Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w09 4/1 uku. 31
  • Baba ya Wavulana Wasio na Baba

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Baba ya Wavulana Wasio na Baba
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Pendezwa na ‘Mayatima’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Familia Zisizo na Baba Kukomesha Zoea Hilo
    Amkeni!—2000
  • Je! Watoto Wako ni Wanafunzi wa Kristo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
w09 4/1 uku. 31

Mkaribie Mungu

Baba ya Wavulana Wasio na Baba

Kutoka 22:22-24

‘MUNGU katika makao yake matakatifu ni baba ya wavulana wasio na baba.’ (Zaburi 68:5) Maneno haya ya Biblia yanatufundisha jambo lenye kugusa moyo kumhusu Yehova Mungu. Yanaonyesha kwamba anatambua uhitaji wa wale wanaotaabika. Sheria ambayo aliwapa Waisraeli inaonyesha wazi kwamba anawajali watoto wanaofiwa na mzazi. Tuchunguze andiko la kwanza katika Biblia linalomtaja “mvulana asiye na baba,”a yaani, Kutoka 22:22-24.

Mungu anaonya hivi: ‘Msimtese mvulana yeyote asiye na baba.’ (Mstari wa 22) Maneno haya si maombi tu ya kuwasaidia watoto waliofiwa na mzazi, bali ni amri kutoka kwa Mungu. Mtoto aliyekuwa amefiwa na baba hakuwa na mtu wa kumtunza na kumruzuku, na ingekuwa rahisi kwa wengine kumdhulumu. Sheria iliwaamuru watu ‘wasimtese’ mtoto asiye na baba kwa njia yoyote ile. Katika tafsiri nyingine za Biblia neno “msimtese” linatafsiriwa “msimdhulumu,” “msitende mtu vibaya,” au “msimkandamize mtu ili kujipatia faida.” Lilikuwa kosa zito machoni pa Mungu kumdhulumu mtoto asiye na baba. Lilikuwa zito kadiri gani?

Sheria inasema: “Mkimtesa hata kidogo, naye anililie hata kidogo, sitakosa kukisikia kilio chake.” (Mstari wa 23) Katika lugha ya awali ya Kiebrania neno linalotafsiriwa “msimtese” katika mstari wa 22 linaonyesha wingi, lakini katika mstari wa 23 neno hilo linatafsiriwa katika hali ya umoja. Kwa hiyo, lugha ya awali inaonyesha kwamba taifa zima na pia mtu mmoja-mmoja alikuwa na wajibu uleule wa kutii amri hii ya Mungu. Yehova alikuwa akitazama; alisikia kilio cha wavulana wasio na baba, na alikuwa tayari daima kuwasaidia walipomwomba msaada.—Zaburi 10:14; Methali 23:10, 11.

Basi, matokeo yangekuwa nini ikiwa mtu angemdhulumu mvulana asiye na baba na yule mtoto amlilie Mungu? Yehova anasema: “Hasira yangu itawaka kwelikweli, nami hakika nitawaua kwa upanga.” (Mstari wa 24) Kitabu kimoja cha marejeo ya Biblia kinasema kwamba “tafsiri ya neno kwa neno ya maneno hayo ni ‘na pua yangu itawaka moto,’ usemi unaomaanisha hasira kali sana.” Yehova hakuwaachia waamuzi wanadamu wa taifa la Israeli jukumu la kutekeleza sheria hii. Mungu mwenyewe angemhukumu mtu yeyote aliyemdhulumu mtoto asiyeweza kujitetea.—Kumbukumbu la Torati 10:17, 18.

Yehova hajabadilika. (Malaki 3:6) Anawahurumia sana watoto ambao wamepoteza mzazi mmoja au wazazi wote wawili. (Yakobo 1:27) Uwe na hakika kwamba hasira ya haki ya Baba ya wavulana wasio na baba inawaka anapowaona watoto wasio na hatia wakidhulumiwa. Watu wanaomdhulumu mtoto asiyeweza kujitetea hawataepuka “hasira inayowaka ya Yehova.” (Sefania 2:2) Watu hao waovu watajua kwamba “ni jambo lenye kuogopesha kuanguka mikononi mwa Mungu aliye hai.”—Waebrania 10:31.

[Maelezo ya chini]

a Maneno “mvulana asiye na baba” yanapatikana mara 40 hivi katika Biblia. Ingawa neno la Kiebrania linalotafsiriwa “mvulana asiye na baba” linataja mtoto wa kiume, hatupaswi kukata kauli kwamba kanuni zinazozungumziwa hazihusu wasichana wasio na baba. Sheria ya Musa ilitetea haki ya wasichana wasio na baba sawa na wavulana.—Hesabu 27:1-8.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki