Sehemu za Pekee za Mkusanyiko Zaunganisha
1 “Tazama, jinsi ilivyo vema, na kupendeza, ndugu wakae pamoja, kwa umoja.” (Zab. 133:1) Baada ya kufurahia programu yetu ya “Haki ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya pamoja na sehemu zayo mbalimbali za pekee, maneno haya yamekuwa yenye umaana zaidi kwa udugu wa ulimwenguni pote wa watu wa Yehova.
2 Jambo la pekee lilikuwa kutolewa kwa kichapo chenye mabuku mawili chenye kichwa Insight on the Scriptures. Lo, ni kichapo chenye vielezi vizuri kama nini! Jinsi kitakavyotuunganisha katika kufanya uchunguzi wa habari za Biblia ili tunene kwa upatano kuhusu umaana halisi wa Maandiko!—1 Kor. 1:10.
3 Ni mshangao ulioje wenye kupendeza tuliopata Jumamosi alasiri wakati tangazo lilipofanywa kwamba kichapo kipya chenye kichwa Revelation—It’s Grand Climax at Hand! kilikuwa kikitolewa. Hakika kitabu hicho chenye kurasa 320 kitatusaidia tuunganishe mawazo yetu kuhusu maana ya semi nyingi za ufananisho zinazopatikana katika kitabu cha mwisho cha Biblia.
4 Jambo ambalo haliwezi kusahaulika ni ile sehemu ya pekee ambamo wamisionari walieleza mambo waliyojionea wenyewe kwenye mikusanyiko iliyo mingi. Jinsi tunavyothamini miaka ambayo wametumia katika utumishi kwa uaminifu! Vijapokuwa vipingamizi vingi, kama vile afya mbaya, matatizo ya lugha, na upinzani, wao wamepanua kazi ya kuhubiri habari njema katika mabara ya mbali.
5 Hakika Yehova ametubariki na mengi zaidi ya tulivyotazamia. Sasa tunapaswa kupiga moyo konde tupeleke ushuhuda kuhusu haki ya kimungu ili kwamba wengine wenye mioyo yenye uadilifu waweze kuitikia.