwenguni Pote—Kolombia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mashahidi wa Yehova Ulimwenguni Pote—Kolombia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Wakuu wa Biashara Wavutiwa
  • Kweli Yafikia Watu wa Aina Zote
  • Mashahidi wa Yehova—Ripoti ya Kitabu-Mwaka 1994
    1994 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • 1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Ya Kwanza Miaka 100 Iliyopita
    Amkeni!—2000
  • Makao Makuu ya Ulimwengu na Ofisi ya Tawi Makuu ya Mashahidi wa Yehova
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 7/15 kur. 8-9

Mashahidi wa Yehova Ulimwenguni Pote—Kolombia

KOLOMBIA ni nchi ya kipekee ya Amerika Kusini. Bahari zote mbili za Atlantiki na Pasifiki ndizo pwani za nchi hii iliyojaa volkeno. Hali ya hewa yatofautiana kutoka joto la tropiki katika pwani hadi baridi kwenye vilele virefu vyenye theluji vya Milima Andes.a

Ingawa Kolombia inajulikana sana kwa kutokeza dhahabu na zumaradi, thamani yayo kubwa sana ni watu wayo. Leo, Yehova ajaza nyumba yake ya kiroho utukufu. Waabudu wake wanaopendeza na kutamanika wanamiminikia nyumba yake kutoka sehemu zote za dunia, kutia ndani Kolombia.—Hagai 2:7.

Wakuu wa Biashara Wavutiwa

Jumapili, Novemba 1, 1992, ilikuwa siku ya kuweka wakfu ofisi mpya ya tawi na kiwanda cha uchapishaji cha Watch Tower Society katika Facatativá, iliyoko kilometa 42 kaskazini-magharibi mwa Bogotá. Matembezi kwenye ofisi ya tawi yamevutia sana wageni. Mara tu mgeni mmoja aliporudi kwenye kiwanda alikofanya kazi, kwa msisimko aliwahimiza mameneja wake waende wakatazame shirika lililo ‘ajabu kwa habari ya ustadi, utaratibu, na ari ya wafanyakazi.’ Katika ziara yao iliyofuata, wakuu hao walipendezwa sana, nao wakauliza maswali mengi.

Wakuu hao walitaka walete waelekezi, wasimamizi, na wanyapara wao—kwa hakika, wafanyakazi wao wote—waje kuzuru. Kila juma, walikuwa wakipanga wafanyakazi kati ya 15 na 25 waje kuzuru mpaka wafanyakazi wote 1,300 waweze kuona ustadi huo wa mpango wa kazi.

Mamia ya wafanyakazi wao wamezuru ofisi ya tawi na wametazama ile video Jehovah’s Witnesses—The Organization Behind the Name. Kwa kuvutiwa na ukubwa na tengenezo na kazi ya kuhubiri Ufalme kotekote ulimwenguni, wao walistaajabia ufundi wa hali ya juu unaotumiwa katika kazi za Sosaiti. Wakati wa kuondoka, wengi husikika wakisema kwamba wanahisi kana kwamba walikuwa ‘wakiacha Paradiso na kurudia ulimwengu usio na utaratibu.’

Kweli Yafikia Watu wa Aina Zote

Watu wa aina zote wanafikiwa na habari njema. (1 Timotheo 2:3, 4) Kwa kielelezo, mtu mmoja aliyekuwa mtungaji-muziki na pia kiongozi wa beni ya muziki wa mdundo mzito alikubali kweli ya Biblia, akafanya mabadiliko katika maisha yake, na upesi akawa painia wa kawaida. Baadaye aliwekwa rasmi kuwa mtumishi wa huduma. Watu kadhaa waliokuwa washiriki wa vikundi haramu wamejifunza kuweka hakika yao na tumaini lao katika Ufalme wa Yehova. Sasa wao ni watendaji wenye bidii katika kuhubiri ujumbe wa ulimwengu mpya wenye amani.

Waraibu na walanguzi wa dawa za kulevya pia wamekuja kwenye kweli. Kijana mmoja ambaye sasa ni Shahidi alikuwa amelima shamba la dawa za kulevya na kuendesha maabara ya kokeini msituni kwa muda wa miaka mitano kabla ya yeye kuacha maisha ya aina hiyo. Yeye amepata furaha kujifunza na kufuata maishani kanuni za Biblia. Katika gereza moja, wauaji fulani waliohukumiwa walisukumwa na funzo la unyoofu la Biblia nao wanasali kwa bidii kwamba Yehova awasamehe dhambi zao na awakubali kuwa watumishi wake.

Kwa hiyo watu wa aina zote wanaitikia ujumbe wa Ufalme. Nchini Kolombia, kama ilivyo na kwingineko, Yehova anajaza vivyohivyo nyumba yake utukufu.

[Maelezo ya Chini]

a Kwa habari zaidi, ona 1994 Calendar of Jehovah’s Witnesses.

[Sanduku katika ukurasa wa 8]

HABARI ZA NCHI

Mwaka wa Utumishi wa 1993

KILELE CHA WANAOTOA USHAHIDI: 60,854

UWIANO: Shahidi 1 kwa watu 558

HUDHURIO LA UKUMBUSHO: 249,271

WASTANI WA WAHUBIRI WALIO MAPAINIA: 8,487

WASTANI WA MAFUNZO YA BIBLIA: 100,927

IDADI YA WALIOBATIZWA: 5,183

IDADI YA MAKUTANIKO: 751

OFISI YA TAWI: FACATATIVÁ

[Picha katika ukurasa wa 9]

Wafanyakazi wa ofisi ya tawi na wamishonari mwaka wa 1956

[Picha katika ukurasa wa 9]

Picha ya juu ya ofisi ya tawi

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki