Je! Wewe Unafanya Ziara za Kurudia Zako?
1 Lo, ni ripoti ya utendaji wenye nishati-msukumo inayosisimua kama nini ambayo imetolewa katika Kitabu cha Mwaka 1989 cha Mashahidi wa Yehova! Mamilioni ya watu wamekuwa wakisikia habari njema na mamilioni ya fasihi zimeangushiwa watu wenye kupendezwa. Ripoti hiyo inaonyesha ufahamu mwingi wa uhitaji wa kurudi ambapo mbegu za ukweli zimepandwa. (1 Kor. 3:6, 7) Uangalifu zaidi ni wa muhimu. Kushiriki kikamili katika kazi hii kumewaletea watu wa Yehova shangwe kubwa, ambao walifanya jumla ya ziara za kurudia 288,017,474 mwaka uliopita.
WAKATI GANI?
2 Unapopata watu wanaopendezwa, je! wewe unafanya ziara ya kurudia kabla kupendezwa kule kwa mwanzoni hakujapoa? Mara nyingi kurudia katika siku chache kunaleta matokeo mazuri. Tunza maandishi sahihi na yaliyo kamili ya vyovyote ulivyoangusha na kupendezwa ulikopata. Rudia maandishi hayo kwa ukawaida ili uhakikishe kwamba ziara zako zote za kurudia zinafanywa mara moja. Juhudi na udumifu wako utabarikiwa na Yehova na utanufaisha sana wale ambao wameonyesha kupendezwa.
3 Februari ni mwezi mzuri wa kuratibu wakati zaidi kwa ajili ya kufanya ziara za kurudia na kuanzisha mafunzo ya Biblia. Je! kuna watu ambao wamekuwa wakiyachukua magazeti kwa ukawaida na ambao sasa wana nia ya kujifunza? Ndugu mmoja alimwangushia mwanamume mmoja magazeti mawili lakini hakufanya ziara ya kurudia, akiwaza kwamba mtu huyo hakupendezwa sana. Mwanamume huyo aliandikia barua kundi la mahali hapo, akiomba msaada wa kiroho. Mapainia wengi wanaripoti kwamba mafunzo mazuri sana yanatokea kwa kufuatilia maangusho ya magazeti, Je! kuna watu mmoja mmoja ambao wamehudhuria Ukumbusho au mikutano mingine katika pindi fulani ambao wangependa kujifunza?
KUANZISHA FUNZO
4 Kitabu Kuishi Milele kimethibitika kuwa chombo chenye matokeo katika huduma yetu. Hata hivyo, kukiangusha ni hatua ya kwanza tu kuelekea kuanzisha funzo. Katika ziara ya kwanza au wakati wa kufanya ziara ya kurudia, uliza: “Je! wewe umewahi kufikiri juu ya kuishi milele? [Ruhusu itikio.] Bila shaka, watu wengi hawangependa sana kuvumilia milele kuteseka, jeuri, na njaa ambavyo vimesumbua wengi sana wakati huu.” Ukifungua kurasa 11-13, huenda ukauliza hivi: “Lakini tuseme kwamba ungeweza kuishi milele chini ya hali hizi. Je! hilo halingekuwa jambo lenye kufurahisha? (Ruhusu itikio.] Kuishi milele chini ya hali kamilifu kama hizi kunataka jambo fulani kwetu. Angalia fungu 19 linavyosema. [Soma.] Acha nikuonyeshe jinsi kitabu hiki kimetayarishwa ili kikusaidie utwae maarifa hayo.”
5 Wahubiri wanatiwa moyo waachie watu mmoja mmoja trakti ambao hawachukui toleo la fasihi ya kawaida au mahali ambapo hakuna mtu nyumbani. Hizo zinaweza kutumiwa kwa matokeo mazuri kwenye ziara za kurudia ili kuonyesha njia yetu ya kujifunza. Kila trakti inazungumzia habari mbili au tatu. Soma fungu moja moja pamoja na mwenye nyumba. Swali linapoulizwa, tua na kumwomba mwenye nyumba atoe maelezo yake mwenyewe. Fungua na kutumia maandiko ambayo yameonyeshwa.
6 Mambo yaliyoonwa yameonyesha kwamba ni jambo zuri kuratibu wakati uliowekwa kwa ajili ya ziara za kurudia, kusitawisha na kuongoza mafunzo. Kuwa na wakati hususa kwa ajili ya kazi hiyo kutatusaidia kufuatia kupendezwa mara moja. Labda wakati unaweza kuwekwa kando jioni, wakati wa mwisho-juma, au baada ya kumaliza kazi ya nyumba kwa nyumba. Chagua wakati ulio bora kwako na kwa eneo. Kisha ujitahidi kushiriki katika kazi hiyo kwa ukawaida, ili kufanya wanafunzi.—Mt. 28:19, 20.