Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/89 uku. 3
  • Chukua Kila Fursa Kutoa Ushuhuda—Sehemu 1

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Chukua Kila Fursa Kutoa Ushuhuda—Sehemu 1
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UWE UMEJITAYARISHA
  • ANZISHA MAZUNGUMZO
  • Unaweza Kuhubiri Isivyo Rasmi!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Je, Uko Tayari Kuhubiri Isivyo Rasmi?
    Huduma ya Ufalme—2009
  • Kwa Kufanyiza Fursa za Kutoa Ushahidi wa Vivi Hivi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Ongea Juu ya Utukufu wa Umaliki wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1989
km 6/89 uku. 3

Chukua Kila Fursa Kutoa Ushuhuda—Sehemu 1

1 Alipokuwa akiwaandikia Wakristo Waebrania, mtume Paulo aliwasihi: “Basi, kwa njia yake yeye, na tumpe Mungu dhabihu ya sifa daima, yaani, tunda la midomo iliungamayo jina lake.” (Ebr. 13:15) Njia moja tunayoweza kufanya hivyo ni kwa kuunga mkono mipango ya utumishi wa shambani ya kundi letu. Njia nyingine yenye matokeo ya kumpa Mungu dhabihu ya sifa ni kwa kuchukua kila fursa kutoa ushuhuda wa vivi hivi.

2 Wakati wa utendaji wetu wa kila siku, walio wengi wetu tunashirikiana na watu wengine. Tukiwa macho kutambua fursa kisha tujitahidi, tunapaswa kuwa na uwezo wa kupanda mbegu nyingi za ukweli wa Ufalme kupitia ushuhuda wa vivi hivi. Huenda isihitaji zaidi ya maelezo mafupi au swali kuhusu hali au mahangaiko ya mahali penu ili kuanzisha mazungumzo ambayo yatafungua njia ya kutoa ushuhuda. Ikitegemea hali na itikio la mtu, huenda hata tukaweza kuangusha kichapo.

UWE UMEJITAYARISHA

3 Ushuhuda wa vivi hivi wenye matokeo unahitaji matayarisho ya mapema. Je! tuna nia ya kujitahidi? Tukichanganua yale ambayo tutafanya wakati wa siku, tufikirie watu ambao huenda tukakutana nao, na kufikiria yale ambayo tunaweza kusema ili kuanzisha mazungumzo, twapaswa kuwa tayari kiakili na kuona ikiwa rahisi zaidi kutoa ushuhuda wa vivi hivi. Hakikisha una trakti, magazeti, au vichapo vingine tayari ambavyo unaweza kuwatolea wenye kuitikia. Namna gani Biblia? Biblia ya mfukoni inatosha kwa urahisi katika kibeti au mfuko wa koti na inaweza kutumiwa fursa inapotokea. Je! kuna jambo jingine tunaloweza kufanya ili kuwa tumejitayarisha vizuri?

4 Tunapaswa kujua habari zinazohusu matukio ya karibuni yanayohusiana na unabii wa Biblia na kuwa tayari kuanzisha mazungumzo ya Biblia kwa mazungumzo ambayo yatavutia watu wenye njaa ya ukweli leo. Makala za “Kuutazama Ulimwengu” na “Muono-Ndani Juu ya Habari” zinazopatikana katika magazeti yetu ni vifaa vyenye thamani kuhusiana na jambo hili. Tukikumbuka habari hizi, tunaweza kuwa na uhakika katika kuanzisha mazungumzo ya mambo mengi yenye kuvutia sana.

ANZISHA MAZUNGUMZO

5 Karibu kila pindi tunapokutana na watu wengine inatoa fursa ya kutoa ushuhuda. Hata wahubiri ambao wamelazwa hospitalini wamechukua nafasi ya hali yao na wamekuwa wenye matokeo katika kuzungumza juu ya ukweli kwa madaktari, wauguzi, wafanya kazi wa hospitali, wageni, na wagonjwa wengine. Wahubiri wengine hutumia wakati wao wa mapumziko ya chakula cha mchana kazini au shuleni na wakati unaotumiwa kungojea mwadi. Fursa za kutoa ushuhuda zinaweza kutokea wakati wa kununua vitu, wakati wa likizo, au wakati wa kusafiri kwa basi, ndege, au gari-moshi. Wahubiri wengine wana matokeo katika kutoa ushuhuda wa vivi hivi katika makao yao wenyewe kwa watu wenye kuuza vitu, wenye kuleta vitu, majirani, watu wa ukoo, na wengineo wanaowatembelea.—Ona Kitabu cha Mwaka 1970 (Kiingereza), kurasa 97-8, 231-2, na 263-4.

6 “Ujitoaji Kimungu” Mikusanyiko ya Wilaya inatutolea fursa nzuri za kutoa ushuhuda wa vivi hivi. Baji za shavu la koti mara nyingi husukuma watu waulize sisi ni nani na tunakwenda wapi. Bila shaka, tunaweza kuanzisha mazungumzo kwa kuwaambia watu kwamba sisi ni wajumbe wa mkusanyiko na kueleza kwa nini tunahudhuria. Tunaponunua petroli, kula katika mikahawa, katika hoteli, au tunapoenda kununua vitu, au tunapopunga hewa tu, tunapaswa kutafuta njia zinazofaa kutoa ushuhuda wa vivi hivi.—Mhu. 11:6.

7 Uthamini wa ukweli wenye kutoka moyoni na kujua uharaka wa nyakati zetu unapasa utuchochee tuchukue kila fursa kushiriki pamoja na wengine ujumbe wa ajabu wa tumaini tulio nao. Na tuendelee kuchukua kila fursa kupanda mbegu za ukweli wa Ufalme kwa kutoa ushuhuda wa vivi hivi.—Mt. 24:14.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki