Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w12 6/15 uku. 32
  • Fadhili Huondoa Uchungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Fadhili Huondoa Uchungu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Habari Zinazolingana
  • Kutoka Mshuko wa Moyo Hadi Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Mwishowe Mbegu Ilichipuka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Kutatua Matatizo ya Vijana
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Waambie Unawapenda
    Masimulizi ya Mashahidi wa Yehova
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
w12 6/15 uku. 32

Fadhili Huondoa Uchungu

MWANAMKE mmoja mzee hakuonyesha urafiki wakati Mashahidi wawili huko Uholanzi, George na Manon, walipomhubiria habari njema ya Ufalme. Walitambua kwamba alikuwa amefiwa na mtoto wake wa kiume, mume wake wa kwanza na wa pili na alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa mbaya wa yabisi-kavu. Ingawa alitulia kwa kiasi fulani wakati wa mazungumzo hayo, hakuwa mwenye urafiki hata kidogo.

Hata hivyo, George alimpendekezea Manon kwamba wamrudie mwanamke huyo na kumpelekea shada la maua kwa sababu alionekana mpweke na mwenye uchungu moyoni. Walipofanya hivyo, mwenye nyumba huyo anayeitwa Rie, alifurahi na kushangaa. Hata hivyo, haukuwa wakati unaofaa wa kuzungumza naye, kwa hiyo walipanga kumtembelea siku nyingine. George na Manon waliporudi siku waliyopanga, hakuna mtu aliyefungua mlango. Ingawa walijaribu kumtembelea nyakati tofauti-tofauti, hawakumpata tena. Hata walianza kufikiri kwamba alikuwa akiwaepuka.

Hatimaye siku moja, George alimkuta Rie nyumbani. Na Rie akaomba msamaha kwa kutotimiza ahadi na akawaambia kwamba alikuwa hospitalini. “Lakini, hamwezi kamwe kuwazia kile nilichofanya baada ya ninyi kuondoka,” akasema. “Nilianza kusoma Biblia!” Walikuwa na mazungumzo mazuri, na funzo la Biblia likaanzishwa.

Kadiri Rie alivyoendelea kujifunza Biblia, ndivyo alivyobadilika na kuwa mtu mwenye furaha na fadhili, badala ya kuwa mtu mwenye uchungu. Ingawa hangeweza kutoka nyumbani kwa sababu ya ugonjwa, alianza mara moja kumweleza yeyote aliyekuja kumtembelea kuhusu imani yake mpya. Afya yake mbaya haikumruhusu kuhudhuria mikutano ya kutaniko kwa ukawaida, hata hivyo alifurahi kuona ndugu na dada wakimtembelea. Siku alipofikisha umri wa miaka 82, alihudhuria kusanyiko la mzunguko na kisha akabatizwa ili kuonyesha wakfu wake kwa Mungu.

Miezi michache tu baada ya kifo chake, shairi aliloandika kabla ya kifo chake lilipatikana. Katika shairi hilo, alieleza kuhusu taabu ya upweke hasa mtu anapokuwa mzee na akakazia umuhimu wa fadhili. “Niliguswa moyo sana niliposoma shairi hilo,” akasema Manon, “na ninafurahi sana kwamba Yehova alitusaidia kumwonyesha mwanamke huyo fadhili.”

Ndiyo, mfano wa Yehova mwenyewe unatuchochea kuonyesha upendo na fadhili kama hiyo. (Efe. 5:1, 2) Huduma yetu itakuwa yenye matokeo zaidi tukiendelea ‘kujipendekeza kuwa wahudumu wa Mungu, kwa fadhili.’—2 Kor. 6:4, 6.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki