Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w99 6/1 uku. 8
  • “Kwa Mungu Mambo Yote Yawezekana”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Kwa Mungu Mambo Yote Yawezekana”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Habari Zinazolingana
  • Nashukuru kwa Ajili ya Utegemezo wa Yehova Usioshindwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Mambo Mawili juu ya Msiba
    Amkeni!—1998
  • Kutatua Matatizo ya Vijana
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Jinsi Nilivyonufaika Kutokana na Utunzaji wa Mungu
    Amkeni!—1995
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
w99 6/1 uku. 8

Wapiga-mbiu wa Ufalme Waripoti

“Kwa Mungu Mambo Yote Yawezekana”

MANENO haya yaliyo juu, yapatikanayo kwenye Mathayo 19:26, yalibainika kuwa ya kweli kwa mwanamke mmoja kijana wa Venezuela. Baada ya kujifunza kumtumaini Yehova kabisa, aliweza kushinda tatizo kubwa. Yeye anasimulia hivi:

“Nyanya yangu alikuwa mwenye fadhili na mwenye upendo sana. Kwa kusikitisha, alikufa nilipokuwa na umri wa miaka 16 tu. Kifo chake kiliniathiri sana. Nilivurugika sana akili, nisitake hata kutoka nje ya nyumba kwenda uani. Niliishia kuwa mtu ambaye karibu amejitenga kabisa.

“Sikwenda shuleni, wala sikuwa na kazi. Nilikaa tu chumbani mwangu. Kwa sababu ya upweke na kukosa rafiki kabisa, nilipatwa na mshuko-moyo mkubwa. Nilijihisi sifai kitu kabisa, nikataka kufa na mambo yaishe. Nilijiuliza tena na tena, ‘Kwa nini niko hai?’

“Mama yangu alikuwa akipokea magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! kutoka kwa Shahidi mmoja mchanga aitwaye Gisela. Siku moja mama yangu alimwona Gisela alipokuwa akipita karibu na nyumba yetu na kumwuliza kama angeweza kunisaidia. Gisela alikubali kujaribu, lakini nikakataa kukutana naye. Kufanya hivyo hakukumzuia Gisela. Aliniandikia barua na kuniambia kwamba alitaka kuwa rafiki yangu na kwamba mtu fulani aliye wa maana zaidi kumshinda alitaka pia kuwa rafiki yangu. Alisema mtu huyo ni Yehova Mungu.

“Jambo hilo lilinigusa moyo, nami nikajibu barua yake. Tuliandikiana barua kwa muda wa miezi mitatu. Hatimaye, nilipata ujasiri wa kukutana na Gisela baada tu ya kusihiwa sana naye. Tulipokutana mara ya kwanza, Gisela alijifunza Biblia pamoja nami, akitumia kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Baada ya funzo hilo, alinialika nihudhurie mkutano kwenye Jumba la Ufalme la kwetu. Nikashtuka. Sikuwa nimetoka nyumbani kwa muda wa miaka minne, na wazo la kuwa barabarani liliniogopesha.

“Gisela alinionyesha subira nyingi. Alinihakikishia kwamba sikuhitaji kuogopa chochote na kwamba angeandamana nami kwenda kwenye mkutano huo. Hatimaye nikakubali. Tulipofika kwenye Jumba la Ufalme, nilianza kutetemeka na kutoa jasho. Sikuweza kusalimu mtu yeyote. Hata hivyo, nilikubali kuendelea kuhudhuria mikutano, naye Gisela alipitia nyumbani kunichukua kila juma bila kukosa.

“Gisela alinipeleka kwenye mikutano mapema sana ili kunisaidia kuondoa wasiwasi wangu. Tulisimama mlangoni na kusalimu kila mtu walipokuwa wakiwasili. Kwa njia hiyo, nilikutana na mtu mmoja au wawili kwa wakati mmoja, badala ya kikundi chote mara moja. Nilipohisi kwamba singeweza kuvumilia zaidi, Gisela alininukulia andiko la Mathayo 19:26: ‘Kwa wanadamu hilo haliwezekani, bali kwa Mungu mambo yote yawezekana.’

“Ingawa haikuwa rahisi, hatimaye niliweza kuhudhuria mkutano wenye watu wengi hata zaidi kwenye kusanyiko la mzunguko. Hiyo ilikuwa hatua kubwa kama nini niliyofanya! Katika Septemba mwaka wa 1995, nilipiga moyo konde kuzungumza na wazee juu ya kushiriki katika huduma ya nyumba hadi nyumba. Miezi sita baadaye, Aprili mwaka wa 1996, nilionyesha wakfu wangu kwa Yehova kwa ubatizo wa maji.

“Wakati mtu fulani aliponiuliza hivi majuzi jinsi nilivyopata ujasiri wa kufanya hivyo, nilimjibu hivi: ‘Tamaa yangu ya kumpendeza Yehova ni kubwa kushinda hofu yangu.’ Ingawa bado mimi hupatwa na mshuko-moyo mara kwa mara, shangwe yangu inazidishwa kwa kutumikia nikiwa painia wa kawaida. Nikumbukapo, sina budi kukubaliana na Gisela. Sasa nina Rafiki anayependezwa nami na ‘anayenipa nguvu.’”—Wafilipi 4:13.

[Picha katika ukurasa wa 8]

“Tamaa yangu ya kumpendeza Yehova ni kubwa kushinda hofu yangu”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki