Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w96 7/15 uku. 30
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Habari Zinazolingana
  • “Ni Nini Itakayokuwa Ishara ya Kuwapo Kwako?”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • “Tuambie, Mambo Haya Yatakuwa Wakati Gani?”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Matetemeko Makubwa ya Ardhi—Biblia Ilitabiri Nini?
    Habari Zaidi
  • Matetemeko ya Ardhi Ni Ishara ya Ule Mwisho?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
w96 7/15 uku. 30

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Naelewa kwamba neno la Kigiriki “toʹte” (ndipo) hutumiwa ili kutolea utangulizi jambo linalofuata. Basi, kwa nini Mathayo 24:9 (NW) husomwa hivi: “Ndipo [“toʹte”] watu watakapowakabidhi nyinyi kwenye dhiki,” hali simulizi kwenye Luka 21:12 (NW) linalolingana, lasema hivi: “Lakini kabla ya mambo yote hayo watu watawawekea mikono ili wawashike na kuwanyanyasa nyinyi”?

Ni sahihi kwamba toʹte laweza kutumiwa kutolea utangulizi jambo linalofuata, yaani, jambo lenye kuandama. Lakini hatupasi kuelewa kwamba huo ndio utumizi pekee wa Kibiblia wa hilo neno.

Kitabu A Greek-English Lexicon of the New Testament and Other Early Christian Literature, cha Bauer, Arndt, na Gingrich, huonyesha kwamba neno toʹte hutumiwa katika maana mbili za msingi katika Maandiko.

Moja ni “wakati huo.” Hilo laweza kuwa “ndipo ya wakati uliopita.” Kielelezo kitolewacho ni Mathayo 2:17: “Ndipo lilipotimia neno lililonenwa na nabii Yeremia.” Hilo halirejezei jambo fulani katika mfululizo bali laonyesha wakati hususa katika wakati uliopita, wakati huo. Vivyo hivyo, toʹte laweza kutumiwa “kuhusu ndipo ya wakati ujao.” Kisa kimoja chapatikana kwenye 1 Wakorintho 13:12 (NW): “Kwa maana wakati wa sasa twaona katika njia isiyo ya waziwazi kupitia kioo cha madini, lakini wakati huo itakuwa uso kwa uso. Wakati wa sasa najua kwa sehemu tu, lakini wakati huo nitajua kwa usahihi kama vile nijulikanavyo kwa usahihi.” Paulo hapa alitumia toʹte katika maana ya ‘kwenye wakati huo ujao.’

Kulingana na kamusi hiyo, matumizi mengine ya toʹte ni “kutolea utangulizi jambo linalofuata katika wakati.” Kamusi hiyo inatoa vielelezo vingi vipatikanavyo katika masimulizi matatu ya jibu la Yesu kwa swali la mitume juu ya ishara ya kuwapo kwake.a Vikiwa vielelezo vya matumizi ya toʹte “ili kutolea utangulizi jambo linalofuata katika wakati,” hiyo kamusi ilinukuu Mathayo 24:10, 14, 16, 30; Marko 13:14, 21; na Luka 21:20, 27. Kufikiria muktadha huonyesha kwa nini jambo fulani linalofuata katika wakati ndio uelewevu mzuri. Na hilo ni lenye msaada katika kupata maana ya unabii wa Yesu uliotia ndani kusitawi kwa matukio ya wakati ujao.

Hata hivyo, hatuhitaji kukata maneno kwamba katika kila kisa cha toʹte katika masimulizi hayo lazima chatolea utangulizi jambo linalofuata katika wakati. Kwa mfano, kwenye Mathayo 24:7, 8, twasoma kwamba Yesu alitabiri kwamba taifa lingeinuka dhidi ya taifa na kwamba kungekuwa na upungufu wa chakula na matetemeko ya dunia. Mstari wa 9 (NW) waendelea kusema: “Ndipo watu watakapowakabidhi nyinyi kwenye dhiki na watawaua nyinyi, nanyi mtakuwa vitu vya kuchukiwa na mataifa yote kwa sababu ya jina langu.” Je, ingefaa kuelewa kwamba vita, upungufu wa chakula, na matetemeko ya dunia yaliyotabiriwa lazima yote yatukie, na labda hata yakome, kabla ya mnyanyaso kuanza?

Hilo halipatani na kufikiri kuzuri, wala halionyeshwi na yale tujuayo kuhusu utimizo katika karne ya kwanza. Simulizi katika kitabu cha Matendo hufunua kwamba karibu mara moja baada ya washiriki wa kutaniko jipya la Kikristo walipoanza kuhubiri, walipatwa na upinzani mkali. (Matendo 4:5-21; 5:17-40) Kwa hakika hatuwezi kusema kwamba vita vyote, njaa kuu zote, na matetemeko yote ya dunia ambayo Yesu alisema juu yayo yalitendeka kabla ya mnyanyaso huo wa mapema. Badala ya hivyo, upinzani huo ulitokea “kabla ya” mengi ya yale mambo mengine yaliyotabiriwa, jambo ambalo hupatana na vile Luka alivyoeleza mambo: “Lakini kabla ya mambo yote hayo watu watawawekea mikono ili wawashike na kuwanyanyasa nyinyi.” (Luka 21:12, NW) Hilo lingedokeza kwamba kwenye Mathayo 24:9, toʹte hutumiwa zaidi katika maana ya “wakati huo.” Katika kile kipindi cha vita, njaa kuu, na matetemeko ya dunia, au wakati huo, wafuasi wa Yesu wangenyanyaswa.

[Maelezo ya Chini]

a Masimulizi hayo yanayolingana katika Mathayo, Marko, na Luka yaliorodheshwa katika safu kwenye kurasa 14 na 15 za Mnara wa Mlinzi la Februari 15, 1994. Herufi nene zimetumiwa mahali toʹte lifasiriwapo kuwa “ndipo.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki